-
UponyajiKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Unaweza kujibu hivi: ‘Yeyote ambaye haamini kwamba Mungu ana uwezo wa kuponya haiamini Biblia. Lakini nina shaka ikiwa watu wanafanya uponyaji kwa njia iliyo sawa leo.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Acha nikusomee andiko moja, na uone ikiwa unatambua zoea lililo tofauti sana leo. (Mt. 10:7, 8) . . . Je, unatambua pia jambo fulani hapa ambalo Yesu alisema wanafunzi wake wangeweza kufanya lakini ambalo waponyaji wa leo wameshindwa kulifanya? (Hawawezi kufufua wafu.)’ (2) ‘Sisi hatuwahukumu watu wengine, lakini ona kwamba andiko la Mathayo 24:24 linataja jambo fulani tunalohitaji kujihadhari nalo.’
Au unaweza kusema: ‘Ninaamini hakika kwamba yale ambayo Biblia inasema kuhusu uponyaji ni ya kweli. Lakini uponyaji wowote unaofanywa katika mfumo huu wa mambo ni wa faida za muda mfupi tu, sivyo? Mwishowe sisi sote hufa. Je, kutakuwa na wakati ambapo kila mtu anayeishi atakuwa na afya njema naye hatakufa kamwe? (Ufu. 21:3, 4)’
-
-
Urithi wa UpapaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Urithi wa Upapa
Maana: Fundisho la kwamba wale mitume 12 wana warithi ambao wamepokea mamlaka iliyopitishwa kutoka kwa Mungu. Katika Kanisa Katoliki, inasemekana kwamba maaskofu wakiwa kikundi ni warithi wa mitume, na papa anadaiwa kuwa mrithi wa Petro. Inaaminiwa kwamba mapapa Wakatoliki wanamfuata Petro, ambaye inasemwa kwamba Kristo alimpa ukuu wa mamlaka juu ya Kanisa zima, wakichukua cheo cha Petro na kutimiza kazi zake. Hilo si fundisho la Biblia.
Je, Petro ndiye “mwamba” ambao kanisa lilijengwa juu yake?
Mt. 16:18, UV: “Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.” (Katika muktadha [mstari wa 13 na wa 20], ona kwamba mazungumzo hayo yanakazia utambulisho wa Yesu.)
Mitume Petro na Paulo walielewa nani kuwa “mwamba,” lile “jiwe la pembeni”?
Mdo. 4:8-11, UV: “Ndipo Petro, akijaa Roho Mtakatifu, akawaambia, Enyi wakubwa wa watu na wazee . . . kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulibisha, na Mungu akamfufua katika wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu. Yeye ndiye jiwe lile lililodharauliwa na ninyi waashi, nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la pembeni.”
1 Pet. 2:4-8, UV: “Mmwendee yeye [Bwana Yesu Kristo], . . . ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo. Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, na kila amwaminiye hatatahayarika. Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini, jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni. Tena, jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha.”
Efe. 2:20, UV: “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.”
Agustino (ambaye Kanisa Katoliki lilimwona kuwa mtakatifu) aliamini nini?
“Katika kipindi hicho cha upadre wangu, mimi pia niliandika kitabu dhidi ya barua ya Donato . . . Kwenye fungu fulani katika kitabu hicho, nilisema hivi kumhusu Mtume Petro: ‘Kanisa lilijengwa juu yake kana kwamba juu ya mwamba.’ . . . Lakini najua kwamba baadaye, nilieleza mara nyingi yale ambayo Bwana alisema: ‘Wewe ni Petro, na juu ya mwamba huu nitajenga Kanisa langu,’ kwamba ieleweke kuwa lilijengwa juu ya Yule ambaye Petro alimkiri akisema: ‘Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai,’ na kwa hiyo Petro, aliyeitwa jina la mwamba huo, aliwakilisha mtu wa Kanisa lililojengwa juu ya mwamba huo, na amepokea ‘funguo za ufalme wa mbinguni.’ Kwa maana aliambiwa, ‘Wewe ni Petro’ wala hakuambiwa, ‘Wewe ndiwe mwamba.’ Lakini, kwa kumkiri yule ambaye Kanisa lote pia linamkiri, ‘mwamba ulikuwa Kristo,’ Simoni aliitwa Petro.”—The Fathers of the Church—Saint Augustine, the Retractations (Washington, D.C.; 1968), kilichotafsiriwa na Mary I. Bogan, Buku 1, uku. 90.
Je, mitume wengine walimwona Petro kuwa mkuu kati yao?
Luka 22:24-26, UV: “Yakatokea mashindano kati yao, kwamba ni nani anayehesabiwa kuwa mkubwa. Akawaambia, Wafalme wa Mataifa hutawala, na wenye mamlaka juu yao huitwa Wenye fadhili; lakini kwenu ninyi sivyo; bali aliye mkubwa kwenu na awe kama aliye mdogo; na mwenye kuongoza kama yule atumikaye.” (Ikiwa Petro ndiye aliyekuwa “mwamba,” je, yeyote angeuliza ni yupi kati yao anayepaswa ‘kuhesabiwa kuwa mkubwa’?)
Kwa kuwa Yesu Kristo, aliye kichwa cha kutaniko, yu hai, je, anahitaji kuwa na warithi?
Ebr. 7:23-25, UV: “Tena wale walifanywa makuhani wengi [katika Israeli], kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae; bali yeye [Yesu Kristo], kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka. Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye.”
Rom. 6:9, UV: “Tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena.”
Efe. 5:23, UV: “Kristo naye ni kichwa cha Kanisa.”
“Funguo” alizokabidhiwa Petro zilikuwa nini?
Mt. 16:19, UV: “Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.”
Katika Ufunuo, Yesu alitaja ufunguo wa mfano ambao yeye mwenyewe anautumia kuwafungulia wanadamu mapendeleo na nafasi
Ufu. 3:7, 8, UV: “Haya ndiyo anenayo yeye aliye mtakatifu, aliye wa kweli, aliye na ufunguo wa Daudi, yeye mwenye kufungua wala hapana afungaye, naye afunga wala hapana afunguaye. . . . Nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako.”
Petro alizitumia “funguo” alizokabidhiwa ili kuwafungulia (Wayahudi, Wasamaria, Mataifa) nafasi ya kupokea roho ya Mungu wakiwa na tumaini la kuingia katika Ufalme wa mbinguni
Mdo. 2:14-39, UV: “Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu . . . Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo. Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.”
-