Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Roho ya Ulimwengu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Shetani alisitawisha tamaa hiyo ndani ya Hawa, akamshawishi afanye jambo lililoharibu uhusiano wake na Mungu. (Mwa. 3:6; 1 Yoh. 2:16) Yesu alikataa kwa uthabiti kishawishi cha namna hiyo. (Mt. 4:8-10) Wale wanaotaka kumpendeza Yehova wanahitaji kujilinda wasije wakaruhusu ulimwengu wa kibiashara usitawishe roho kama hiyo ndani yao. Watu wanaonaswa na mtego huo hupata huzuni nyingi na kuangamia kiroho.—Mt. 13:22; 1 Tim. 6:7-10.

      Mtu kujionyesha mali zake na mambo yanayodhaniwa kuwa mafanikio

      Zoea hilo, pia, “hutokana na ulimwengu” na wale wanaokuwa watumishi wa Mungu wanahitaji kuliacha kabisa. (1 Yoh. 2:16) Linatokana na kiburi, na badala ya kujenga wengine kiroho, huwawekea vishawishi vya vitu vya kimwili na miradi ya kupata mafanikio ya kilimwengu.—Rom. 15:2.

      Mtu kuonyesha hisia zake kwa kutumia matukano na matendo ya jeuri

      Hayo ni “matendo ya mwili” ambayo watu wengi wanapaswa kupigana sana nayo. Wakiwa na imani ya kweli na msaada wa roho ya Mungu, wanaweza kuushinda ulimwengu badala ya kuacha roho yake iwatawale.—Gal. 5:19, 20, 22, 23; Efe. 4:31; 1 Kor. 13:4-8; 1 Yoh. 5:4.

      Mtu kuutumaini na kuutegemea uwezo wa wanadamu kutatua mahangaiko yake

      Mtu wa kimwili huona kwamba yale anayoweza kuona na kugusa ndiyo mambo muhimu kikweli. Matumaini na mahangaiko yake hutegemea ahadi na vitisho vya wanadamu wengine. Yeye huwategemea wanadamu wanaotawala wamsaidie, naye hukata tamaa wanaposhindwa. (Zab. 146:3, 4; Isa. 8:12, 13) Kwa maoni yake, hakuna uzima mwingine. Hatari ya kifo humfanya kuwa mtumwa kwa urahisi. (Kwa kutofautisha, ona Mathayo 10:28; Waebrania 2:14, 15.) Lakini nguvu mpya huendesha akili za watu wanaopata kumjua Yehova, wale wanaojaza ahadi zake katika akili na mioyo yao, na wanaojifunza kumwomba msaada kila wakati wanapokuwa na uhitaji.—Efe. 4:23, 24; Zab. 46:1; 68:19.

      Kuwapa wanadamu na vitu heshima ya ibada ambayo ni haki ya Mungu

      “Mungu wa mfumo huu wa mambo,” Shetani Ibilisi, huchochea matendo yote mbalimbali ambayo hupotosha mwelekeo wa ibada ambao Mungu alimpa mwanadamu. (2 Kor. 4:4) Watawala fulani wametendewa kama miungu. (Mdo. 12:21-23) Mamilioni ya watu husujudia sanamu. Mamilioni zaidi huwatukuza waigizaji na wanamichezo mashuhuri. Mara nyingi sherehe huwapa wanadamu fulani heshima wasiyostahili. Roho hii imeenea sana hivi kwamba wale wanaompenda Yehova kikweli na wanaotaka kumtolea ibada ya pekee wanahitaji kukaa macho kila siku ili wajiepushe na uvutano wa roho hiyo.

  • Sabato
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Sabato

      Maana: Neno Sabato limetokana na neno la Kiebrania sha·vathʹ, linalomaanisha “pumzika, koma, acha.” Mfumo wa sabato ulioandikwa katika Sheria ya Musa ulitia ndani siku ya Sabato ya kila juma, siku kadhaa za ziada zilizotajwa waziwazi katika kila mwaka, mwaka wa saba, na mwaka wa hamsini. Sabato ya kila juma ya Wayahudi, siku ya saba ya juma lao la kalenda, inaanza wakati wa kutua kwa jua siku ya Ijumaa mpaka kutua kwa jua siku ya Jumamosi. Watu wengi wanaojiita Wakristo wameshika tangu zamani Jumapili kuwa siku yao ya pumziko na ya ibada; wengine wameshikamana na siku iliyowekwa kando katika kalenda ya Kiyahudi.

      Je, Wakristo wana wajibu wa kushika siku ya sabato ya kila juma?

      Kut. 31:16, 17: “Wana wa Israeli lazima waishike sabato, ili kuitimiza sabato katika vizazi vyao. Ni agano mpaka wakati usio na kipimo [“agano la milele,” UV]. Kati yangu na wana wa Israeli ni ishara mpaka wakati usio na kipimo.” (Ona kwamba kushika sabato kulikuwa ishara kati ya Yehova na Israeli; haingekuwa hivyo ikiwa watu wengine wote wangekuwa na wajibu wa kushika Sabato. Neno la Kiebrania lililotafsiriwa “milele” katika UV ni ‛oh·lamʹ, ambalo kwa msingi linamaanisha kipindi cha wakati ambacho, kwa sasa, hakina kipimo au kimefichwa lakini ni cha muda mrefu. Hicho kinaweza kumaanisha milele, lakini si lazima kiwe hivyo. Katika Hesabu 25:13 neno lilelile la Kiebrania linatumiwa kuhusu ukuhani, ambao baadaye ulikoma, kulingana na Waebrania 7:12.)

      Rom. 10:4: “Kristo ndiye mwisho wa Sheria, ili kila mtu anayeonyesha imani awe na uadilifu.” (Kushika sabato kulikuwa sehemu ya Sheria hiyo. Mungu alimtumia Kristo kuikomesha Sheria hiyo. Kupata msimamo wenye uadilifu mbele za Mungu kunategemea imani katika Kristo, wala si kushika sabato ya kila juma.) (Ona pia Wagalatia 4:9-11; Waefeso 2:13-16)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki