Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Falsafa
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kol. 2:8: “Mjihadhari: labda kuna mtu ambaye atawachukua ninyi kama windo lake kupitia falsafa na udanganyifu mtupu kulingana na pokeo la wanadamu, kulingana na mambo ya msingi ya ulimwengu na si kulingana na Kristo.” (Lingekuwa kosa baya kama nini kuchagua falsafa hiyo yenye udanganyifu ya wanadamu badala ya kujipatia hekima ya kweli tukiwa wanafunzi wa Yesu Kristo, ambaye ndiye mtu wa pili kwa ukuu ulimwenguni, wa pili kutoka kwa Mungu mwenyewe!)

      Mungu anaionaje “hekima” inayotokana na falsafa ya wanadamu?

      1 Kor. 1:19-25: “Imeandikwa: ‘Nitaiangamiza hekima ya watu wenye hekima, na akili ya watu wenye akili nitaitupa kando.’ Yuko wapi mtu mwenye hekima? Yuko wapi mwandishi? Yuko wapi mwenye kubishania maneno wa mfumo huu wa mambo? Je, Mungu hakuifanya hekima ya ulimwengu iwe upumbavu? Maana, kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kupitia hekima yake haukuja kumjua Mungu, Mungu aliona vema kupitia upumbavu wa linalohubiriwa awaokoe wale wanaoamini. . . . Kwa sababu kitu kipumbavu [machoni pa watu wa ulimwengu] cha Mungu ni chenye hekima zaidi kuliko wanadamu, na kitu dhaifu [machoni pa watu wa ulimwengu] cha Mungu ni chenye nguvu zaidi kuliko wanadamu.” (Maoni hayo ya Mungu hakika si ya kuonea wala hayakosi kupatana na akili. Yeye ameandaa katika Biblia, ambayo ni kitabu kinachoenezwa zaidi ulimwenguni, taarifa iliyo wazi kuhusu kusudi lake. Amewatuma mashahidi wake wawatangazie wote wanaotaka kusikiliza. Ni upumbavu kama nini kwa kiumbe chochote kufikiri kwamba kina hekima nyingi kuliko Mungu!)

  • Fidia
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Fidia

      Maana: Bei inayolipwa ili kurudisha au kuachilia huru kitu fulani kutoka katika wajibu fulani au hali mbaya. Bei ya fidia iliyo muhimu zaidi kuliko zote ni damu ya Yesu Kristo iliyomwagwa. Kwa kulipa thamani ya fidia hiyo mbinguni, Yesu aliwafungulia njia wazao wa Adamu ili wakombolewe kutoka katika dhambi na kifo ambavyo sisi sote tumerithi kwa sababu ya dhambi ya babu yetu Adamu.

      Kifo cha Yesu Kristo kilitofautianaje na cha wale wengine waliouawa kwa sababu ya imani yao?

      Yesu alikuwa mwanadamu mkamilifu. Alizaliwa bila dosari ya dhambi na alidumisha ukamilifu huo katika maisha yake yote. “Yeye hakufanya dhambi.” Yeye alikuwa “asiye na unajisi, aliyetengwa kutoka kwa watenda-dhambi.”—1 Pet. 2:22; Ebr. 7:26.

      Alikuwa Mwana wa pekee wa Mungu. Mungu mwenyewe alisema jambo hilo kwa sauti kutoka mbinguni. (Mt. 3:17; 17:5) Hapo mwanzoni Mwana huyo alikuwa ameishi mbinguni; kupitia yeye Mungu aliumba watu na vitu vingine vyote vilivyoumbwa ulimwenguni kote. Ili kutimiza mapenzi Yake, Mungu aliuhamisha kimuujiza uhai wa Mwana huyo, akauweka katika tumbo la uzazi la msichana bikira ili azaliwe akiwa mwanadamu. Ili kukazia kwamba kwa kweli alikuwa amekuja kuwa mwanadamu, Yesu alijiita Mwana wa binadamu.—Kol. 1:15-20; Yoh. 1:14; Luka 5:24.

      Hakukosa uwezo mbele ya wauaji wake. Yeye alisema: “Ninaitoa nafsi yangu . . . Hakuna mtu ambaye ameichukua kutoka kwangu, bali ninaitoa kwa uamuzi wangu mwenyewe.” (Yoh. 10:17, 18) Alikataa kuomba msaada kutoka kwa majeshi ya malaika wapate kuingilia kati ili asikamatwe. (Mt. 26:53, 54) Ijapokuwa watu waovu waliruhusiwa watimize hila zao za kumuua, kwa kweli kifo chake kilikuwa cha kidhabihu.

      Damu yake iliyomwagwa ina thamani ya kuwaandalia wengine ukombozi. “Mwana wa binadamu alikuja, si kuhudumiwa, bali kuhudumu na kutoa nafsi yake iwe fidia badala ya wengi.” (Marko 10:45) Kwa hiyo, hakufa tu kwa sababu ya imani yake, bali kifo chake kilikuwa na maana zaidi.

      Ona pia ukurasa wa 336, 337, chini ya kichwa, “Ukumbusho.”

      Kwa nini ilikuwa lazima fidia itolewe kwa njia hiyo ili tupate uzima wa milele?

      Rom. 5:12: “Kupitia mtu mmoja [Adamu] dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi.” (Hata tukiishi kwa unyoofu namna gani, sisi sote ni watenda-dhambi tangu kuzaliwa. [Zab. 51:5] Hatuwezi kamwe kujipatia wenyewe haki ya kuishi milele.)

      Rom. 6:23: “Mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo.”

      Zab. 49:6-9: “Wale wanaotegemea riziki zao, na ambao wanaendelea kujisifu juu ya wingi wa utajiri wao, hakuna hata mmoja wao anayeweza kumkomboa hata ndugu, wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake; (nayo bei ya ukombozi wa nafsi yao ni yenye thamani sana hivi kwamba imekoma mpaka wakati usio na kipimo) hivi kwamba yeye aendelee kuishi milele na asilione shimo.” (Hakuna mwanadamu asiyekamilika anayeweza kumkomboa mtu mwingine kutoka katika dhambi na kifo. Pesa zake haziwezi kununua uzima wa milele, na nafsi yake inayokufa kwa sababu ya dhambi, haina thamani ya kumkomboa mtu yeyote.)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki