Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mashahidi wa Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Mtu Akisema—

      ‘Kwa nini hamshiriki kufanya ulimwengu (jumuiya) kuwa mahali bora pa kuishi?’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Bila shaka hali za jumuiya ni muhimu kwako na kwangu pia. Hebu nikuulize, Unafikiri ni tatizo gani linalopaswa kutatuliwa kwanza?’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Kwa nini unafikiri hilo limekuwa uhitaji mkubwa hivyo? . . . Bila shaka, hatua ya haraka kuhusu jambo hilo inaweza kunufaisha, lakini nina hakika utakubali kwamba tungependa kuona marekebisho ya kudumu. Hivyo ndivyo sisi Mashahidi wa Yehova tunavyoshughulikia jambo hilo. (Eleza tunayofanya ili kuwasaidia watu wafuate kanuni za Biblia katika maisha yao ili mtu binafsi afikie utatuzi wa jambo hilo; pia, jambo ambalo Ufalme wa Mungu utafanya, na kwa nini hilo litawatatulia wanadamu tatizo hilo daima.)’

      Au unaweza kusema: ‘(Baada ya kuzungumzia baadhi ya mambo yaliyo katika jibu linalotangulia . . . ) Watu fulani huchangia maendeleo ya jumuiya kwa kutoa pesa; wengine hufanya hivyo kwa kujitolea kutumikia. Mashahidi wa Yehova hufanya yote hayo. Acha nikueleze.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Ili mtu awe mmoja wa Mashahidi wa Yehova, ni lazima alipe kodi zake kwa unyoofu; kufanya hivyo husaidia serikali kupata pesa za kutoa huduma zinazohitajiwa.’ (2) ‘Sisi hufanya mengi zaidi, tunawatembelea watu nyumbani, na kuwatolea funzo la Biblia bila malipo. Wanapofahamu mambo ambayo Biblia inasema, wanajifunza kufuata kanuni za Biblia na hivyo wanakabiliana na matatizo yao.’

      Pia unaweza kusema: ‘Ninafurahi kwamba umetokeza jambo hilo. Watu wengi hawajawahi kuuliza ili wajue jambo ambalo Mashahidi wanafanya katika jumuiya. Bila shaka kuna njia nyingi za kutoa msaada.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Watu fulani hufanya hivyo kwa kuanzisha mashirika—hospitali, makao ya wazee, vituo vya kuwarekebishia waraibu wa dawa za kulevya, na kadhalika. Huenda wengine wakajitolea kwenda moja kwa moja kwenye nyumba za watu na kutoa msaada unaofaa kulingana na uwezo wao. Hivyo ndivyo Mashahidi wa Yehova wanavyofanya.’ (2) ‘Tumeona kwamba kuna jambo linaloweza kugeuza mtazamo mzima wa mtu kuhusu maisha, na jambo hilo ni kujua yale ambayo Biblia inasema kuwa ndilo kusudi halisi la maisha na yale yatakayotukia wakati ujao.’

      Pendekezo lingine: ‘Asante kwa kuuliza swali hilo. Tungependa kuona hali zikiwa bora, sivyo? Hebu nikuulize, Wewe unaonaje yale ambayo Yesu Kristo mwenyewe alifanya? Je, ungesema kwamba njia aliyotumia kuwasaidia watu ilikuwa nzuri? . . . Sisi hujaribu kufuata mfano wake.’

      ‘Wakristo wanapaswa kuwa mashahidi wa Yesu, wala si wa Yehova’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Hilo ni jambo lenye kupendeza. Na ni kweli kwamba tunapaswa kuwa mashahidi wa Yesu. Ndiyo sababu cheo cha Yesu katika kusudi la Mungu kinakaziwa katika vichapo vyetu. (Unaweza kutumia kitabu cha sasa au gazeti ili kuonyesha jambo hilo.) Lakini hapa pana jambo fulani ambalo huenda likawa jipya kwako. (Ufu. 1:5) . . . Yesu alikuwa “Shahidi Mwaminifu” wa nani? (Yoh. 5:43; 17:6) . . . Yesu alituwekea mfano tunaopaswa kufuata, sivyo?  . . . Kwa nini ni muhimu sana kumjua Yesu na Baba yake pia? (Yoh. 17:3)’

  • Mbingu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Mbingu

      Maana: Makao ya Yehova Mungu na viumbe roho waaminifu; makao yasiyoonekana kwa macho ya kibinadamu. Biblia pia inatumia neno “mbingu” katika maana nyingine mbalimbali; kwa mfano: kuwakilisha Mungu mwenyewe, tengenezo lake la viumbe roho waaminifu, hali ya kuwa na kibali cha Mungu, ulimwengu unaoonekana mbali na dunia, anga inayozunguka Dunia, serikali za kibinadamu chini ya utawala wa Shetani, na serikali mpya ya mbinguni yenye uadilifu ambayo Yesu Kristo pamoja na warithi-washirika wake wamepewa mamlaka na Yehova watawale ndani yake.

      Je, sisi sote tulikuwa katika makao ya kiroho kabla hatujazaliwa tukiwa wanadamu?

      Yoh. 8:23: “[Yesu Kristo alisema:] ‘Ninyi mnatoka kwenye makao ya chini; mimi ninatoka kwenye makao ya juu. Ninyi mnatoka katika ulimwengu huu; mimi sitoki katika ulimwengu huu.’” (Yesu alitoka katika makao ya kiroho. Lakini, kama Yesu alivyosema, wanadamu wengine hawakutoka huko.)

      Rom. 9:10-12: “Rebeka alipochukua mimba ya mapacha . . . Walipokuwa bado hawajazaliwa wala kufanya jambo lolote jema au baya, ili kusudi la Mungu kuhusu kuchagua liendelee kutegemea, si matendo, bali Yeye ambaye huita, Rebeka aliambiwa: ‘Mkubwa atakuwa mtumwa wa mdogo.’” (Bila shaka, ikiwa mapacha hao, Yakobo na Esau, walikuwa wameishi katika makao ya kiroho kwa hakika wangekuwa na sifa ya kuwa wema au wabaya ikitegemea mwenendo wao huko, sivyo? Lakini hawakuwa na sifa zozote za aina hiyo mpaka baada ya kuzaliwa kwao wakiwa wanadamu.)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki