-
MajaliwaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Efe. 1:4, 5: “[Alituchagua] katika muungano naye [Yesu Kristo] kabla ya kuwekwa msingi wa ulimwengu, ili tuwe watakatifu na bila dosari mbele zake katika upendo. Kwa maana alituagiza kimbele ili tufanywe kuwa wana kwake kupitia Yesu Kristo, kulingana na upendezi mwema wa mapenzi yake.” (Inafaa kuangaliwa kwamba, katika Luka 11:50, 51, Yesu alilinganisha “kuwekwa msingi wa ulimwengu” na wakati wa Abeli. Abeli ndiye mwanadamu wa kwanza aliyekuwa na kibali cha Mungu katika maisha yake yote. Kwa hiyo, Mungu alifanyiza kusudi lake la kuleta “uzao” ambao ungeandaa ukombozi baada ya uasi katika Edeni lakini kabla ya kuchukuliwa mimba kwa Abeli. [Mwa. 3:15] Mungu alikusudia kwamba wale wa kushirikiana na Uzao mkuu, Yesu Kristo, wangekuwa kikundi cha wafuasi wake waaminifu ambao wangeshiriki pamoja naye katika serikali mpya juu ya dunia, Ufalme wa Masihi.)
Je, nyota na sayari huongoza matukio katika maisha yetu au hutoa ishara ambazo tunapaswa kupima tunapofanya maamuzi?
Unajimu ulitoka wapi?
“Unajimu wa nchi za magharibi unaweza kufuatwa na kuonekana kwamba ulitokana na nadharia na mazoea ya Wakaldayo na Wababiloni wa miaka ya 2000 K.W.K.”—The Encyclopedia Americana (1977), Buku la 2, uku. 557.
“Unajimu ulitegemea mawazo mawili ya Babiloni: ukanda wa nyota, na uungu wa sayari za mbinguni . . . . Wababiloni waliamini sayari zina uvutano kama ule ambao mtu angetazamia kutoka kwa mungu wake.”—Great Cities of the Ancient World (New York, 1972), L. Sprague de Camp, uku. 150.
“Katika Babilonia na vilevile katika Ashuru, ufalme uliotokana moja kwa moja na utamaduni wa Babiloni . . . unajimu uko katika dini rasmi ukiwa mojawapo ya njia kuu mbili zilizotumiwa na makuhani . . . katika kutambua mapenzi na kusudi la miungu, njia nyingine ni kupitia uchunguzi wa ini la mnyama wa dhabihu. . . . Miendo ya jua, mwezi na sayari tano ilionwa kuwa inawakilisha utendaji wa miungu mitano inayohusika, pamoja na Sini, ambaye ni mungu-mwezi, na Shamashi, ambaye ni mungu-jua, katika kutayarisha matukio duniani.”—Encyclopædia Britannica (1911), Buku la Pili, uku. 796.
Muumba wa wanadamu analionaje zoea hilo?
Kum. 18:10-12: “Asipatikane ndani yako yeyote . . . anayefanya uaguzi, mwenye kufanya uchawi au yeyote anayetafuta ishara za bahati au mlozi . . . Kwa maana kila mtu anayefanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova.”
Aliwaambia Wababiloni hivi: “Na wasimame, sasa, na kukuokoa, wanaoabudu mbingu, watazamaji wa nyota, ambao kwenye miezi mipya wanajulisha habari za mambo yatakayokuja juu yako. Tazama! Wamekuwa kama majani makavu. . . . Wale ambao umefanya kazi pamoja nao kama wachawi wako tangu ujana wako. Kwa kweli watatanga-tanga, kila mmoja kwenda katika eneo lake mwenyewe. Hakutakuwa na yeyote wa kukuokoa.”—Isa. 47:13-15.
-
-
Manabii wa UwongoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Manabii wa Uwongo
Maana: Mtu mmoja-mmoja na mashirika yanayotangaza ujumbe ambao wanadai hautoki kwa wanadamu, lakini ujumbe huo hautoki kwa Mungu wa kweli na haupatani na mapenzi yake yaliyofunuliwa.
Manabii wa kweli na wa uwongo wanaweza kutambuliwaje?
Manabii wa kweli hutangaza imani yao katika Yesu, lakini mengi yanahitajiwa kuliko kudai kuhubiri katika jina lake
1 Yoh. 4:1-3: “Yajaribuni maneno yaliyoongozwa na roho ili kuona kama yanatokana na Mungu, kwa sababu manabii wengi wa uwongo wameingia ulimwenguni. Mnalijua neno lililoongozwa na roho kutoka kwa Mungu kwa njia hii: Kila neno lililoongozwa na roho linalomkiri Yesu Kristo kuwa alikuja katika mwili hutokana na Mungu, lakini kila neno lililoongozwa na roho ambalo halimkiri Yesu halitokani na Mungu.”
Mt. 7:21-23: “Si kila mtu anayeniambia, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika ufalme wa mbinguni, bali yule anayefanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni ndiye atakayeingia. Wengi wataniambia siku hiyo, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii katika jina lako . . . ?’ Na hata hivyo nitawaambia waziwazi: Sikuwajua ninyi kamwe! Ondokeni kwangu, ninyi wenye matendo ya uasi-sheria.”
Manabii wa kweli hutumia jina la Mungu, lakini kudai tu kumwakilisha hakutoshi
Kum. 18:18-20: “Nitawainulia wao nabii kutoka katikati ya ndugu zao, kama wewe; nami nitaweka maneno yangu katika kinywa chake, naye atasema nao yote nitakayomwamuru. Na itatukia kwamba mtu ambaye hatasikiliza maneno yangu ambayo atayasema katika jina langu, mimi mwenyewe nitamtaka ajibu. Hata hivyo, nabii atakayethubutu kusema katika jina langu neno ambalo sijamwamuru kusema au atakayesema katika jina la miungu mingine, nabii huyo lazima afe.” (Linganisha na Yeremia 14:14; 28:11, 15.)
-