Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mrt makala 32
  • Jilinde Dhidi ya Habari za Uwongo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jilinde Dhidi ya Habari za Uwongo
  • Habari Zaidi
  • Habari Zinazolingana
  • Watoto na Mitandao ya Kijamii—Sehemu ya 1: Je, Mtoto Wangu Atumie Mitandao ya Kijamii?
    Msaada kwa Ajili ya Familia
  • Mitandao ya Kijamii Inaniathirije?
    Vijana Huuliza
  • Jilinde Dhidi ya Habari za Uwongo
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
  • Je, Mitandao ya Kijamii Inamdhuru Mtoto Wako?​—⁠Biblia Inaweza Kuwasaidiaje Wazazi?
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
Habari Zaidi
mrt makala 32
Mwanamume akichunguza habari kutoka vyanzo vingi mbalimbali.

Jilinde Dhidi ya Habari za Uwongo

Leo ni rahisi kupata habari kuliko wakati mwingine wowote, kutia ndani habari inayoweza kukusaidia kuwa salama na kudumisha afya nzuri. Hata hivyo, unapotafuta habari unapaswa kuwa mwangalifu dhidi ya habari za uwongo, kama vile:

  • Taarifa za habari zenye kupotosha

  • Ripoti za uwongo

  • Fununu zisizo na msingi

Kwa mfano, wakati wa janga la corona (COVID-19), katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa alionya dhidi ya habari za uwongo zinazosambazwa kuhusu janga hilo. Alisema hivi: “Kuna ongezeko la ushauri kuhusu tiba na mbinu za uwongo za kibiashara. Kuna uwongo mwingi unaosambazwa kwenye vyombo vya habari. Fununu zisizo na msingi zinaenezwa kwenye Intaneti. Chuki na ubaguzi unaenezwa kwa kasi dhidi ya watu na jamii mbalimbali.”

Bila shaka, habari za uwongo hazijaanza kuenezwa juzi. Hata hivyo, Biblia ilitabiri kwamba katika siku zetu, “watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mpaka ubaya zaidi, wakipotosha na kupotoshwa.” (2 Timotheo 3:1, 13) Sasa Intaneti inaturuhusu kupokea—na kueneza bila kukusudia—habari za uwongo kwa urahisi na haraka zaidi kuliko wakati mwingine wowote. Kwa sababu hiyo, barua-pepe yetu, mtandao wa kijamii, taarifa fupi za habari zinaweza kuwa na mambo mengi yaliyopotoshwa na kweli nusunusu.

Unaweza kufanya nini ili kujilinda dhidi ya habari za uwongo na fununu zisizo na msingi? Fikiria kanuni fulani za Biblia.

  • Mwanamume akifikiria kuhusu mambo ambayo ameona na kusikia.

    Usiamini kila kitu unachoona au kusikia

    Biblia inasema nini: “Mjinga huamini kila neno, lakini mwerevu hutafakari kila hatua.”—Methali 14:15.

    Tusipokuwa waangalifu tunaweza kudanganywa kwa urahisi. Kwa mfano, fikiria picha au video fupi zilizo na maandishi zinazoenezwa sana mtandaoni, hasa kupitia mitandao ya kijamii. Vitu hivyo, ambavyo vinajulikana kama meme, mara nyingi hukusudiwa kuwa vyenye kuchekesha. Hata hivyo, picha na video hizo fupi zinaweza kubadilishwa au kutumiwa kubadili maana ya maneno au tukio fulani kwa sababu hazionyeshi tukio lote. Hata watu wanaweza kutokeza video inayoonyesha watu halisi wakifanya au kusema mambo ambayo hawakuwahi kufanya au kusema.

    “Habari ya uwongo ambayo watafiti wamepata kwenye mitandao ya kijamii inahusisha picha na video zinazopotosha muktadha wa tukio halisi, kama vile meme.”—Axios Media.

    Jiulize: ‘Je, habari hii ni taarifa halisi au ni meme tu?’

  • Kioo cha kukuza mwonekano wa vitu.

    Chunguza chanzo na habari yenyewe

    Biblia inasema nini: “Hakikisheni mambo yote.”—1 Wathesalonike 5:21.

    Kabla ya kuamini hadithi fulani na kuisambaza, hata ikiwa inajulikana sana au imerudiwa katika habari, hakikisha ikiwa ni kweli. Jinsi gani?

    Chunguza chanzo chake kinategemeka kadiri gani. Kampuni za vyombo vya habari na mashirika mengine yanaweza kusimulia hadithi fulani kwa njia ambayo inaunga mkono masilahi yao wenyewe ya kibiashara au ya kisiasa. Linganisha kile unachoona katika kituo kimoja cha habari na vyanzo vingine. Nyakati nyingine, huenda marafiki wakashiriki habari za uwongo kupitia barua-pepe au mitandao ya kijamii. Hivyo, usiamini habari fulani isipokuwa uwe unaweza kuchunguza chanzo chake.

    Hakikisha kwamba habari yote ni ya karibuni na ni sahihi. Angalia tarehe, mambo hakika, na uthibitisho wenye nguvu unaounga mkono habari inayozungumziwa. Uwe mwangalifu hasa kuhusu habari tata inayozungumziwa kwa njia nyepesi au ikiwa ripoti yenyewe imekusudiwa kuamsha hisia.

    “Inaonekana kwamba siku hizi kuchunguza mambo hakika kumekuwa muhimu kama tu kunawa mikono.”—Sridhar Dharmapuri, Ofisa wa Ngazi za Juu wa Shirika la Usalama wa Chakula na Lishe la Umoja wa Mataifa.

    Jiulize: ‘Je, ripoti hii ya habari inaficha tofauti kati ya mambo hakika na maoni ya mtu au kutoa upande mmoja tu wa habari?’

  • Orodha.

    Ongozwa na mambo hakika, si mapendezi ya kibinafsi

    Biblia inasema nini: “Yeyote anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu.”—Methali 28:26.

    Kwa kawaida tuna mwelekeo wa kuamini habari inayounga mkono jambo tunalotaka kuamini. Mara nyingi kampuni za Intaneti huchanganua habari kuhusu mapendezi yetu na historia yetu ya utafutaji na kuzipatanisha na habari tunazotafuta au zinazojitokeza kwenye mitandao ya kijamii. Hata hivyo, si nyakati zote ambazo kile tunachotaka kusikia ndicho tunachohitaji kusikia.

    “Wanadamu wana uwezo wa kufikiri na kuchanganua mambo, lakini mara nyingi mapendezi, matarajio, woga, na nia yetu hubadili mambo na kufanya iwe rahisi zaidi kukubali kitu kuwa ni kweli maadamu kinaunga mkono tunachotaka kuamini.”—Peter Ditto, mwanasaikolojia wa jamii.

    Jiulize: ‘Je, ninaamini habari hii kwa sababu tu inasema ninachotaka kuamini?’

  • Habari ya uwongo ikitupwa kwenye takataka.

    Komesha kuenea kwa habari za uwongo

    Biblia inasema nini: “Usieneze habari za uwongo.”—Kutoka 23:1.

    Kumbuka kwamba habari unayowapitishia wengine ina uwezo wa kuathiri mawazo na matendo yao. Hata ikiwa unapitisha habari ya uwongo bila kukusudia, inaweza kutokeza madhara.

    “Sheria Na. 1 ni kupunguza mwendo, kutua, na kujiuliza, ʻNina uhakika kadiri gani kuhusu habari hii ili niwaeleze wengine?’ Ikiwa kila mtu angejiuliza swali hilo, kungekuwa na habari chache zaidi za uwongo mtandaoni.”— Peter Adams, naibu msimamizi wa Shirika la Kuwaelimisha Wanahabari.

    Jiulize: ‘Je, ninawaeleza wengine habari hii kwa sababu ninajua ni ya kweli?’

Ukweli kuhusu fununu zisizo na msingi

Shauna Bowes, mtafiti wa saikolojia, anasema hivi: “Fununu zisizo na msingi zinaathiri zaidi kufikiri na tabia za watu leo kuliko wakati mwingine wowote.” Yafuatayo ndiyo mambo unayohitaji kujua kuhusu fununu zisizo na msingi.

Fununu isiyo na msingi ni nini? Fununu isiyo na msingi [inayozungumziwa katika makala hii] ni dai la kwamba vikundi fulani vya kihalifu na vyenye nguvu vimepanga njama ya kutenda jambo fulani kubwa au lenye madhara.

Kwa nini fununu hizo ni hatari? Fununu zisizo na msingi zinaweza kuwafanya watu wasiamini vyanzo vinavyoaminika vya habari, na kuwafanya watu fulani wapuuze ushauri kuhusu afya au usalama. Fununu kama hizo huwachochea watu kuwa na ubaguzi au kutenda kwa jeuri kuelekea kikundi kinachohusishwa katika fununu hizo.

Kwa nini zinatumiwa sana? Kitabu Encyclopaedia Britannica kinasema kwamba fununu zisizo na msingi huongezeka wakati ambapo “watu wana wasiwasi mwingi, wamechanganyikiwa, au wanakabili hali ngumu” kama vile “wakati wa vita, mshuko wa kiuchumi, na baada ya misiba ya asili kama vile tsunami, matetemeko ya ardhi, na magonjwa ya kuenea (tandavu).” Katika pindi kama hizo zenye msukosuko, watu huamini fununu hizo zisizo na msingi kwa sababu zinaunga mkono mambo wanayoamini au zinawasaidia kuelewa kwa nini mambo mabaya yanatokea.

Biblia inaweza kukusaidiaje ujilinde dhidi ya fununu zisizo na msingi? Biblia inatoa ushauri unaofaa unaoweza kutusaidia kudhibiti wasiwasi wetu tunapokabili hali zenye mkazo. Inafunua chanzo halisi cha matatizo yaliyopo na pia jinsi matatizo hayo yatakavyotatuliwa. Ili ujifunze mengi zaidi, tazama video yenye kichwa Kwa Nini Ujifunze Biblia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki