“Sikujua Kwamba Mungu ana Jina”
◼ Mwanamke mmoja alisema hivyo baada ya kusoma kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Aliongezea hivi: “Lakini ni jambo linalopatana na akili kwamba Mungu ana jina. Nilipotafuta jina la Mungu katika Biblia yangu, nililipata!” Alieleza hivi: “Sijawahi kusoma kitabu cha Biblia kinachotoa msaada na kilicho rahisi kuelewa kama hicho.”
Mbali na kuonyesha kwamba lilikuwa kusudi la awali la Mungu dunia iwe paradiso, kitabu Biblia Inafundisha kinaonyesha wazi jinsi kusudi hilo litakavyotimizwa. Kitabu hicho kinafunua jukumu muhimu la Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, katika kutimiza kusudi hilo. Kinaeleza ufafanuzi wa Biblia kuhusu sababu inayotufanya tuzeeke na kufa, kwa nini Mungu anaruhusu kuteseka, na jinsi Ufalme wa Mungu utakavyoleta kitulizo kwa wote wanaoteseka.
Ingawa kitabu Biblia Inafundisha kimekuwapo kwa miaka mitatu tu, tayari nakala zaidi ya milioni 79 zimechapishwa katika lugha 220. Unaweza kuomba kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
❑ Bila masharti, ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa hapa.
❑ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.