Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ibada ya Mababu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Yoh. 4:23, 24: “Saa inakuja, nayo ipo sasa, wakati ambapo waabudu wa kweli watamwabudu Baba kwa roho na kweli, kwa maana, kwa kweli, Baba anawatafuta watu wa namna hiyo wamwabudu. Mungu ni Roho, na wale wanaomwabudu lazima wamwabudu kwa roho na kweli.”

      Je, kuna tumaini kwamba wakati ujao washiriki wa familia, kutia ndani wale waliokufa, wataungana pamoja?

      Yoh. 5:28, 29: “Msistaajabie jambo hili, kwa sababu saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake na kutoka, wale waliotenda mambo mema kwenye ufufuo wa uzima, wale waliokuwa na zoea la kutenda mambo maovu kwenye ufufuo wa hukumu.”

  • Imani
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Imani

      Maana: “Imani ni tarajio lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa, uthibitisho ulio wazi wa mambo halisi ingawa hayaonekani.” (Ebr. 11:1) Imani ya kweli si kuamini jambo haraka-haraka bila uthibitisho mzuri au kwa sababu tu mtu anataka iwe hivyo. Ili mtu awe na imani ya kweli, anahitaji kuwa na ujuzi wa msingi, kujua uthibitisho, na pia kuthamini kutoka moyoni yale ambayo uthibitisho huo unaonyesha. Kwa hiyo, ijapokuwa haiwezekani kuwa na imani ya kweli bila ujuzi sahihi, Biblia inasema kwamba mtu huamini “kwa moyo.”—Rom. 10:10.

      Kwa nini watu wengi hawana imani?

      Imani ni tunda la roho ya Mungu, na kwa upendo Mungu huwapa roho yake wale wanaoitafuta. (Gal. 5:22; Luka 11:13) Basi watu wasio na imani hawaitafuti roho hiyo, au wanafanya hivyo kwa kusudi baya au wanapinga utendaji wa roho hiyo maishani mwao. Mambo mengi husababisha hali hiyo:

      Kutokuwa na ujuzi sahihi wa Biblia: Biblia imeandikwa kwa uongozi wa roho ya Mungu. (2 Tim. 3:16, 17; 2 Sam. 23:2) Mtu asipojifunza Biblia, hawezi kusitawisha imani ya kweli. Ijapokuwa huenda wanadini wakawa na Biblia, ikiwa wamefundishwa mafundisho ya wanadamu badala ya Neno la Mungu, watakosa imani ya kweli katika Mungu na kusudi lake. Ili kutatua matatizo ya maisha, inaelekea watayategemea mawazo yao wenyewe na yale ya wanadamu wengine.—Linganisha na Mathayo 15:3-9.

      Kukatishwa tamaa na dini: Watu wengi wamekatishwa tamaa na unafiki wa wafuasi wa makanisa yanayodai kuwa ya Kikristo ambao hudai kufundisha Neno la Mungu, lakini hawaishi kulingana na yale ambayo linasema. Wengine walikuwa wafuasi wa dini zisizo za Kikristo, lakini wakaona matunda mabaya ya matendo yake au wakaona kwamba imani zao hazikuwasaidia wakabiliane na matatizo ya maisha. Kwa kuwa hawana ujuzi sahihi wa Mungu wa kweli, watu hao hujitenga na kila jambo linalohusiana na dini.—Linganisha na Waroma 3:3, 4; Mathayo 7:21-23.

      Hawaelewi kwa nini Mungu anaruhusu uovu: Watu wengi hawaelewi kwa nini Mungu anaruhusu uovu na kwa hiyo wanamlaumu kwa mambo yote mabaya yanayotukia. Hawajui kwamba mwelekeo wa mwanadamu wa kufanya mabaya si mapenzi ya Mungu, bali unatokana na dhambi ya Adamu. (Rom. 5:12) Huenda wasijue kuhusu kuwapo kwa Shetani Ibilisi na uvutano wake juu ya mambo ya ulimwengu, hivyo wanamlaumu Mungu kwa mambo maovu yanayoendelezwa na Shetani. (1 Yoh. 5:19; Ufu. 12:12) Ikiwa kwa kadiri fulani wanajua mambo hayo, huenda wakaona kwamba Mungu anakawia kuchukua hatua, kwa sababu hawaelewi waziwazi lile suala la enzi kuu ya ulimwengu wote, nao hawafahamu kwamba subira ya Mungu mpaka wakati huu inawatolea nafasi isiyostahiliwa ya kupata wokovu. (Rom. 2:4; 2 Pet. 3:9) Pia, hawajui kikamili kwamba Mungu ameweka wakati wa kuwaharibu milele wote wanaotenda maovu.—Ufu. 22:10-12; 11:18; Hab. 2:3.

      Mambo muhimu maishani ni tamaa na maoni ya kimwili: Kwa ujumla, watu wasio na imani thabiti wamejitoa kufuatia mambo mengine. Wengine huenda wakasema kwamba wanaiamini Biblia lakini huenda hawajajifunza Biblia kwa ukamili au huenda wameshindwa kutafakari kwa uthamini mambo wanayosoma, sababu zinazotolewa, na jinsi inavyohusu maisha ya kila siku. (Linganisha na 1 Nyakati 28:9.) Watu wengine nao wameshindwa kujenga imani waliyokuwa nayo na, badala yake, wakaruhusu tamaa ya vitu visivyo vya uadilifu itawale moyo wao hata wakamwacha Mungu na njia zake.—Ebr. 3:12.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki