-
ImaniKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Ahadi za Biblia kuhusu afya bora, ufufuo wa wafu, na kadhalika, zinatiwa nguvu na habari kuhusu miujiza ambayo Yesu alifanya. Hizo si hadithi za kubuniwa tu. Soma masimulizi ya Injili ukaone uthibitisho unaoonyesha kwamba mambo hayo kwa kweli yalitukia. Majina ya maeneo mbalimbali pamoja na majina ya watawala walioishi wakati huo, yanatajwa; masimulizi ya watu kadhaa waliojionea mambo hayo yamehifadhiwa. Kutafakari uthibitisho huo kwaweza kuimarisha imani yako katika ahadi za Biblia.
Nenda kwenye Majumba ya Ufalme ya Mashahidi wa Yehova na makusanyiko yao makubwa, ndipo utakapojionea mwenyewe kwamba kutumia shauri la Biblia hubadili maisha ya mtu, yaani huwafanya watu wawe wanyoofu na waadilifu, na huwafanya watu wa jamii zote na mataifa yote waishi na kufanya kazi pamoja katika roho ya undugu wa kweli.
Je, kweli matendo ni ya lazima ikiwa mtu ana imani?
Yak. 2:17, 18, 21, 22, 26: “Imani, ikiwa haina matendo, imekufa yenyewe. Hata hivyo, mtu fulani atasema: ‘Wewe una imani, nami nina matendo. Nionyeshe imani yako bila matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.’ Je, Abrahamu baba yetu hakutangazwa kuwa mwadilifu kwa matendo baada ya kumtoa Isaka mwana wake juu ya madhabahu? Mnaona kwamba imani yake ilitenda pamoja na matendo yake na kwa matendo yake imani yake ilikamilishwa. Kwa kweli, kama vile ambavyo mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo pia imani bila matendo imekufa.”
Mfano: Huenda mvulana ana urafiki na msichana, na kumwambia kwamba anampenda. Lakini ikiwa hajamuuliza msichana huyo aolewe naye, je, mvulana huyo kweli anaonyesha kwamba upendo wake ni wa kweli? Vivyo hivyo, matendo huonyesha ukweli wa imani yetu na upendo wetu. Ikiwa hatumtii Mungu, basi hatumpendi kikweli wala hatuamini kwamba njia zake ni za uadilifu. (1 Yoh. 5:3, 4) Lakini hatuwezi kudai wokovu hata tuwe na matendo gani. Uzima wa milele ni zawadi kutoka kwa Mungu kupitia Yesu Kristo, si malipo kwa ajili ya matendo yetu.—Efe. 2:8, 9.
-
-
Jamii za WanadamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Jamii za Wanadamu
Maana: Neno jamii, kama linavyotumiwa hapa, linamaanisha kikundi cha wanadamu walio na sifa fulani za maumbile ambazo zinaweza kurithiwa, na zilizo za kawaida sana katika watu wa kikundi hicho, hivi kwamba wanaweza kubainishwa kuwa jamii tofauti. Hata hivyo, tunapaswa kukumbuka kwamba kwa kuwa jamii hizo mbalimbali zinaweza kuoana na kuzaana, basi, kwa kweli wanadamu wote ni viumbe wa “aina” moja, wote ni familia moja ya wanadamu. Kwa hiyo, jamii hizo tofauti ni namna mbalimbali tu za jamii ya wanadamu.
-