Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Shetani Ibilisi
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Watu fulani hurejezea andiko la Ufunuo 20:3 (lililonukuliwa hapo juu) ili kuunga mkono wazo hilo. Wao husema kwamba “abiso,” au “shimo pasipo mwisho” (ZSB), huwakilisha dunia ikiwa katika hali ya ukiwa. Je, hiyo ni kweli? Andiko la Ufunuo 12:7-9, 12, (ZSB) huonyesha kwamba wakati fulani kabla ya kutupwa kwake katika abiso, Shetani ‘anatupwa’ kutoka mbinguni kuja duniani, ambako anawaletea wanadamu ole nyingi. Kwa hiyo, wakati andiko la Ufunuo 20:3 (ZSB) linaposema kwamba Shetani ‘anatupwa katika shimo pasipo mwisho,’ hakika haachwi tu mahali alipo tayari—akiwa bila kuonekana lakini akiwa amefungiwa katika ujirani wa dunia. Yeye anaondolewa na kupelekwa mbali kutoka hapo, ili “asipate kudanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie.” Ona kwamba andiko la Ufunuo 20:3 linasema kwamba, mwishoni mwa ile miaka elfu, si mataifa yanayofunguliwa kutoka katika abiso, bali ni Shetani. Shetani atakapofunguliwa, watu ambao hapo zamani walifanyiza mataifa hayo watakuwa tayari wapo.

      Nyakati nyingine, andiko la Isaya 24:1-6 na Yeremia 4:23-29 (UV) hutumiwa kuunga mkono imani hiyo. Maandiko hayo yanasema hivi: “Tazama, BWANA ameifanya dunia kuwa tupu, aifanya ukiwa . . . dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana BWANA amenena neno hilo.” “Naliiangalia nchi, na tazama, ilikuwa ukiwa . . . Nikaangalia, na tazama, hapakuwa na mtu hata mmoja . . . Maana BWANA asema hivi, Nchi yote itakuwa ukiwa . . . Kila mji umeachwa, hapana hata mtu mmoja akaaye ndani yake.” Unabii huo unamaanisha nini? Ulitimizwa mara ya kwanza juu ya Yerusalemu na nchi ya Yuda. Katika kutekeleza hukumu yake, Yehova aliwaruhusu Wababiloni waishambulie nchi hiyo. Mwishowe yote iliachwa ukiwa, bila kitu. (Ona Yeremia 36:29.) Lakini Mungu wakati huo hakuwaondoa watu katika dunia yote, wala hatafanya hivyo sasa. (Ona ukurasa wa 69-72, chini ya kichwa “Dunia,” pia kichwa “Mbingu.”) Hata hivyo, ataifanya ukiwa kabisa sehemu ya kisasa inayofananishwa na Yerusalemu lisilo na uaminifu, yaani, Jumuiya ya Wakristo, ambayo kwa mwenendo wake usio mtakatifu inalishutumu jina la Mungu, na sehemu nyingine zote za tengenezo la Shetani linaloonekana.

      Badala ya kuwa ukiwa kabisa, wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo, na wakati Shetani atakapokuwa katika abiso, dunia yote itakuwa paradiso. (Ona “Paradiso.”)

  • Sikukuu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Sikukuu

      Maana: Siku ambazo watu hawaendi kazini na shuleni ili kuadhimisha tukio fulani. Huenda siku hizo pia zikawa vipindi vya sherehe za familia au za jamii. Huenda washiriki wakaziona kuwa ni sikukuu za kidini au za kijamii au kilimwengu.

      Je, mwadhimisho wa Krismasi unapatana na Biblia?

      Tarehe ya mwadhimisho

      Cyclopædia ya M’Clintock na Strong inasema: “Mungu hakuagiza Krismasi iadhimishwe, wala mwadhimisho huo hautokani na A[gano] J[ipya]. A[gano] J[ipya] wala chanzo kingine chochote, hakitaji siku ya kuzaliwa kwa Kristo.”—(New York, 1871) Buku la 2, uku. 276.

      Luka 2:8-11 huonyesha kwamba wakati wa kuzaliwa kwa Yesu, wachungaji walikuwa nje usiku. Kitabu Daily Life in the Time of Jesus chaeleza: ‘Wakati wa baridi kali, makundi ya wanyama hayakutoka nje; na hilo pekee linaweza kuthibitisha kwamba tarehe ya Krismasi, ya wakati wa baridi kali, haiwezi kuwa sahihi, kwa kuwa Injili husema kwamba wachungaji walikuwa nje.’—(New York, 1962), Henri Daniel-Rops, uku. 228.

      The Encyclopedia Americana husema hivi: “Sababu ya kuchagua Desemba 25 kuwa siku ya Krismasi haieleweki waziwazi, lakini inaaminiwa kwamba siku hiyo ilichaguliwa ili ilingane na sherehe za kipagani zilizotukia karibu na wakati ambapo jua huwa mbali zaidi na ikweta, wakati wa baridi kali, siku zinapoanza kurefuka, ili kusherehekea ‘kuzaliwa upya kwa jua.’ . . . Satanalia ya Kiroma (sikukuu ya zohali, mungu wa kilimo, na ya nguvu mpya za jua), pia iliadhimishwa wakati huo, na inaonekana kwamba desturi fulani za Krismasi zilianzia katika mwadhimisho huo wa kale wa kipagani.”—(1977), Buku la 6, uku. 666.

      New Catholic Encyclopedia inakubali hivi: “Tarehe ya kuzaliwa kwa Kristo haijulikani. Injili hazitaji siku wala mwezi . . . Kulingana na nadharia iliyotolewa na H. Usener . . . na inayokubaliwa na wasomi wengi leo, kuzaliwa kwa Kristo kulipewa tarehe ambayo jua linakuwa mbali zaidi na ikweta, wakati wa baridi kali, (Desemba 25 katika kalenda ya Julias, Januari 6 katika kalenda ya Misri), kwa sababu siku hiyo, jua lilipoanza kurudi kwenye anga za kaskazini, waabudu wa kipagani wa Mithra walisherehekea dies natalis Solis Invicti (kuzaliwa kwa jua lisiloshindika). Katika Desemba 25, 274, Aurelian alikuwa amemtangaza mungu-jua kuwa mdhamini mkuu wa milki na kumjengea hekalu katika Uwanja wa Martius. Krismasi ilianza wakati madhehebu ya jua yalipositawi nchini Roma.”—(1967), Buku la 3, uku. 656.

      Watu wenye hekima, au Mamajusi, walioongozwa na nyota

      Mamajusi hao walikuwa wanajimu kutoka mashariki. (Mt. 2:1, 2) Ijapokuwa unajimu unapendwa na watu wengi leo, Biblia inapinga kabisa zoea hilo. (Ona ukurasa wa 175, 176 chini ya kichwa “Majaliwa.”) Je, Mungu angewaelekeza kwa Yesu aliyezaliwa karibuni watu wenye mazoea ambayo Yeye mwenyewe anayashutumu?

      Mathayo 2:1-16 huonyesha kwamba nyota hiyo iliwaongoza wanajimu hao kwa Mfalme Herode kwanza kisha kwa Yesu na kwamba Herode alipanga Yesu auawe. Biblia haitaji mtu mwingine yeyote aliyeiona “nyota” hiyo ila wanajimu hao. Walipoondoka, malaika wa Yehova alimwagiza Yosefu akimbilie Misri ili kumlinda mtoto. Je, “nyota” hiyo ilikuwa ishara kutoka kwa Mungu au kutoka kwa mtu fulani aliyetaka kumwangamiza Mwana wa Mungu?

      Ona kwamba masimulizi ya Biblia hayasemi kwamba walimkuta Yesu mchanga katika hori, kama vile ambavyo huonyeshwa katika picha za Krismasi. Wanajimu walipofika, Yesu na wazazi wake walikuwa wakiishi katika nyumba. Kuhusu umri wa Yesu wakati huo, kumbuka kwamba, ikitegemea habari ambazo Herode alikuwa amepata kutokana na wanajimu, alitoa amri kwamba wavulana wote katika wilaya ya Bethlehemu wenye umri wa miaka miwili kurudi chini waangamizwe.—Mt. 2:1, 11, 16.

      Kutoa zawadi wakati wa maadhimisho hayo; hadithi za Baba Krismasi, n.k.

      Zoea la kutoa zawadi za Krismasi halitokani na zawadi zilizotolewa na wale Mamajusi. Kama tulivyoona, hawakufika wakati wa kuzaliwa kwa Yesu. Isitoshe, badala ya kupeana zawadi wao kwa wao, walimpa zawadi Yesu mchanga, kulingana na desturi ya siku hizo wakati wa kutembelea watu mashuhuri.

      The Encyclopedia Americana inaeleza hivi: “Wakati wa Satanalia . . . kulikuwa na karamu, na watu walipeana zawadi.” (1977, Buku la 24, uku. 299) Katika visa vingi hilo lawakilisha roho ya Krismasi—kupeana zawadi. Roho hiyo ya kutoa zawadi haileti furaha ya kweli, kwa sababu inavunja kanuni za Kikristo kama zile zinazopatikana katika Mathayo 6:3, 4 na 2 Wakorintho 9:7. Kwa kweli, upendo unaweza kumchochea Mkristo awape wengine zawadi nyakati nyingine mwakani, akifanya hivyo kwa kadiri anavyotaka.

      Watoto huambiwa kwamba zawadi huletwa na Baba-Krismasi. (The World Book Encyclopedia, 1984, Buku la 3, uku. 414) Bila shaka, hadithi hizo si za kweli. Je, kusimuliwa kwa hadithi hizo huwafanya watoto waione kweli kuwa jambo muhimu? Na je, zoea hilo linamheshimu Yesu Kristo, aliyefundisha kwamba ni lazima Mungu aabudiwe kwa kweli?—Yoh. 4:23, 24.

      Je, kuna ubaya wowote kusherehekea maadhimisho ambayo huenda yasiwe ya Kikristo maadamu si maadhimisho ya kidini?

      Efe. 5:10, 11: “Endeleeni kuhakikisha lile linalokubalika kwa Bwana; na mwache kushirikiana pamoja nao katika matendo yasiyozaa matunda, ambayo ni ya giza, lakini badala yake muwe hata mkiyakaripia.”

      2 Kor. 6:14-18: “Kuna ushirika gani kati ya uadilifu na uasi-sheria? Au nuru ina ushirika gani na giza? Na zaidi, kuna upatano gani kati ya Kristo na Beliali? Au mtu mwaminifu ana fungu gani na asiye mwamini? Na hekalu la Mungu lina upatano gani na sanamu? . . . ‘“Kwa hiyo tokeni katikati yao, na mjitenge,” asema Yehova, “na mwache kugusa kitu kilicho najisi”’; ‘“nami nitawakaribisha ndani, . . .  nanyi mtakuwa wana na mabinti kwangu,” asema Yehova Mweza-Yote.’” (Kumpenda Yehova kikweli na kutaka sana kumpendeza kutamsaidia mtu aache mazoea yasiyo ya Kikristo ambayo huenda yakauvutia moyo wake. Mtu ambaye kwa kweli anamjua na kumpenda Yehova haoni kwamba ananyimwa furaha kwa njia yoyote kwa kuacha mazoea yanayoheshimu miungu ya uwongo au yanayoendeleza uwongo. Upendo wa kweli unamfanya ashangilie kweli, wala si ukosefu wa uadilifu. Ona 1 Wakorintho 13:6.)

      Linganisha na Kutoka 32:4-10. Ona kwamba Waisraeli walifuata zoea la kidini la Kimisri lakini wakalipa jina jipya, “sherehe kwa ajili ya Yehova.” Lakini Yehova aliwaadhibu vikali kwa sababu ya zoea hilo. Leo tunaona tu mazoea ya karne ya 20 yanayopatikana katika sikukuu nyingi. Huenda mazoea mengine yakaonekana kuwa hayana madhara. Lakini Yehova aliyaona mazoea ya kidini ya kipagani ambayo ndiyo chanzo cha mazoea ya leo. Je, hatupaswi kuzingatia hasa maoni yake?

      Mfano: Tuseme umati wa watu umefika kwenye nyumba ya bwana mmoja wakisema wamekuja kuadhimisha sikukuu ya kuzaliwa kwake. Yeye hapendezwi na maadhimisho hayo ya sikukuu za kuzaliwa. Hapendi kuona watu wakila kupita kiasi au wakilewa au wakijihusisha katika mwenendo mpotovu. Lakini baadhi yao wanatenda mambo yote hayo, na kuwaletea zawadi wote waliopo isipokuwa yeye! Isitoshe, wanachagua tarehe ya kuzaliwa kwa mmoja kati ya adui za mtu huyo kuwa siku ya kufanya maadhimisho hayo. Mtu huyo angeonaje? Je, wewe ungependa kushirikiana nao? Hivyo ndivyo inavyofanywa katika maadhimisho ya Krismasi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki