-
MunguKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
‘Mimi naamini tu kitu ninachoweza kuona, nami sijamwona Mungu kamwe’
Unaweza kujibu hivi: ‘Siku hizi watu wengi huamini hivyo. Na kuna sababu ya maoni hayo. Tunaishi katika jamii inayofuatilia mali za kimwili. Lakini wewe ni mtu anayependa uhakika, sivyo.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Je, kuna vitu fulani ambavyo hatuwezi kuona kwa macho yetu lakini tunaamini kwamba viko kwa kuwa tuna sababu nzuri za kuamini hivyo? Namna gani hewa tunayopumua? Huenda tukaihisi kunapokuwa na upepo. Tunaweza kujua inapojaa katika mapafu yetu, hata ingawa hatuioni. Kwa sababu tunaona matokeo, kuna sababu nzuri ya kuamini kwamba ipo, sivyo?’ (2) ‘Na hatuwezi kuziona nguvu za uvutano. Lakini tunapoangusha kitu fulani tunaona uthibitisho kwamba nguvu za uvutano zinatenda kazi. Wala hatuoni harufu, lakini pua yetu inainusa. Hatuwezi kuona mawimbi ya sauti, lakini masikio yetu yanayasikia. Kwa hiyo tunaamini vitu tusivyoweza kuona—maadamu kuna sababu nzuri ya kufanya hivyo, sivyo?’ (3) ‘Je, kweli kuna uthibitisho kwamba Mungu asiyeonekana yuko? (Tumia habari iliyo katika ukurasa wa 215, 216, chini ya kichwa kidogo “Je, kuna sababu nzuri za kuamini kwamba kuna Mungu?”)’
‘Mimi nina maoni yangu mwenyewe kumhusu Mungu’
Unaweza kujibu hivi: ‘Ninafurahi kusikia kwamba umelifikiria jambo hilo na kwamba unamwamini Mungu. Hebu nikuulize, Una maoni gani kumhusu Mungu?’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Nina hakika unatambua kuwa ni muhimu kuhakikisha kwamba lolote tunaloamini linapatana na yale ambayo Mungu mwenyewe anasema. Je, nikuonyeshe wazo moja tu katika Biblia kuhusu jambo hilo? (Zab. 83:18)’
-
-
NafsiKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Nafsi
Maana: Katika Biblia, neno “nafsi” hutafsiriwa kutoka neno la Kiebrania neʹphesh na neno la Kigiriki psy·kheʹ. Matumizi ya Biblia huonyesha nafsi ni mtu au mnyama au uhai wa mtu au mnyama. Hata hivyo, kwa watu wengi, “nafsi” humaanisha sehemu isiyo na mwili au roho ya mwanadamu inayoendelea kuishi baada ya kufa kwa mwili. Wengine wanaielewa kuwa ndiyo msingi wa uhai. Lakini maoni hayo ya mwisho si mafundisho ya Biblia.
-