Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 11/12 kur. 18-20
  • Ninaweza Kukabilianaje na Mkazo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ninaweza Kukabilianaje na Mkazo?
  • Amkeni!—2012
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Punguza Mzigo wa Mkazo
  • Pata “Injini” Yenye Nguvu Zaidi
  • Ninaweza Kukabiliana Jinsi Gani na Mikazo Shuleni?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
  • Ninaweza Kukabilianaje na Mfadhaiko Shuleni?
    Amkeni!—2008
  • Jinsi ya Kudhibiti Mfadhaiko
    Amkeni!—2010
  • Unaweza Kukabiliana na Mfadhaiko!
    Amkeni!—2005
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2012
g 11/12 kur. 18-20

Vijana Huuliza

Ninaweza Kukabilianaje na Mkazo?

Wewe una mkazo kiasi gani?

  • Nimelemewa na mkazo

  • Nina mkazo mwingi sana

  • Ninaweza kukabiliana na mkazo wangu

  • Mimi sina mkazo wowote

KUSHUGHULIKA na mkazo ni kama kuvuta kontena nzito. Gari kubwa la kuvuta mizigo linaweza kuvuta kontena hilo kwa urahisi. Lakini gari dogo haliwezi. Kujaribu kuvuta mzigo kama huo kwa kutumia gari dogo kunaweza kuharibu injini ya gari hilo, hata ikiwa hutafika mbali sana. Ndivyo hali ilivyo ikiwa “injini” yako, yaani, mwili wako, utalemewa na mkazo.

Je, kuna tumaini? Ndiyo! Ili usilemewe na mkazo utahitaji ama kupunguza mzigo wako ama kutafuta “injini” yenye nguvu zaidi. Hata hivyo, inawezekana kufanya mambo yote mawili. Acheni tuone.

Punguza Mzigo wa Mkazo

TATIZO: Kuwa na mambo mengi mno ya kufanya.

“Watu huniomba niwasaidie kufanya mambo au niende kwenye tafrija wakati ambapo nina mmbo ya kufanya. Mimi hushindwa kukataa.”​—Karina.a

SULUHISHO: Jifunze kukataa.

“Wenye kiasi wana hekima,” inasema Biblia. (Methali 11:2) Kuwa na kiasi, yaani, kutambua mipaka yako kutakusaidia kusema hapana mzigo unapokuwa mkubwa kuliko unavyoweza kubeba.

Bila shaka, si kila jambo utakaloweza kukataa kufanya—kwa mfano, wazazi wako wakikukumbusha kwamba unapaswa kufanya kazi za nyumbani! Lakini ikiwa utakubali kila mtu akuongezee mzigo, mwishowe utakulemea. Hata magari makubwa ya mizigo yana kiwango hususa cha mzigo ambacho yanaweza kubeba.

Dokezo: Ikiwa ni vigumu kwako kukataa waziwazi jaribu kusema, “Nitakueleza baadaye.” kabla Kisha, ya kumjibu mtu huyo kwanza jiulize, ‘Je, kweli nina muda na nguvu za kutosha kufanya kazi hiyo?’

TATIZO: Kuahirisha mambo.

“Ikiwa kazi inaonekana kuwa ngumu, mimi huiacha kwanza. Lakini baadaye mimi huwa na wasiwasi kwa sababu bado lazima nitaifanya. Wakati ambapo nahitaji kuifanya lazima niharakishe ili niimalize kwa wakati, na hilo hunipa mkazo.”​—Serena.

SULUHISHO: Anza mara moja—hata kama hutamaliza wakati huo.

Biblia inashauri hivi: “Msiwe wavivu katika kazi zenu.” (Waroma 12:11) Kufanya kazi ngumu kunachosha, sasa kwa nini ujiongezee mkazo kwa kuiahirisha? Hata ukiiahirisha, utalazimika tu kuifanya!

Ili kupata kichocheo, andika orodha ya mambo unayopaswa kufanya. Panga kufanya kazi kubwa hatua hatua. kwa “Ninapenda kuandika orodha,” anasema msichana anayeitwa Carol. “Kwa kawaida mimi huorodhesha mambo ambayo sipendi kwanza, kisha kadiri ninavyoyafuta mambo rahisi ndiyo yanayosalia. Baada ya muda, unabaki na mambo ambayo wewe hufurahia kuyafanya.”

Dokezo: Ikiwa ni vigumu kwako kuanza kazi fulani, weka kengele ya saa ilie baada ya dakika 10 au 15 kisha anza kazi hiyo mara moja. Wakati ambapo kengele ya saa italia, utakuwa umefanya kazi kwa dakika 10 au 15. Sasa kwa kuwa tayari umeanza kazi hiyo, huenda ukaona kuwa ni rahisi kuikamilisha.

Weka chumba chako kikiwa nadhifu! Ikiwa itakubidi kutafuta kazi zako za shule au nguo safi kwenye rundo kubwa la vitu vilivyowekwa ovyoovyo, hilo litakuongezea mkazo. Ili kupunguza kuwa na kazi nyingi asubuhi, tumia dakika tano kuacha kila kitu kikiwa nadhifu kabla ya kwenda kulala.

Pata “Injini” Yenye Nguvu Zaidi

[Picha katika ukurasa wa 20]

Hakikisha kwamba “injini” yako inaweza kubeba mzigo wako

Tunza mwili wako.

Wataalamu wanakubali kwamba kula chakula chenye lishe, kufanya mazoezi kwa ukawaida, na kulala vya kutosha kutakusaidia kutimiza mengi.b Usiwe na wasiwasi—kutunza mwili wako si jambo gumu. Mambo machache yatakusaidia kufanikiwa. Kwa mfano kuhusu usingizi, jaribu kufanya mambo yafuatayo.

  1. Lala vya kutosha. Panga saa hususa wa kulala na kuamka, hasa katika siku za kazi au shule.

  2. Punguza shughuli kabla ya saa za kulala kufika. Usifanye mazoezi saa tatu kabla ya wakati wa kulala, na epuka kula vyakula vingi na vinywaji vyenye kafeini wakati wa kulala unapokaribia.

  3. Wakati wa kulala unapofika, hakikisha kwamba hakuna kelele na mwangaza katika chumba chako cha kulala, na jaribu kufanya chumba kiwe chenye kustarehesha.

Omba msaada.

Usisite kuomba msaada kutoka kwa wazazi au rafiki zako. Je, kuna faida ya kufanya hivyo? Ndiyo, kwa kuwa utafiti unaonyesha kwamba msaada wa kihisia unasaidia kupunguza mkazo ambao unaweza kudhuru moyo, mishipa ya damu, na mfumo wa kinga.

Utafiti huo unakubaliana na maneno ya Biblia, ambayo yanasema: “Hangaiko katika moyo wa mtu huufanya uiname, lakini neno jema huufanya ushangilie.” (Methali 12:25) Wakati “hangaiko” linapokulemea, marafiki wa kweli wanaweza kusema “neno jema” lenye kutia moyo, ambalo huenda ndilo unalohitaji ili kukabiliana na mkazo.

Je, bado unahitaji msaada ili kukabiliana na mkazo? Ona sura zifuatazo kwenye kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1 na 2, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

BUKU LA 1

  • Sura ya 18: Ninaweza Kukabiliana Jinsi Gani na Mikazo Shuleni?

  • Sura ya 21: Ninaweza Kutumia Jinsi Gani Wakati Wangu Vizuri?

BUKU LA 2

  • Sura ya 26: Ninaweza Kudhibiti Jinsi Gani Hisia Zangu?

  • Sura ya 27: Kwa Nini Siridhiki?

Kuanzia toleo la Amkeni! la Januari 2013, makala za “Vijana Huuliza” zitapatikana tu kwenye Intaneti kwenye Tovuti ya www.jw.org/sw

a Baadhi ya majina yamebadilishwa

b Unaweza kupata madokezo kuhusu chakula na mazoezi, katika sura ya 10 ya kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza​—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

VIJANA WENZAKO WANASEMA NINI?

[Picha]

Patricia​—Ninapokuwa na mkazo, michezo kama vile kukimbia, kuendesha baiskeli au kufanya mazoezi ya mwili, hunisaidia kutulia. Pia, mimi huwaeleza wazazi wangu au rafiki yangu wa karibu hisia zangu​—kwa sababu ninawatumaini na wananielewa vizuri. Utegemezo wao hunisaidia sana.

[Picha]

Zachary​—Nimegundua kwamba nina tabia ya kuwa na wasiwasi kupita kiasi, jambo ambalo hufanya niwe na mkazo na kufanya mambo kuwa magumu. Kwa hiyo, mimi hujaribu kuona mambo kihalisi. Mimi hujiuliza, matatizo yangu ni makubwa kiasi gani yakilinganishwa na ya watu ambao hawana mahali pa kuishi wala chakula?

[Picha]

Gregory​—Jambo ambalo hunisaidia kukabiliana na mkazo ni ratiba ya kila siku. Ratiba hiyo hunisaidia kufanya mambo kwa utaratibu na kufahamu kila kitu ninachohitaji kufanya. Kwa njia hiyo, mimi hufanya mambo kwa wakati. Kwa upole na unyoofu ninaweza kukubali au kukataa majukumu zaidi kwa kutegemea muda wa ziada nilio nao.

[Mchoro katika ukurasa wa 18]

Hailey​—Ninapojua nina kazi za kufanya kesho, mimi hupanga ratiba usiku, na kuandika wakati ambao ninapaswa kuwa nimemaliza kufanya kila jambo nililopangia. Kwa mfano, ninaposafisha nyumba, ninapanga kwamba ninapaswa kuwa nimemaliza kusafisha jikoni baada ya muda fulani hususa, kisha nimalize kusafisha vyumba vya kulala baada ya saa mbili, na kadhalika. Kufanya hivyo hunisaidia sana!

MBONA USIWAULIZE WAZAZI WAKO?

Mnakabiliana na mkazo wa aina gani maishani mwenu? Mmeona ni njia gani inayofaa zaidi ya kukabiliana na mkazo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki