-
KifoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
‘Mtu hufa wakati wake unapofika’
Unaweza kujibu: ‘Watu wengi wana maoni kama yako. Je, unajua kwamba Wagiriki wengi wa kale walikuwa na maoni hayohayo? Waliamini kwamba kulikuwa na miungu mitatu ya kike iliyoamua muda ambao kila mwanadamu angeishi. Lakini Biblia ina maoni tofauti kabisa kuhusu maisha.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘(Soma Mhubiri 9:11.) Mfano: Jiwe linaweza kuvunjika kutoka kwenye nyumba na kumwangukia mpita-njia. Je, Mungu ndiye aliyesababisha jambo hilo? Ikiwa hivyo ndivyo ilivyo, je, ni haki kumshtaki mwenye nyumba kwa sababu ya uzembe? . . . Kama Biblia inavyosema, kwa mpita-njia huyo, tukio hilo halikuwa limepangwa mapema wala halikuwa limetarajiwa, bali alikuwa papo hapo wakati jiwe hilo lilipoanguka.’ (2) ‘Biblia inatuambia kwamba tukiepuka mwenendo mbaya, tutaulinda uhai wetu. (Met. 16:17) Ikiwa wewe ni mzazi, nina hakika kwamba unatumia kanuni hiyohiyo unapowafundisha watoto wako. Unawaonya juu ya mambo ambayo yanaweza kusababisha kifo. Yehova anawafanyia wanadamu wote jambo hilohilo leo.’ (3) ‘Yehova anajua yatakayotokea wakati ujao. Kupitia Biblia yeye anatuambia jinsi tunavyoweza kufurahia maisha marefu zaidi kuliko yale ya watu wanaopuuza maneno yake. (Yoh. 17:3; Met. 12:28)’ (Ona pia kichwa, “Majaliwa.”)
-
-
Kitia-MoyoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kitia-Moyo
Maana: Jambo linalomtia mtu moyo au kumpa tumaini. Kila mtu anahitaji kutiwa moyo. Mtu anaweza kumtia mwingine moyo kwa kumsaidia au kwa kumshukuru. Mara nyingi huhusisha kumsaidia mtu aone jinsi ya kukabiliana na hali ngumu au kuzungumzia sababu za kuwa na hakika katika wakati ujao ulio bora. Biblia ina msingi bora zaidi wa kitia-moyo hicho, na maandiko yaliyonukuliwa hapa yanaweza kukusaidia unapowatia moyo watu wanaokabili matatizo mbalimbali. Wakati mwingine, mtu anaweza kumsaidia sana mwingine kwa kumsikitikia tu.—Rom. 12:15.
Kwa wale wanaoteseka kwa sababu ya UGONJWA—
Ufu. 21:4, 5: “‘[Mungu] atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.’ Na Yule aliyeketi juu ya kiti cha ufalme akasema: ‘Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.’ Pia, anasema: ‘Andika, kwa sababu maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.’”
-