-
Kitia-MoyoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Zab. 103:13, 14: “Kama vile baba anavyowaonyesha wanawe rehema, ndivyo ambavyo Yehova amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa. Kwa maana yeye mwenyewe analijua vema umbo letu, akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.”
Neh. 9:17: “Wewe ni Mungu wa matendo ya kusamehe, mwenye neema na rehema, si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fadhili zenye upendo.”
2 Pet. 3:9, 15: “Yehova hakawii kuhusiana na ahadi yake, kama watu fulani wanavyoona kukawia, bali yeye ni mwenye subira kwenu kwa sababu hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba. Zaidi ya hayo, ioneni subira ya Bwana wetu kuwa wokovu.”
-
-
KunyakuliwaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kunyakuliwa
Maana: Imani ya kwamba Wakristo waaminifu watachukuliwa kimwili kutoka duniani, waondolewe ghafula kutoka katika ulimwengu, ili waende kuungana pamoja na Bwana “hewani.” Watu fulani huamini kwamba andiko la 1 Wathesalonike 4:17 linazungumzia “kunyakuliwa” huko.
Mtume Paulo aliposema kwamba Wakristo ‘watanyakuliwa’ wakawe pamoja na Bwana, alikuwa akizungumza juu ya nini?
1 The. 4:13-18, UV: “Hatutaki msijue habari zao waliolala mauti [“wale wanaokufa,” NAJ], msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini. Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye. Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. Basi, farijianeni kwa maneno hayo.” (Inaonekana kwamba washiriki fulani wa kutaniko la Kikristo katika Thesalonike walikuwa wamekufa. Paulo aliwatia moyo waliobaki wafarijiane kwa tumaini la ufufuo. Aliwakumbusha kwamba Yesu alifufuliwa baada ya kufa kwake; kwa hiyo, pia, wakati wa kuja kwa Bwana, wale Wakristo waaminifu kati yao waliokuwa wamekufa wangefufuliwa wakawe pamoja na Kristo.)
Ni nani ‘watakaonyakuliwa katika mawingu,’ kama ilivyoandikwa katika 1 Wathesalonike 4:17?
Mstari wa 15 unaeleza kwamba hao ni waaminifu ‘watakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana,’ yaani, watakuwa wangali hai wakati wa kuja kwa Kristo. Je, watapata kufa? Kulingana na Waroma 6:3-5 na 1 Wakorintho 15:35, 36, 44 (maandiko yaliyonukuliwa katika ukurasa wa 113), ni lazima wafe kabla ya kwenda kuishi mbinguni. Lakini si lazima wabaki katika kifo wakingojea kurudi kwa Kristo. Wao ‘watanyakuliwa’ mara moja, “kufumba na kufumbua,” wakawe pamoja na Bwana.—1 Kor. 15:51, 52, UV; pia Ufunuo 14:13.
Je, Kristo atatokea akionekana kwa macho juu ya wingu, kisha awachukue Wakristo waaminifu waende mbinguni huku ulimwengu ukitazama?
Je, Yesu alisema kwamba ulimwengu utamwona tena kwa macho yao halisi?
Yoh. 14:19, UV: “Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena; bali ninyi [wanafunzi wake waaminifu] mnaniona. Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai.” (Italiki ni zetu.) (Linganisha na 1 Timotheo 6:16.)
Maneno ‘Bwana atashuka kutoka mbinguni’ yanamaanisha nini?
Je, Bwana anaweza ‘kushuka kutoka mbinguni,’ kama inavyoelezwa katika 1 Wathesalonike 4:16, bila kuonekana kwa macho halisi? Katika siku za Sodoma na Gomora, majiji ya zamani, Yehova alisema kwamba “nitashuka sasa nione” mambo ambayo watu wanatenda. (Mwa. 18:21, UV) Lakini Yehova alipofanya ukaguzi huo, hakuna mwanadamu yeyote aliyemwona, ingawa waliwaona wale malaika aliowatuma wamwakilishe. (Yoh. 1:18) Vivyo hivyo, bila kurudi katika mwili, Yesu anaweza kuwaelekezea fikira zake wafuasi wake waaminifu duniani ili awape thawabu.
-