Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kifo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • ‘Mtu hufa wakati wake unapofika’

      Unaweza kujibu: ‘Watu wengi wana maoni kama yako. Je, unajua kwamba Wagiriki wengi wa kale walikuwa na maoni hayohayo? Waliamini kwamba kulikuwa na miungu mitatu ya kike iliyoamua muda ambao kila mwanadamu angeishi. Lakini Biblia ina maoni tofauti kabisa kuhusu maisha.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘(Soma Mhubiri 9:11.) Mfano: Jiwe linaweza kuvunjika kutoka kwenye nyumba na kumwangukia mpita-njia. Je, Mungu ndiye aliyesababisha jambo hilo? Ikiwa hivyo ndivyo ilivyo, je, ni haki kumshtaki mwenye nyumba kwa sababu ya uzembe? . . . Kama Biblia inavyosema, kwa mpita-njia huyo, tukio hilo halikuwa limepangwa mapema wala halikuwa limetarajiwa, bali alikuwa papo hapo wakati jiwe hilo lilipoanguka.’ (2) ‘Biblia inatuambia kwamba tukiepuka mwenendo mbaya, tutaulinda uhai wetu. (Met. 16:17) Ikiwa wewe ni mzazi, nina hakika kwamba unatumia kanuni hiyohiyo unapowafundisha watoto wako. Unawaonya juu ya mambo ambayo yanaweza kusababisha kifo. Yehova anawafanyia wanadamu wote jambo hilohilo leo.’ (3) ‘Yehova anajua yatakayotokea wakati ujao. Kupitia Biblia yeye anatuambia jinsi tunavyoweza kufurahia maisha marefu zaidi kuliko yale ya watu wanaopuuza maneno yake. (Yoh. 17:3; Met. 12:28)’ (Ona pia kichwa, “Majaliwa.”)

  • Kitia-Moyo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kitia-Moyo

      Maana: Jambo linalomtia mtu moyo au kumpa tumaini. Kila mtu anahitaji kutiwa moyo. Mtu anaweza kumtia mwingine moyo kwa kumsaidia au kwa kumshukuru. Mara nyingi huhusisha kumsaidia mtu aone jinsi ya kukabiliana na hali ngumu au kuzungumzia sababu za kuwa na hakika katika wakati ujao ulio bora. Biblia ina msingi bora zaidi wa kitia-moyo hicho, na maandiko yaliyonukuliwa hapa yanaweza kukusaidia unapowatia moyo watu wanaokabili matatizo mbalimbali. Wakati mwingine, mtu anaweza kumsaidia sana mwingine kwa kumsikitikia tu.—Rom. 12:15.

      Kwa wale wanaoteseka kwa sababu ya UGONJWA—

      Ufu. 21:4, 5: “‘[Mungu] atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.’ Na Yule aliyeketi juu ya kiti cha ufalme akasema: ‘Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.’ Pia, anasema: ‘Andika, kwa sababu maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.’”

      Mt. 9:35: “Yesu akaondoka ili kutembelea majiji na vijiji vyote, akifundisha . . . na kuhubiri habari njema ya ufalme na kuponya kila namna ya magonjwa na kila namna ya udhaifu.” (Kwa kuhusianisha uponyaji huo na mahubiri yake juu ya Ufalme, Yesu alionyesha mambo mazuri atakayowafanyia wanadamu wakati wa Utawala wake wa Miaka Elfu.)

      2 Kor. 4:13, 16: “Sisi pia tunaonyesha imani . . . Kwa hiyo hatufi moyo, lakini hata ikiwa mtu tuliye kwa nje [mwili wetu] anachakaa, hakika mtu tuliye kwa ndani anafanywa upya [au tunapewa nguvu mpya] siku baada ya siku.” (Huenda tukawa tunadhoofika kimwili, lakini kiroho tunafanywa upya tunapoendelea kujilisha ahadi nzuri za Mungu.)

      Ona pia Luka 7:20-23.

      Kwa wale ambao wapendwa wao WAMEKUFA—

      Isa. 25:8, 9: “Yeye kwa kweli atameza kifo milele, na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote. . . . Na katika siku hiyo hakika mtu atasema: ‘Tazama! Huyu ndiye Mungu wetu. Tumemtumaini yeye, naye atatuokoa. Huyu ndiye Yehova. Tumemtumaini yeye. Na tuwe na shangwe na kushangilia katika wokovu wake.’”

      Yoh. 5:28, 29: “Msistaajabie jambo hili, kwa sababu saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake na kutoka, wale waliotenda mambo mema kwenye ufufuo wa uzima, wale waliokuwa na zoea la kutenda mambo maovu kwenye ufufuo wa hukumu.”

      Yoh. 11:25, 26: “Yesu akamwambia: ‘Mimi ndiye ufufuo na uzima. Yule anayeniamini, hata akifa, atarudi kwenye uzima; na kila mtu aliye hai na ananiamini hatakufa kamwe. Je, unaamini hilo?’”

      Zab. 146:5, 9: “Mwenye furaha ni yule . . . ambaye tumaini lake liko katika Yehova Mungu wake. . . . Humtuliza mvulana asiye na baba na mjane.” (Sasa hivi Mungu anawahangaikia kwa upendo wale waliofiwa.)

      Ona pia Luka 7:11-16; 8:49-56.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki