Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g21 Na. 1 uku. 14
  • Ujuzi Utakaotusaidia Kumkaribia Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ujuzi Utakaotusaidia Kumkaribia Mungu
  • Amkeni!—2021
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Muumba Wetu Ana Jina la Kibinafsi
  • Yehova Ni Mungu Mwenye Upendo
  • Yehova Ni Mungu Anayesamehe
  • Yehova Anatualika Tusali Kwake
  • ‘Endeleeni Kusameheana kwa Hiari’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Yehova—Mfano Bora wa Kusamehe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Ukweli Kumhusu Mungu
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Mungu Ni Nani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2021
g21 Na. 1 uku. 14

Ujuzi Utakaotusaidia Kumkaribia Mungu

Muumba wetu ana nguvu, lakini pia ana sifa nyingi zenye kupendeza. Na anataka tujifunze kumhusu na kumkaribia. (Yohana 17:3; Yakobo 4:8) Hiyo ndiyo sababu ametufunulia mambo mengi kujihusu.

Muumba Wetu Ana Jina la Kibinafsi

“Na watu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”​​—ZABURI 83:18.

Biblia inafundisha kwamba Yehova ndiye Mungu pekee wa kweli. Yeye ndiye Muumba wa ulimwengu na viumbe vyote. Yeye peke yake ndiye anayestahili kuabudiwa.—Ufunuo 4:11.

Yehova Ni Mungu Mwenye Upendo

Jina la Muumba wetu, Yehova, likiwa limeandikwa katika Kihindi, Kipunjabi, Kigujarati, Kitelugu, Kitamil, na Kiswahili.

“Mungu ni upendo.”​​—1 YOHANA 4:8.

Kupitia Biblia na uumbaji unaotuzunguka, Yehova amefunua sifa zake nyingi. Upendo ndiyo sifa yake kuu. Kila kitu anachofanya kinaongozwa na upendo. Kadiri tunavyoendelea kujifunza kumhusu Yehova, ndivyo tunavyoendelea kumpenda.

Yehova Ni Mungu Anayesamehe

“Wewe ni Mungu uliye tayari kusamehe.”​​—NEHEMIA 9:17.

Yehova anajua kwamba sisi si wakamilifu. Kwa hiyo, yuko tayari kutusamehe. Tukimwomba msamaha na kujitahidi kabisa kuacha kufanya mambo mabaya, atatusamehe na hatatuhukumu kwa sababu ya makosa tuliyofanya zamani.​—Zaburi 103:12, 13.

Yehova Anatualika Tusali Kwake

“Yehova yuko karibu na wote wanaomwitia . . . Husikia kilio chao cha kuomba msaada.”​​—ZABURI 145:18, 19.

Hatuhitaji kufuata desturi fulani au kutumia sanamu au kitu kingine chochote ili kumwabudu Yehova. Anasikiliza sala zetu kama wazazi wenye upendo wanavyowasikiliza watoto wao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki