Kiliniwezesha Kuhutubu Shuleni
Shule moja ya ufundi huko Ujerumani ina wanafunzi wengi kutoka nchi za kigeni. Wametoka nchi kama vile Afrika Kusini, Georgia, India, Lebanoni, Poland, Ufaransa, Ukrainia, Urusi, Vietnam, na Yugoslavia ya zamani.
Mwanafunzi mmoja anaandika hivi: “Kulipokuwa na nafasi ya kutoa hotuba, nilijitolea kufanya hivyo. Nilichagua kichwa: ‘Majibu Yanayotumika kwa Maswali Ambayo Vijana Huuliza,’ kilichotegemea kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi. Wanafunzi walivutiwa na vichwa vinavyozungumziwa katika kitabu hicho na mapendekezo mazuri ambayo kinatoa.
“Nilipomaliza, wanafunzi walionyesha uthamini kwa kupiga makofi kwa nguvu. Kwa kuwa wote wanajifunza lugha na wanaelewa Kiingereza vizuri, niliwaachia nakala 30 za Kiingereza za kitabu Vijana Huuliza, na pia nilimwachia mwalimu nakala yake katika Kijerumani.”
Katika siku zilizofuata, mwanafunzi huyo aliendeleza mazungumzo hayo na baadhi ya wanafunzi, nao walipendezwa. Aliwaachia vichapo vya ziada vinavyotegemea Biblia katika Kiarabu, Kibengali, Kigeorgia, Kihispania, Kipolishi, Kirusi, na Kivietnamu.
Labda unajua kijana ambaye angenufaika kwa kusoma kitabu Vijana Huuliza. Kati ya sura zake 39 kuna vichwa kama vile: “Naweza Kufanyaje Marafiki wa Kweli?,” “Vipi Juu ya Ngono Kabla ya Ndoa?,” na “Nijueje Kama Ni Upendo Halisi?” Unaweza kuomba kitabu hiki kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa hapa chini bila masharti.
□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.