Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Msalaba
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kama inavyoelezwa katika Ezekieli 8:17, Wayahudi waasi-imani pia ‘walinyoosha chipukizi kuelekea pua ya Yehova.’ Yeye aliliona hilo kuwa “machukizo” na kitu cha ‘kumtia uchungu.’ Kwa nini? Kulingana na maelezo ya watu fulani, “chipukizi,” lilikuwa kiwakilishi cha kiungo cha uzazi cha kiume, kilichotumiwa katika ibada ya viungo vya uzazi. Basi, Yehova ataonaje mtu anapotumia msalaba, ambao, kama tulivyokwisha kuona, ulikuwa mfano uliotumiwa zamani za kale katika ibada ya viungo vya uzazi?

  • Mungu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Mungu

      Maana: Mkuu Kuliko Wote, ambaye jina lake la pekee ni Yehova. Maneno ambayo lugha ya Kiebrania inatumia kumaanisha “Mungu” yanatoa wazo la nguvu, pia fahari, adhama, na utukufu. Kuna miungu ya uwongo, ambayo ni tofauti na Mungu wa kweli. Baadhi ya miungu hiyo imejifanya yenyewe kuwa miungu; mingine imefanywa vitu vya kuabudiwa na wale wanaoitumikia.

      Je, kuna sababu nzuri za kuamini kwamba kuna Mungu?

      Zab. 19:1: “Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu; nalo anga linatangaza kazi ya mikono yake.”

      Zab. 104:24: “Jinsi kazi zako zilivyo nyingi, Ee Yehova! Zote umezifanya kwa hekima. Dunia imejaa vitu ulivyotokeza.”

      Rom. 1:20: “Sifa zake ambazo hazionekani, zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaeleweka kwa vitu vilivyofanywa.”

      Gazeti New Scientist lilisema: “Watu wa kawaida wanaendelea kuwa na maoni kwamba wanasayansi ‘wameikana’ dini. Kulingana na maoni hayo, kwa ujumla wanasayansi hawatazamiwi kuwa waamini; wanaamini kwamba Darwin aliondoa kabisa uwezekano wa kuwapo kwa Mungu; na kwamba mfululizo wa mavumbuzi ya kisayansi na ya kitekinolojia tangu wakati huo yameondoa uwezekano wa ufufuo wowote. Maoni hayo ni yenye makosa kabisa.”—Mei 26, 1977, uku. 478.

      Mwanachama wa French Academy of Sciences alisema: “Utaratibu wa kiasili haukubuniwa na akili ya mwanadamu wala kuanzishwa na nguvu fulani zenye fahamu. . . . Kuwako kwa utaratibu kunaonyesha kwamba lazima kuwe na akili fulani yenye kupanga mambo. Akili hiyo si ya mtu mwingine bali ni ya Mungu.”—Dieu existe? Oui (Paris, 1979), Christian Chabanis, akimnukuu Pierre-Paul Grassé, uku. 94.

      Wanasayansi wametambua elementi zaidi ya 100 za kemikali. Muundo wa atomu zake unaonyesha uhusiano tata wa hesabu kati ya elementi hizo. Jedwali ya elementi huonyesha ubuni ulio wazi. Haiwezekani kwamba ubuni huo wenye kustaajabisha ulijitokeza wenyewe tu.

      Mfano: Tunapoona kamera, redio, au kompyuta, tunakubali haraka kwamba bila shaka vitu hivyo vimefanyizwa na mbuni mwenye akili. Basi, je, lingekuwa jambo linalopatana na akili kusema kwamba vitu tata zaidi—jicho, sikio, na ubongo wa mwanadamu—havikufanyizwa na Mbuni mwenye akili?

      Ona pia ukurasa wa 390-392 chini ya kichwa “Uumbaji.”

      Je, kuwako kwa uovu na kuteseka kunathibitisha kwamba hakuna Mungu?

      Fikiria mifano hii: Kwa kuwa visu vimetumiwa kuua watu, je, hilo linathibitisha kwamba hakuna mtu aliyevitengeneza? Ndege zinapotumiwa kuangusha mabomu wakati wa vita, je, hilo linathibitisha kwamba hakuna mtu aliyezitengeneza? Je, kinachomletea mwanadamu msiba si jinsi vitu hivyo vinavyotumiwa?

      Je, si kweli kwamba magonjwa mengi yanatokea kwa sababu ya mazoea mabaya ya maisha ya mwanadamu mwenyewe na kwa kujiharibia mwenyewe na wengine mazingira? Je, vita vinavyopiganwa na wanadamu si kisababishi kikubwa cha kuteseka kwa wanadamu? Je, si kweli pia kwamba, huku mamilioni wakiteseka kwa kukosa chakula, kuna chakula cha ziada katika nchi nyingine, hivi kwamba mojawapo ya matatizo ya msingi ni pupa ya wanadamu? Mambo yote hayo yanathibitisha, si kwamba hakuna Mungu, bali kwamba wanadamu kwa kusikitisha wanatumia vibaya dunia na uwezo wao waliopewa na Mungu.

      Je, kweli Mungu anajali yanayotupata sisi wanadamu?

      Ndiyo, anajali! Fikiria uthibitisho: Biblia inatuambia kwamba Mungu alimpa mwanadamu mwanzo mkamilifu. (Mwa. 1:27, 31; Kum. 32:4) Hata hivyo, ili wanadamu waendelee kuwa na kibali cha Mungu, walipaswa kumtii Muumba wao. (Mwa. 2:16, 17) Ikiwa mwanadamu angetii, angeendelea kuishi maisha makamilifu—bila ugonjwa, bila kuteseka, bila kifo. Muumba angempa mwanadamu mwongozo unaohitajiwa na angetumia uwezo Wake kumlinda mwanadamu asipate msiba wowote. Lakini mwanadamu alikataa mwongozo wa Mungu; akachagua kujitawala mwenyewe. Kwa kujaribu kufanya jambo ambalo hakukusudiwa kamwe kufanya, yeye mwenyewe amejiletea msiba. (Yer. 10:23; Mhu 8:9; Rom. 5:12) Hata hivyo, kwa miaka mingi Mungu amekuwa akitafuta kwa subira wale ambao wana nia ya kumtumikia kwa sababu wanampenda yeye na njia zake. Yeye anaweka mbele yao nafasi ya kupata baraka zote ambazo wamenyimwa kwa sababu ya kutokamilika na utawala mbaya wa wanadamu. (Ufu. 21:3-5) Uandalizi ambao Mungu alifanya kupitia Mwanawe ili kuwakomboa wanadamu katika dhambi na kifo ni uthibitisho mzuri wa upendo mkuu wa Mungu kwa wanadamu. (Yoh. 3:16) Pia Mungu ameweka wakati atakapowaharibu wale wanaoiharibu dunia naye atawafanya wale wanaopenda uadilifu waishi kupatana na kusudi lake la kwanza.—Ufu. 11:18; Zab. 37:10, 11; ona pia vichwa “Kuteseka” na “Uovu.”

      Je, Mungu ni mtu halisi?

      Ebr. 9:24: “Kristo . . . aliingia mbinguni kwenyewe, ili sasa aonekane mbele za uso wa Mungu kwa ajili yetu.”

      Yoh. 4:24: “Mungu ni Roho.”

      Yoh. 7:28: “Yule aliyenituma ni halisi,” akasema Yesu.

      1 Kor. 15:44: “Ikiwa kuna mwili wa nyama, kuna wa roho pia.”

      Je, Mungu ana hisia kama za watu walio hai?

      Yoh. 16:27: “Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu mmenipenda na mmeamini kwamba mimi nilitoka nikiwa mwakilishi wa Baba.”

      Isa. 63:9: “Wakati wa taabu zao zote hilo lilimtaabisha. . . . Katika upendo wake na katika huruma yake yeye mwenyewe aliwakomboa.”

      1 Tim. 1:11: “Mungu mwenye furaha.”

      Je, Mungu alikuwa na mwanzo?

      Zab. 90:2: “Kabla ya kuzaliwa kwa milima, au kutokezwa kwa dunia na nchi yenye kuzaa kana kwamba kwa maumivu ya kuzaa, tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo wewe ni Mungu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki