Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Utatu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Pendekezo lingine: ‘Nimeona kwamba watu wanaposema kuhusu Utatu, wana maoni mbalimbali kuhusu fundisho hilo. Labda ninaweza kulijibu swali lako vizuri zaidi nikijua unachomaanisha.’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Asante kwa maelezo hayo. Lakini mambo ninayoamini ni yale tu ambayo Biblia hufundisha. Je, umewahi kuona neno “Utatu” katika Biblia? . . . (Rejelea konkodansi katika Biblia yako.) Lakini je, Kristo anatajwa katika Biblia? . . . Ndiyo, nasi tunamwamini. Ona hapa katika konkodansi chini ya “Kristo” kwamba mojawapo ya marejeo ni andiko la Mathayo 16:16. (Lisome.) Hilo ndilo ninaloamini.’

      Au unaweza kujibu hivi: (ikiwa mtu anataja kihususa andiko la Yohana 1:1): ‘Naujua mstari huo. Tafsiri fulani za Biblia husema kwamba Yesu ni “Mungu,” na nyingine husema kwamba yeye ni “mungu.” Kwa nini hivyo?’ (1) ‘Je, labda ni kwa sababu mstari unaofuata unasema kwamba yeye alikuwa “pamoja na Mungu”?’ (2) ‘Je, labda pia ni kwa sababu ya yale yanayopatikana hapa katika Yohana 1:18?’ (3) ‘Je, umewahi kujiuliza ikiwa Yesu mwenyewe humwabudu mwingine akiwa Mungu? (Yoh. 20:17)’

      ‘Je, unaamini kwamba Kristo ni mungu?’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Ndiyo, bila shaka naamini. Lakini labda maoni yangu ni tofauti na yako unaposema “Kristo ni mungu.”’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Kwa nini nasema hivyo? Katika andiko la Isaya 9:6 Yesu Kristo anaitwa “Mungu Mwenye Nguvu,” lakini Baba yake peke yake ndiye anayeitwa Mungu Mweza-Yote katika Biblia.’ (2) ‘Na ona kwamba katika Yohana 17:3 Yesu anamwita Baba yake kuwa “Mungu wa pekee wa kweli.” Kwa hiyo, Yesu ni mrudisho tu wa utukufu wa Mungu wa kweli.’ (3) ‘Tunapaswa kufanya nini ili tumpendeze Mungu? (Yoh. 4:23, 24)’

  • Uumbaji
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Uumbaji

      Maana: Uumbaji, kama unavyoelezwa katika Biblia, humaanisha kwamba Mungu Mweza-Yote aliubuni na kuutokeza ulimwengu, kutia ndani watu wengine wa kiroho na aina zote za msingi za viumbe vilivyo duniani.

      Katika ulimwengu huu wa kisasa, wa kisayansi, je, ni jambo linalopatana na akili kuamini uumbaji?

      “Sheria za asili za ulimwengu ni sahihi sana hivi kwamba si vigumu kutengeneza vyombo vya angani viruke mpaka mwezini na tunaweza kupima kwa usahihi safari yake hata kwa sehemu ya sekunde. Lazima sheria hizo ziliwekwa na mtu fulani.”—Akasema Wernher von Braun, aliyehusika sana katika kuwatuma wanaanga wa Marekani mwezini.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki