Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mbingu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Yoh. 10:16: “Nina kondoo wengine, ambao si wa zizi hili; hao pia nitawaleta, nao wataisikiliza sauti yangu, nao watakuwa kundi moja, mchungaji mmoja.” (Hao “kondoo wengine” ni nani? Ni wafuasi wa Mchungaji Mwema, Yesu Kristo, lakini hawamo katika zizi la kondoo la “agano jipya,” wakiwa na tumaini la uzima wa mbinguni. Hata hivyo wanashirikiana kwa ukaribu na wale walio katika zizi hilo la kondoo.)

      2 Pet. 3:13: “Kulingana na ahadi yake tunangojea mbingu mpya na dunia mpya, na humo uadilifu utakaa.” (Pia Ufunuo 21:1-4)

      Ufu. 7:9, 10: “Baada ya mambo haya [baada ya mtume Yohana kuona hesabu kamili ya wale “waliotiwa muhuri” ambao walikuwa “wamenunuliwa kutoka duniani” ili wakawe na Kristo katika Mlima Sayuni wa mbinguni; ona Ufunuo 7:3, 4; 14:1-3] nikaona, na, tazama! umati mkubwa, ambao hakuna mtu aliyeweza kuuhesabu, kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha, wamesimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wamevikwa kanzu nyeupe; na kulikuwa na matawi ya mitende mikononi mwao. Nao wanaendelea kupaaza sauti kubwa, wakisema: ‘Wokovu unatoka kwa Mungu wetu, anayeketi juu ya kiti cha ufalme, na Mwana-Kondoo.’”

      Biblia inawatolea watu wangapi tumaini la uzima wa mbinguni?

      Luka 12:32: “Msiogope, kundi dogo, kwa sababu Baba yenu amekubali kuwapa ninyi ufalme.”

      Ufu. 14:1-3: “Nami nikaona, na, tazama! Mwana-Kondoo [Yesu Kristo] amesimama juu ya Mlima Sayuni [mbinguni; ona Waebrania 12:22-24], na pamoja naye 144,000 wakiwa na jina lake na jina la Baba yake limeandikwa juu ya mapaji ya nyuso zao. . . . Nao wanaimba kana kwamba ni wimbo mpya . . . na hakuna yeyote aliyeweza kujifunza kikamili wimbo ule ila wale 144,000, ambao wamenunuliwa kutoka duniani.”

      Je, wale 144,000 ni Wayahudi wa asili peke yao?

      Ufu. 7:4-8: “Nikaisikia hesabu ya wale waliotiwa muhuri, 144,000, waliotiwa muhuri kutoka kila kabila la wana wa Israeli: . . . Yuda . . . Rubeni . . . Gadi . . . Asheri . . . Naftali . . . Manase . . . Simeoni . . . Lawi . . . Isakari . . . Zabuloni . . . Yosefu . . . Benyamini.” (Hayo hayawezi kuwa makabila ya Israeli ya asili kwa sababu hakukuwa kamwe na kabila la Yosefu, makabila ya Efraimu na Dani hayamo kwenye orodha hii, na Walawi walitengwa kwa ajili ya utumishi wa hekalu lakini hawakuhesabiwa kati ya yale makabila 12. Ona Hesabu 1:4-16.)

      Rom. 2:28, 29: “Yeye si Myahudi aliye hivyo kwa nje, wala kutahiriwa si kule ambako ni kwa nje juu ya mwili. Bali yeye ni Myahudi aliye hivyo kwa ndani, na kutahiriwa kwake ni kule kwa moyo kupitia roho, wala si kupitia sheria zilizoandikwa.”

      Gal. 3:26-29: “Ninyi nyote, kwa kweli, ni wana wa Mungu kupitia imani yenu katika Kristo Yesu. . . . Hakuna Myahudi wala Mgiriki, hakuna mtumwa wala mtu huru, hakuna mwanamume wala mwanamke; kwa maana ninyi nyote ni mtu mmoja katika muungano na Kristo Yesu. Zaidi ya hayo, ikiwa ninyi ni wa Kristo, ninyi kwa kweli ni uzao wa Abrahamu, warithi kuhusiana na ahadi.”

      Je, namba 144,000 ni ya mfano tu?

      Jibu linaonyeshwa na uhakika wa kwamba, baada ya kutajwa kwa namba halisi 144,000, andiko la Ufunuo 7:9 linataja “umati mkubwa, ambao hakuna mtu aliyeweza kuuhesabu.” Ikiwa namba 144,000 haingekuwa halisi, basi haingekuwa na maana ikilinganishwa na “umati mkubwa.” Kuiona namba hiyo kuwa halisi kunapatana na maneno ya Yesu katika Mathayo 22:14 kuhusu Ufalme wa mbinguni: “Wanaoalikwa ni wengi, lakini wanaochaguliwa ni wachache.”

      Je, “umati mkubwa” unaotajwa katika Ufunuo 7:9, 10 pia huenda mbinguni?

      Andiko la Ufunuo haliwataji kama linavyowataja wale 144,000, kwamba wao “wamenunuliwa kutoka duniani” wakawe pamoja na Kristo juu ya Mlima Sayuni wa mbinguni.—Ufu. 14:1-3.

      Maelezo kwamba “wamesimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo” si lazima yamaanishe ni mahali fulani, bali ni hali yenye kukubaliwa. (Linganisha na Ufunuo 6:17; Luka 21:36.) Maneno “mbele ya kiti cha ufalme” (Kigiriki, e·noʹpi·on tou throʹnou; kihalisi, “machoni pa kiti cha ufalme”) si lazima yamaanishe kwamba wako mbinguni. Wamesimama tu “machoni” pa Mungu, anayetuambia kwamba yeye anawaona wanadamu akiwa mbinguni.—Zab. 11:4; linganisha na Mathayo 25:31-33; Luka 1:74, 75; Matendo 10:33.

      “Umati mkubwa mbinguni” unaotajwa katika Ufunuo 19:1, 6 si sawa na ule “umati mkubwa” wa Ufunuo 7:9. Wale walio mbinguni hawasemwi kuwa ‘wametoka katika mataifa yote’ wala hawamhesabii Mwana-Kondoo wokovu wao; wao ni malaika. Maneno “umati mkubwa” yanatumiwa katika miktadha katika Biblia.—Marko 5:24; 6:34; 12:37.

      Wale wanaoenda mbinguni watafanya nini huko?

      Ufu. 20:6: “Watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye ile miaka elfu.” (Ona pia Danieli 7:27)

      1 Kor. 6:2: “Hamjui kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu?”

      Ufu. 5:10: “Ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, nao watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia.”

      Ni nani anayewachagua wale watakaoenda mbinguni?

      2 The. 2:13, 14: “Tuna wajibu wa kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, akina ndugu mnaopendwa na Yehova, kwa sababu Mungu aliwachagua ninyi tangu mwanzo kwa ajili ya wokovu kwa kuwatakasa ninyi kwa roho na kwa imani yenu katika kweli. Kwa lengo hili aliwaita ninyi kupitia habari njema tunayoitangaza, kwa kusudi la kujipatia utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.”

      Rom. 9:6, 16: “Si wote wanaotokana na Israeli ni ‘Israeli’ kikweli.   . . . Haitegemei yule anayetaka wala yule anayekimbia, bali hutegemea Mungu, aliye na rehema.”

  • Misa
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Misa

      Maana: Kama inavyoelezwa na Kundi Takatifu la Ibada za Kanisa Katoliki, Misa ni “—Dhabihu ambayo katika hiyo Dhabihu ya Msalaba inadumishwa;—Ukumbusho wa kifo na ufufuo wa Bwana, aliyesema ‘fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu’ (Luka 22:19);—Karamu takatifu ambapo, kupitia ushirika wa Mwili na Damu ya Bwana, Watu wa Mungu hushiriki faida za Dhabihu ya Pasaka, hufanya upya Agano Jipya ambalo Mungu amefanya pamoja na wanadamu mara moja kwa wakati wote kupitia Damu ya Kristo, na katika imani na tumaini hutangulia kuonyesha na kutarajia karamu ya mwisho katika ufalme wa Baba, wakitangaza kifo cha Bwana ‘hata ajapo.’” (Eucharisticum Mysterium, Mei 25, 1967) Hiyo ndiyo njia ya Kanisa Katoliki ya kufanya kile wanachoelewa kwamba Yesu Kristo alifanya katika Mlo wa Jioni wa Bwana.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki