Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Falsafa
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Zinachochewa na roho waovu: “Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.” (1 Yoh. 5:19) “Yeye anayeitwa Ibilisi na Shetani, anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa.” (Ufu. 12:9) “Wakati fulani mlitembea ndani yake kulingana na mfumo wa mambo wa ulimwengu huu, kulingana na mtawala wa mamlaka ya hewa, roho ambayo sasa hutenda katika wana wa kutotii.” (Efe. 2:2) (Falsafa zinazowatia watu moyo wasitii matakwa mazuri na manyoofu ya Mungu zinaonyesha uvutano huo. Si ajabu kwamba, kama historia inavyothibitisha, mara nyingi falsafa na mipango ya wanadamu imewaletea watu wengi huzuni.)

      Kwa nini ni jambo la busara kujifunza mafundisho ya Yesu Kristo badala ya falsafa za wanadamu?

      Kol. 1:15-17: “Yeye [Yesu Kristo] ndiye mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote; kwa sababu kwa njia yake vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani . . . Vitu vingine vyote vimeumbwa kupitia yeye na kwa ajili yake. Pia, yeye ni wa kabla ya vitu vingine vyote na kwa njia yake vitu vingine vyote vilifanywa kuwapo.” (Uhusiano wake wa karibu sana na Mungu unamwezesha atusaidie tujifunze kweli kumhusu Mungu. Zaidi ya hayo, akiwa yule ambaye vitu vingine vyote viliumbwa kupitia kwake, Yesu ana ujuzi kamili wa ulimwengu mzima ulioumbwa. Hakuna mwanafalsafa yeyote anayeweza kutupa msaada huo.)

      Kol. 1:19, 20: “Mungu aliona ni vema ujazo wote ukae katika yeye [Yesu Kristo], na kupitia yeye apatanishe tena kwake mwenyewe vitu vingine vyote kwa kufanya amani kupitia damu aliyomwaga juu ya mti wa mateso.” (Kwa hiyo, Yesu Kristo ndiye yule ambaye kupitia kwake Mungu amekusudia kuupatanisha pamoja Naye tena uumbaji wote. Mungu pia amemkabidhi Yesu utawala juu ya dunia yote, kama inavyoonyeshwa katika Danieli 7:13, 14. Kwa hiyo, matazamio yetu ya kupata uzima wakati ujao yanategemea kumjua yeye na kukubali mafundisho yake.)

      Kol. 2:8: “Mjihadhari: labda kuna mtu ambaye atawachukua ninyi kama windo lake kupitia falsafa na udanganyifu mtupu kulingana na pokeo la wanadamu, kulingana na mambo ya msingi ya ulimwengu na si kulingana na Kristo.” (Lingekuwa kosa baya kama nini kuchagua falsafa hiyo yenye udanganyifu ya wanadamu badala ya kujipatia hekima ya kweli tukiwa wanafunzi wa Yesu Kristo, ambaye ndiye mtu wa pili kwa ukuu ulimwenguni, wa pili kutoka kwa Mungu mwenyewe!)

      Mungu anaionaje “hekima” inayotokana na falsafa ya wanadamu?

      1 Kor. 1:19-25: “Imeandikwa: ‘Nitaiangamiza hekima ya watu wenye hekima, na akili ya watu wenye akili nitaitupa kando.’ Yuko wapi mtu mwenye hekima? Yuko wapi mwandishi? Yuko wapi mwenye kubishania maneno wa mfumo huu wa mambo? Je, Mungu hakuifanya hekima ya ulimwengu iwe upumbavu? Maana, kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kupitia hekima yake haukuja kumjua Mungu, Mungu aliona vema kupitia upumbavu wa linalohubiriwa awaokoe wale wanaoamini. . . . Kwa sababu kitu kipumbavu [machoni pa watu wa ulimwengu] cha Mungu ni chenye hekima zaidi kuliko wanadamu, na kitu dhaifu [machoni pa watu wa ulimwengu] cha Mungu ni chenye nguvu zaidi kuliko wanadamu.” (Maoni hayo ya Mungu hakika si ya kuonea wala hayakosi kupatana na akili. Yeye ameandaa katika Biblia, ambayo ni kitabu kinachoenezwa zaidi ulimwenguni, taarifa iliyo wazi kuhusu kusudi lake. Amewatuma mashahidi wake wawatangazie wote wanaotaka kusikiliza. Ni upumbavu kama nini kwa kiumbe chochote kufikiri kwamba kina hekima nyingi kuliko Mungu!)

  • Fidia
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Fidia

      Maana: Bei inayolipwa ili kurudisha au kuachilia huru kitu fulani kutoka katika wajibu fulani au hali mbaya. Bei ya fidia iliyo muhimu zaidi kuliko zote ni damu ya Yesu Kristo iliyomwagwa. Kwa kulipa thamani ya fidia hiyo mbinguni, Yesu aliwafungulia njia wazao wa Adamu ili wakombolewe kutoka katika dhambi na kifo ambavyo sisi sote tumerithi kwa sababu ya dhambi ya babu yetu Adamu.

      Kifo cha Yesu Kristo kilitofautianaje na cha wale wengine waliouawa kwa sababu ya imani yao?

      Yesu alikuwa mwanadamu mkamilifu. Alizaliwa bila dosari ya dhambi na alidumisha ukamilifu huo katika maisha yake yote. “Yeye hakufanya dhambi.” Yeye alikuwa “asiye na unajisi, aliyetengwa kutoka kwa watenda-dhambi.”—1 Pet. 2:22; Ebr. 7:26.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki