Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ngono
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Au unaweza kusema: ‘Ninapojibu hilo, ninaweza kusema nimeona kwamba watu wengi ambao hawaoni ngono kati ya watu wa jinsia moja kuwa jambo la aibu hawakubali Biblia kuwa ni Neno la Mungu. Je, una maoni gani kuhusu Biblia?’ Mtu huyo akidai kwamba anaiamini Biblia, unaweza kuongezea: ‘Ngono kati ya watu wa jinsia moja si suala jipya. Biblia inasema maoni ya Yehova Mungu yasiyobadilika kwa kutumia maneno yaliyo wazi sana. (Labda tumia habari katika ukurasa wa 235, 236.)’ Mtu huyo akionyesha shaka juu ya kuwako kwa Mungu au juu ya Biblia, unaweza kuongezea: ‘Ikiwa hakuna Mungu, ni jambo linalopatana na akili kwamba hatuwezi kuwajibika kwake nasi tunaweza kuishi kama tunavyopenda. Kwa hiyo swali ni hili, Je, kuna Mungu na je, mimi nipo kwa sababu aliniumba [pia, unaweza kusema, Je, Biblia iliongozwa na roho ya Mungu]? (Tumia habari kutoka ukurasa wa 215-221 au 32-42.)’

  • Paradiso
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Paradiso

      Maana: Katika tafsiri ya Biblia ya Kigiriki inayoitwa Septuajinti watafsiri walitumia inavyofaa neno “paradiso” (pa·raʹdei·sos) kumaanisha bustani ya Edeni, kwa sababu inaonekana ilikuwa bustani iliyozungushiwa ua. Baada ya masimulizi katika Mwanzo, maandishi ya Biblia yanayosema kuhusu paradiso yanarejelea (1) bustani ya Edeni yenyewe, au (2) dunia nzima itakapogeuzwa wakati ujao iwe kama ilivyokuwa ile Edeni, au (3) hali nzuri za kiroho kati ya watumishi wa Mungu duniani, au (4) maandalizi mbinguni yanayotukumbusha kuhusu Edeni.

      Je, “Agano Jipya” linasema kuhusu paradiso duniani wakati ujao, au habari hizo zimo katika “Agano la Kale” tu?

      Kuigawanya Biblia katika sehemu mbili, na kupima ubora wa maneno kwa msingi wa kama yamo katika sehemu ya agano la “Kale” au “Jipya” si jambo la Kimaandiko. Katika 2 Timotheo 3:16 tunaambiwa hivi: “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo.” Andiko la Waroma 15:4 linarejelea Maandiko yaliyoongozwa na roho ya Mungu kabla ya Ukristo linaposema hivi: “Mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi.” Kwa hiyo, jibu zuri kwa swali hilo linapaswa kuzingatia Biblia nzima.

      Andiko la Mwanzo 2:8 linasema hivi: “Yehova Mungu akapanda bustani [“shamba,” ZSB; pa·raʹdei·son, Septuajinti] katika Edeni, kuelekea mashariki, na hapo akamweka mtu [Adamu] ambaye alikuwa amemfanya.” Kulikuwa na mimea na wanyama wengi wa aina mbalimbali wanaopendeza. Yehova aliwabariki watu wa kwanza wawili na kuwaambia: “Zaeni, muwe wengi, mjaze dunia na kuitiisha, na mtawale samaki wa baharini na viumbe vinavyoruka vya mbinguni na kila kiumbe hai kinachotambaa juu ya dunia.” (Mwa. 1:28) Kusudi la kwanza la Mungu kwamba dunia yote iwe paradiso inayokaliwa na watu wanaopenda kutii sheria zake halitakosa kutimizwa. (Isa. 45:18; 55:10, 11) Hiyo ndiyo sababu Yesu alisema: “Wenye furaha ni wale walio na tabia-pole, kwa kuwa watairithi dunia.” Hiyo ndiyo sababu pia aliwafundisha wanafunzi wake wasali hivi: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.” (Mt. 5:5; 6:9, 10) Kupatana na hilo, andiko la Waefeso 1:9-11, linaeleza kusudi la Mungu la “kukusanya tena pamoja vitu vyote katika Kristo, vitu vilivyo mbinguni na vitu vilivyo duniani.” Andiko la Waebrania 2:5 linataja “dunia yenye kukaliwa inayokuja.” Andiko la Ufunuo 5:10 linataja wale ambao, wakiwa warithi pamoja na Kristo, “watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia.” Andiko la Ufunuo 21:1-5 na 22:1, 2 huongezea ufafanuzi mzuri wa hali zitakazokuwa katika “dunia mpya” na zinazotukumbusha ile Paradiso ya kwanza katika Edeni iliyokuwa na mti wa uzima.—Mwa. 2:9.

      Zaidi ya hayo, Yesu alitumia neno la Kigiriki pa·raʹdei·sos alipokuwa akirejelea Paradiso duniani wakati ujao. “Naye akamwambia [mtenda-maovu aliyekuwa akitundikwa pamoja na Yesu na ambaye aliuamini ufalme wa Yesu unaokuja]: ‘Kwa kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja nami katika Paradiso.’”—Luka 23:43.

      Katika andiko la Luka 23:43, Yesu alimaanisha nini alipomwambia yule mtenda-maovu kuhusu Paradiso?

      Je, ilikuwa ni makao ya muda ya ‘nafsi za watu wema waliokufa,’ sehemu ya Hadesi?

      Maoni hayo yalianzia wapi? The New International Dictionary of New Testament Theology inasema hivi: “Kutokana na kupenyeza kwa fundisho la Kigiriki la kutoweza kufa kwa nafsi, paradiso imekuwa makao ya waadilifu wakiwa toharani.” (Grand Rapids, Mich.; 1976, iliyohaririwa na Colin Brown, Buku la 2, uku. 761) Je, maoni hayo ambayo si ya kimaandiko yaliaminiwa na Wayahudi wakati Yesu alipokuwa duniani? Dictionary of the Bible ya Hastings inaonyesha kwamba jambo hilo si hakika.—(Edinburgh, 1905), Buku la 3, uku. 669, 670.

      Hata kama Wayahudi wengi walikuwa na maoni hayo katika karne ya kwanza, je, Yesu angeyaunga mkono kupitia ahadi yake kwa yule mtenda-maovu mwenye kutubu? Yesu alikuwa amewashutumu vikali Mafarisayo na waandishi Wayahudi kwa sababu walifundisha mapokeo yaliyopingana na Neno la Mungu.—Mt. 15:3-9; ona pia kichwa “Nafsi.”

      Yesu alienda Hadesi alipokufa, kama inavyoonyeshwa katika Matendo 2:30, 31. (Mtume Petro, akirejelea Zaburi 16:10, ananukuliwa akitumia Hadesi kama neno linalolingana na Sheoli.) Lakini hakuna mahali ambapo Biblia inasema kwamba Sheoli/Hadesi wala sehemu yoyote yake ni paradiso inayomletea mtu furaha. Badala yake, andiko la Mhubiri 9:5, 10 linasema kwamba wale walio humo “hawajui lolote kamwe.”

      Je, Paradiso inayotajwa katika Luka 23:43 ni mbingu au ni mahali fulani mbinguni?

      Biblia haikubaliani na maoni kwamba Yesu na yule mtenda-maovu walienda mbinguni siku ile ambayo Yesu alisema naye. Yesu alikuwa ametabiri kwamba, baada ya kuuawa kwake, atafufuliwa siku ya tatu. (Luka 9:22) Wakati wa kipindi hicho cha siku tatu yeye hakuwa mbinguni, kwa sababu baada ya ufufuo wake alimwambia Maria Magdalene hivi: “Sijapanda kwenda kwa Baba.” (Yoh. 20:17) Ilikuwa siku 40 baada ya ufufuo wa Yesu ndipo wanafunzi wake walipomwona akiinuliwa kutoka duniani, akafichwa machoni pao wasimwone alipoanza kupanda kwenda mbinguni.—Mdo. 1:3, 6-11.

      Yule mtenda-maovu hakutimiza matakwa ya kwenda mbinguni hata wakati fulani wa baadaye. Yeye hakuwa ‘amezaliwa tena’—hakuwa amebatizwa katika maji wala kuzaliwa kwa roho ya Mungu. Roho takatifu ilimiminwa juu ya wanafunzi wa Yesu zaidi ya siku 50 baada ya kufa kwa yule mtenda-maovu. (Yoh. 3:3, 5; Mdo. 2:1-4) Siku ya kufa kwake, Yesu alikuwa amefanya pamoja na wale ‘waliokuwa wameshikamana naye katika majaribu’ agano kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Yule mtenda-maovu hakuwa na sifa hiyo ya uaminifu naye hakutiwa katika agano hilo.—Luka 22:28-30.

      Ni nini kinachoonyesha kwamba Paradiso hiyo itakuwa duniani?

      Maandiko ya Kiebrania hayakuwafanya kamwe Wayahudi waaminifu watarajie thawabu ya uzima mbinguni. Maandiko hayo yalielekeza kwenye kurudishwa kwa Paradiso hapa duniani. Andiko la Danieli 7:13, 14 lilikuwa limetabiri kwamba wakati “utawala na heshima na ufalme” vitakabidhiwa Masihi, ‘vikundi vyote vya watu, vya mataifa na lugha vitamtumikia yeye.’ Raia hao wa Ufalme watakuwa hapa duniani. Kutokana na yale aliyomwambia Yesu, inaonekana yule mtenda-maovu alikuwa akionyesha tumaini la kwamba Yesu atamkumbuka wakati huo utakapofika.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki