Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kurudi kwa Kristo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Yehova alisema kwamba ‘anashuka’ ili kuvuruga lugha ya wajenzi wa mnara wa Babeli. (Mwa. 11:7) Pia alisema kwamba ‘anashuka’ ili kuwakomboa Waisraeli kutoka utumwani Misri. Na Mungu alimhakikishia Musa kwamba “Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe” ili kuwaongoza Waisraeli kuelekea Nchi ya Ahadi. (Kut. 3:8; 33:14) Lakini hakuna mwanadamu yeyote ambaye alimwona Mungu.—Kut. 33:20; Yoh. 1:18.

      Biblia inahusianisha kuwapo kwa Kristo na matukio gani?

      Dan. 7:13, 14: “Mtu fulani kama mwana wa binadamu [Yesu Kristo] alikuwa anakuja na mawingu ya mbingu; naye akaja kwa Mzee wa Siku [Yehova Mungu], nao wakamleta karibu mbele zake Yule. Naye akapewa utawala na heshima na ufalme, ili vikundi vyote vya watu, vya mataifa na lugha vimtumikie yeye.”

      1 The. 4:15, 16: “Tunawaambia hivi kwa neno la Yehova, kwamba sisi tulio hai ambao tutabaki mpaka kuwapo kwa Bwana hatutawatangulia kwa vyovyote wale ambao wamelala usingizi katika kifo; kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni akiwa na mwito wenye amri, kwa sauti ya malaika mkuu na kwa tarumbeta ya Mungu, na wale walio wafu katika muungano na Kristo watafufuliwa kwanza.” (Kwa hiyo, wale watakaotawala pamoja na Kristo wangefufuliwa wawe pamoja naye mbinguni—kwanza wale waliokuwa wamekufa miaka mingi iliyopita kisha wale ambao wangekufa baada ya kurudi kwa Bwana.)

      Mt. 25:31-33: “Wakati Mwana wa binadamu atakapofika katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu. Na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu, mmoja kutoka kwa mwenzake, kama vile mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi. Naye atawaweka kondoo kwenye mkono wake wa kuume, lakini mbuzi kwenye mkono wake wa kushoto.”

      2 The. 1:7-9: “Kwenu ninyi mnaopata dhiki, kitulizo pamoja nasi wakati wa ufunuo wa Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika zake wenye nguvu katika mwali wa moto, anapoleta kisasi juu ya wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu. Watu hao watahukumiwa adhabu ya uharibifu wa milele kutoka mbele ya Bwana na kutoka kwenye utukufu wa nguvu zake.”

      Luka 23:42, 43: “Naye [yule mtenda-maovu mwenye huruma aliyetundikwa pamoja na Yesu] akaendelea kusema: ‘Yesu, unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.’ Naye akamwambia: ‘Kwa kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja nami katika Paradiso.’” (Chini ya utawala wa Yesu, dunia yote itakuwa Paradiso; wafu walio katika kumbukumbu ya Mungu watafufuliwa na kupewa nafasi ya kupata uzima mkamilifu duniani milele.)

      Ona pia ukurasa wa 284-289, chini ya kichwa, “Siku za Mwisho.”

  • Kusema kwa Lugha
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kusema kwa Lugha

      Maana: Uwezo wa pekee ambao wanafunzi fulani walipewa katika kutaniko la kwanza la Kikristo kupitia roho takatifu uliowawezesha kuhubiri au kumtukuza Mungu katika lugha nyingine.

      Je, Biblia inasema wote walio na roho ya Mungu ‘wangesema kwa lugha’?

      1 Kor. 12:13, 30: “Kwa kweli kwa roho moja sote tulibatizwa katika mwili mmoja . . . Je, wote wana zawadi za maponyo? Je, wote husema kwa lugha?” (Ona pia 1 Wakorintho 14:26.)

      1 Kor. 14:5: “Basi ningependa ninyi nyote mseme kwa lugha, lakini napendelea zaidi kwamba mtoe unabii. Kwa kweli, yeye anayetoa unabii ni mkubwa kuliko yeye anayesema kwa lugha, isipokuwa, kwa kweli, yeye atafsiri, ili kutaniko lijengwe.”

      Mtu akisema kwa maneno ya kusisimuka katika lugha ambayo hajapata kujifunza kamwe, je, hilo linaonyesha kwamba ana roho takatifu?

      Je, uwezo wa ‘kusema kwa lugha’ unaweza kutokana na chanzo kingine isipokuwa Mungu wa kweli?

      1 Yoh. 4:1: “Wapendwa, msiamini kila neno lililoongozwa na roho [“kila roho,” UV, ZSB], lakini yajaribuni maneno yaliyoongozwa na roho ili kuona kama yanatokana na Mungu.” (Ona pia Mathayo 7:21-23; 2 Kor. 11:14, 15.)

      Kati ya wale ‘wanaosema kwa lugha’ leo ni Wapentekoste na Wabaptisti, pia Wakatoliki, Waepiskopali, Wamethodisti, Walutheri, na Wapresibiteri. Yesu alisema kwamba roho takatifu ‘itawaongoza wanafunzi wake ndani ya kweli yote.’ (Yoh. 16:13) Je, wafuasi wa kila moja ya dini hizo wanaamini kwamba wengine ambao pia ‘husema kwa lugha’ wanaongozwa katika “kweli yote”? Hilo lingewezekanaje, kwa kuwa wao wote hawapatani? Ni roho gani inayowawezesha ‘kusema kwa lugha’?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki