-
DamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Unaweza kujibu hivi: ‘Ikiwa hali ni mbaya sana hivyo, je, daktari huyo anaweza kukuhakikishia kwamba mgonjwa huyo hatakufa akitiwa damu?’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Lakini kuna mtu anayeweza kumrudishia mtu uhai, naye ni Mungu. Je, hukubali kwamba, unapokaribia kufa, kuamua kumwacha Mungu kwa kuvunja sheria yake kungekuwa kosa? Kwa kweli mimi ninamwamini Mungu. Namna gani wewe? Neno lake linawaahidi ufufuo wale wanaomwamini Mwanawe. Je, wewe unaamini hivyo? (Yoh. 11:25)’
Au unaweza kusema: ‘Huenda ikamaanisha kwamba yeye mwenyewe hajui jinsi ya kushughulikia kisa hicho bila kutumia damu. Inapowezekana, sisi hujaribu kumwelekeza kwa daktari ambaye amepata ujuzi unaohitajiwa, au tunamwendea daktari mwingine.’
-
-
Dawa za KulevyaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Dawa za Kulevya
Maana: Kuna maana mbalimbali za neno “dawa.” Katika sehemu hii, tutazungumzia dawa za kulevya, ambazo si vyakula, bali ni vitu vinavyobadili tabia ambavyo havionwi kuwa vya lazima kitiba. Watu huvitumia kujaribu kuepuka matatizo ya maisha, ili kupata hisia kama ya ndoto, au hali ya kuhisi vizuri au kusisimuka.
Je, kwa kweli Biblia inakataza kutumia dawa za kulevya ili kupata raha?
Biblia haitaji kwa jina vitu kama heroini, kokeini, LSD, PCP, bangi, na tumbaku. Lakini inatoa miongozo inayohitajiwa ili tujue jambo la kufanya na la kuepuka ili tumpendeze Mungu. Vivyo hivyo, Biblia haisemi kwamba ni kosa kutumia bunduki kumuua mtu, lakini inakataza uuaji.
Luka 10:25-27: “‘Nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?’ . . . ‘“Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote,” na, “jirani yako kama wewe mwenyewe.”’” (Je, kweli mtu anampenda Mungu kwa nafsi yake yote na akili yake yote ikiwa anatenda mambo yanayofupisha maisha yake bila sababu na kufanya akili zake zipumbazike? Je, anampenda jirani yake ikiwa anawaibia wengine ili aendeleze tabia yake ya kutumia dawa za kulevya?)
2 Kor. 7:1: “Kwa kuwa tuna ahadi hizi [za Yehova kuwa Mungu na Baba yetu], acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi wa mwili na roho, tukiukamilisha utakatifu katika kumwogopa Mungu.” (Lakini je, tunaweza kutarajia kukubaliwa na Mungu ikiwa tunafanya kimakusudi mambo yanayochafua miili yetu?)
Tito 2:11, 12: “Fadhili zisizostahiliwa za Mungu zinazowaletea watu wa namna zote wokovu zimeonyeshwa, zikitufundisha kukataa kabisa kutomwogopa Mungu na tamaa za kilimwengu na tuishi kwa utimamu wa akili na uadilifu na ujitoaji-kimungu katikati ya mfumo wa mambo wa sasa.” (Je, kutumia dawa za kulevya zinazoharibu uamuzi wa mtu au zinazofanya mtu ashindwe kujizuia kunapatana na shauri hilo?)
Gal. 5:19-21: “Sasa matendo ya mwili ni wazi, nayo ni . . . mazoea ya kuwasiliana na pepo, . . . karamu za kupindukia, na mambo kama hayo. . . . Wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” (Maana halisi ya neno la Kigiriki phar·ma·kiʹa, linalotafsiriwa hapa “mazoea ya kuwasiliana na pepo,” ni “matumizi ya dawa za kulevya.” Ikitoa maelezo kuhusu neno hilo la Kigiriki, An Expository Dictionary of New Testament Words, ya W. E. Vine inasema hivi: “Katika uchawi, matumizi ya dawa za kulevya, ziwe ni nyepesi au kali, kwa ujumla yalifuatana na utamkaji wa maneno ya uganga na kuomba nguvu za uchawi, pamoja na uandalizi wa hirizi mbalimbali, talasimu, n.k., zinazodaiwa zimekusudiwa kumlinda mwombaji au mgonjwa asifuatwe na nguvu za roho waovu, lakini ambazo kwa kweli zimekusudiwa kumvutia mwombaji kwa uwezo wa kifumbo na nguvu za mchawi.” [London, 1940, Buku la 4, uku. 51, 52] Hali kadhalika leo, wengi wanaotumia dawa za kulevya wanajitia katika mazoea ya kuwasiliana na pepo au wanashirikiana na wale wanaowasiliana na pepo, kwa sababu akili iliyo tupu au mtu anayeona au kusikia vitu visivyokuwako huwa rahisi kupagawa na roho waovu. Linganisha na Luka 11:24-26.)
Tito 3:1: “Wajitiishe na kuzitii serikali na mamlaka zikiwa watawala.” (Katika nchi nyingi, kuwa na dawa fulani za kulevya au kuzitumia ni kuvunja sheria.)
Kwa kuwa dawa fulani za kulevya huenda zikamsisimua mtu, je, kweli ni hatari sana?
2 Tim. 3:1-5: “Katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo. Kwa maana watu watakuwa . . . wanaopenda raha badala ya kumpenda Mungu . . . Nawe geukia mbali kutoka kwa hao.” (Ni wazi kwamba Biblia inaonya kuhusu kutamani raha sana hivi kwamba tunaitanguliza maishani badala ya kufuata kanuni za uadilifu za Neno la Mungu na kupata kibali chake.)
-