Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Dawa za Kulevya
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • “Uchunguzi uliofanywa hivi karibuni . . . ulifunua kwamba wake wasiovuta sigara ambao waume wao huvuta sigara, kwa wastani hufa miaka minne mapema kuliko wanawake ambao waume wao si wavutaji wa sigara.” (The New York Times, Novemba 22, 1978, uku. C5) “Mwanamke anapovuta sigara akiwa mjamzito anaweza kumsababishia mtoto aliye tumboni kasoro mbaya sana hivi kwamba mtoto huyo anaweza kufa akiwa tumboni, au mara tu baada ya kuzaliwa.” (Family Health, Mei 1979, uku. 8) Mtu ambaye anawatendea washiriki wa familia yake kwa njia hiyo isiyo ya upendo anathibitisha wazi kwamba hajiendeshi kama Mkristo.—Linganisha na 1 Timotheo 5:8.

      “Uchunguzi umeonyesha kwamba kwa kuwa mvutaji wa kawaida anavuta sana sigara yake kwa sehemu ndogo tu wakati inapokuwa imewashwa, huenda mtu asiyevuta sigara ambaye ameketi karibu naye akalazimika kuvuta karibu kiasi kilekile cha kaboni monoksidi, lami na nikotini kama yule mvutaji.” (Today’s Health, Aprili 1972, uku. 39) Basi mvutaji wa sigara hampendi mwanadamu mwenzake, na hivyo haonyeshi uthibitisho wa kumpenda Mungu.—Ona 1 Yohana 4:20.

      Ikiwa ni kosa kutumia dawa za kulevya, kwa nini Mungu aliumba mimea inayotokeza dawa hizo?

      Vitu vinavyotumiwa vibaya kwa kawaida vina matumizi yanayofaa pia. Ndivyo ilivyo na viungo vya uzazi vya mwanadamu. Ndivyo ilivyo na divai. Bangi hutokana na majani makavu na maua ya mbangi, ambao hutokeza nyuzi nzuri za kutengeneza kamba na nguo. Majani ya tumbaku, yanayotumiwa vibaya na wavutaji, yanaweza pia kutumiwa kutengeneza dawa za kuua viini vya ugonjwa na wadudu. Mambo mengi hayajajulikana kuhusu jinsi vitu vingi vilivyo duniani vinavyoweza kutumiwa kwa njia yenye kuleta faida. Hata magugu yana faida katika kuzuia mmomonyoko wa udongo na kutia udongo mbolea wakati ambapo haulimwi.

      Mtu anaweza kufanya nini ikiwa amejaribu kuacha kuvuta sigara au kutumia dawa za kulevya lakini hajafanikiwa?

      Kwanza, kwa kujifunza Biblia na kutafakari unahitaji kusitawisha tamaa yenye nguvu ya kumpendeza Mungu na kuishi katika mfumo wake mpya wa mambo wenye uadilifu. Ukimkaribia, atakukaribia, naye atakupa msaada unaohitaji.— Yak. 4:8.

      Ni muhimu mtu asadiki ubaya wa mazoea hayo na kuyachukia kikweli. (Zab. 97:10) Jambo hilo linaweza kufanywa kwa kurudia mambo ya hakika yaliyoandikwa katika sehemu hii ya kitabu na kutafakari, si juu ya raha za muda za sasa ambazo huenda zikatokana na mazoea hayo, bali juu ya yale yanayompendeza Mungu na jinsi matokeo ya mazoea mabaya yanavyochukiza sana.

      Ikiwa unatamani sana kuvuta sigara au kutumia moja kati ya zile dawa nyingine za kulevya, sali kwa Mungu kwa bidii ili akusaidie. (Luka 11:9, 13; linganisha na Wafilipi 4:13.) Fanya hivyo bila kukawia. Pia, chukua Biblia yako na uisome kwa sauti kubwa, au mwendee Mkristo aliyekomaa. Mwambie yanayokupata na umwombe msaada.

  • Dhambi
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Dhambi

      Maana: Kulingana na maandishi ya Biblia ya Kiebrania na Kigiriki, dhambi ni kukosa alama. Mungu mwenyewe huweka “alama” ambayo viumbe wake wenye akili wanapaswa kufikia. Kukosa kufikia alama hiyo ni dhambi, ambayo pia ni ukosefu wa uadilifu, au uasi-sheria. (Rom. 3:23; 1 Yoh. 5:17; 3:4) Dhambi ni chochote ambacho hakipatani na utu wa Mungu, viwango vyake, njia, na mapenzi yake, ambayo yote ni matakatifu. Huenda ikatia ndani mwenendo mbaya, mtu kushindwa kufanya anayopaswa kufanya, maneno mabaya, mawazo machafu, au tamaa au nia ambazo ni za ubinafsi. Biblia inatofautisha kati ya dhambi iliyorithiwa na dhambi ya kukusudiwa, kati ya tendo la dhambi ambalo mtu anatubia na zoea la kutenda dhambi.

      Iliwezekanaje Adamu afanye dhambi ikiwa alikuwa mkamilifu?

      Kuhusu habari ya Adamu kuwa mkamilifu, soma Mwanzo 1:27, 31 na Kumbukumbu la Torati 32:4. Yehova Mungu alipotangaza uumbaji wake wa duniani, kutia ndani mwanamume na mwanamke, kuwa kitu “chema sana,” alimaanisha nini? Ili Mungu, ambaye kazi yake ni kamilifu, aseme kwamba kile alichoumba kilikuwa “chema sana,” ni lazima kilifikia viwango vyake vikamilifu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki