-
Adamu na HawaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Mt. 19:4, 5: “[Yesu] akasema: ‘Je, hamkusoma [katika Mwanzo 1:27; 2:24] kwamba yeye aliyewaumba hao [Adamu na Hawa] kutoka mwanzo aliwafanya mwanamume na mwanamke na kusema, “Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake, na hao wawili watakuwa mwili mmoja”?’” (Kwa kuwa Yesu aliamini kwamba masimulizi ya Mwanzo yalikuwa ya kweli, je, sisi pia hatupaswi kuyaamini?)
Mtu Akisema—
‘Dhambi ya Adamu ilikuwa mapenzi ya Mungu, mpango wa Mungu.’
Unaweza kujibu hivi: ‘Watu wengi wamesema hivyo. Lakini ikiwa ningefanya jambo ambalo ulitaka nifanye, je, ungenihukumu nikilifanya? . . . Basi, ikiwa dhambi ya Adamu ilikuwa mapenzi ya Mungu, kwa nini Adamu alifukuzwa kutoka Edeni akiwa mtenda-dhambi? (Mwa. 3:17-19, 23, 24)’
Au unaweza kusema: ‘Hilo ni jambo lenye kupendeza, na kwa kweli jibu linatia ndani Mungu ni mtu wa aina gani. Je, lingekuwa jambo la haki au la upendo kumhukumu mtu kwa kufanya jambo ambalo wewe mwenyewe ulimpangia afanye?’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Yehova ni Mungu wa upendo. (1 Yoh. 4:8) Njia zake zote ni haki. (Zab. 37:28; Kum. 32:4) Hayakuwa mapenzi ya Mungu Adamu afanye dhambi; alimwonya Adamu. (Mwa. 2:17)’ (2) ‘Mungu alimruhusu Adamu, kama anavyoturuhusu sisi, kuwa na uhuru wa kuchagua jambo ambalo angefanya. Ukamilifu haukuondoa uhuru wa kuchagua kutotii. Adamu alichagua kumwasi Mungu, ingawa alikuwa ameonywa kwamba matokeo yangekuwa kifo.’ (Ona pia ukurasa wa 172, 173.)
-
-
Babiloni MkubwaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Babiloni Mkubwa
Maana: Milki ya ulimwengu ya dini za uwongo, inayotia ndani dini zote ambazo mafundisho na matendo yake hayapatani na ibada ya kweli ya Yehova, Mungu wa pekee wa kweli. Baada ya Gharika ya siku za Noa, dini ya uwongo ilianzia Babeli (ambapo baadaye paliitwa Babiloni). (Mwa. 10:8-10; 11:4-9) Kisha, imani za kidini za Kibabiloni na matendo yalienea kwenye nchi nyingi. Kwa hiyo, Babiloni Mkubwa likawa jina linalofaa dini za uwongo kwa ujumla.
-