Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Har–Magedoni
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • 2 The. 1:6: “Ni jambo la uadilifu kwa upande wa Mungu kuwalipa dhiki wale wanaowafanyia ninyi [watumishi wake] dhiki.”

      Je, inawezekana kutounga mkono upande wowote?

      2 The. 1:8: “Anapoleta kisasi juu ya wale wasiomjua Mungu [kwa kuchagua] na wale wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.”

      Mt. 24:37-39: “Kama vile siku za Noa zilivyokuwa . . . hawakujali mpaka gharika ikaja na kuwafagilia mbali wote, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa.”

      Mt. 12:30: “Yeye asiyekuwa upande wangu ananipinga, naye asiyekusanya pamoja nami anatawanya.”

      Linganisha na Kumbukumbu la Torati 30:19, 20.

      Ni nani anayeyachochea mataifa kwenye hali ya ulimwengu itakayotokeza vita dhidi ya Mungu?

      Ufu. 16:13, 14; 12:9: “Nikaona maneno machafu matatu yaliyoongozwa na roho ambayo yalionekana kama vyura yakitoka katika kinywa cha yule joka mkubwa [Shetani Ibilisi; Ufu. 12:9] na kutoka katika kinywa cha yule mnyama-mwitu na kutoka katika kinywa cha yule nabii wa uwongo. Hayo, kwa kweli, ni maneno yanayoongozwa na roho waovu nayo yanafanya ishara, nayo yanakwenda kwa wafalme wa dunia nzima inayokaliwa, ili kuwakusanya pamoja kwa vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.”

      Linganisha na Luka 4:5, 6; 1 Yohana 5:19; pia Matendo 5:38, 39; 2 Mambo ya Nyakati 32:1, 16, 17.

  • Ibada ya Mababu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Ibada ya Mababu

      Maana: Zoea la kuwaheshimu na kuwaabudu mababu waliokufa (kwa kufanya sherehe au kwa njia nyingine) kwa sababu wanaamini kwamba mababu hao wanaishi katika makao yasiyoonekana na wanaweza kuwasaidia au kuwadhuru walio hai na kwa hiyo wanapaswa kutulizwa. Hilo si fundisho la Biblia.

      Je, mababu waliokufa wanajua mambo ambayo walio hai wanafanya, na je, mababu hao wanaweza kuwasaidia watu walio hai?

      Mhu. 9:5: “Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe.”

      Ayu. 14:10, 21: “Mtu wa udongo hukata pumzi, naye yuko wapi? Wanawe hupewa heshima, lakini yeye hajui hilo.”

      Zab. 49:10, 17-19: “Hata wenye hekima wanakufa, mjinga na asiyetumia akili huangamia wote pamoja, nao hulazimika kuwaachia wengine mali yao. . . . Anapokufa hawezi kuchukua kitu chochote; utukufu wake hautashuka chini pamoja naye. . . . Nafsi yake mwishowe inafikia tu kwenye kizazi cha mababu zake. Hawataona nuru tena kamwe.”

      Je, si kweli kwamba chakula kinachowekwa juu ya madhabahu au juu ya kaburi huwa hakiliwi? Je, hilo halionyeshi kwamba wafu hawawezi kukila?

      Ona pia kichwa, “Kuwasiliana na Pepo.”

      Je, kuna sababu ya kuogopa kwamba mababu zetu waliokufa watatudhuru?

      Mhu. 9:5, 6: “Lakini wafu, . . . upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari zimepotea, na mpaka wakati usio na kipimo hawana fungu lolote tena katika chochote ambacho kitafanywa chini ya jua.”

      Je, mtu ana roho inayoendelea kuishi baada ya mwili kufa?

      Eze. 18:4: “Tazama! Nafsi zote—ni zangu. Kama ilivyo nafsi ya baba ndivyo ilivyo nafsi ya mwana—ni zangu. Nafsi inayotenda dhambi—hiyo yenyewe itakufa.” (Ona pia mstari wa 20.)

      Zab. 146:3, 4: “Msiweke tegemeo lenu katika watu wenye vyeo, wala katika mtu wa udongo, . . . Roho yake hutoka, naye hurudi kwenye udongo wake; siku hiyo mawazo yake hupotea.”

      Wanasayansi na madaktari wa upasuaji hawajaona uthibitisho wa kuwapo kwa sehemu yoyote ya mwanadamu iliyo na ufahamu na inayoendelea kuishi baada ya mwili kufa.

      Ona pia ukurasa wa 102-104, chini ya kichwa, “Kifo.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki