-
Har–MagedoniKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
2 The. 1:6: “Ni jambo la uadilifu kwa upande wa Mungu kuwalipa dhiki wale wanaowafanyia ninyi [watumishi wake] dhiki.”
Je, inawezekana kutounga mkono upande wowote?
2 The. 1:8: “Anapoleta kisasi juu ya wale wasiomjua Mungu [kwa kuchagua] na wale wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.”
Mt. 24:37-39: “Kama vile siku za Noa zilivyokuwa . . . hawakujali mpaka gharika ikaja na kuwafagilia mbali wote, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa.”
Mt. 12:30: “Yeye asiyekuwa upande wangu ananipinga, naye asiyekusanya pamoja nami anatawanya.”
Linganisha na Kumbukumbu la Torati 30:19, 20.
Ni nani anayeyachochea mataifa kwenye hali ya ulimwengu itakayotokeza vita dhidi ya Mungu?
Ufu. 16:13, 14; 12:9: “Nikaona maneno machafu matatu yaliyoongozwa na roho ambayo yalionekana kama vyura yakitoka katika kinywa cha yule joka mkubwa [Shetani Ibilisi; Ufu. 12:9] na kutoka katika kinywa cha yule mnyama-mwitu na kutoka katika kinywa cha yule nabii wa uwongo. Hayo, kwa kweli, ni maneno yanayoongozwa na roho waovu nayo yanafanya ishara, nayo yanakwenda kwa wafalme wa dunia nzima inayokaliwa, ili kuwakusanya pamoja kwa vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.”
Linganisha na Luka 4:5, 6; 1 Yohana 5:19; pia Matendo 5:38, 39; 2 Mambo ya Nyakati 32:1, 16, 17.
-
-
Ibada ya MababuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Ibada ya Mababu
Maana: Zoea la kuwaheshimu na kuwaabudu mababu waliokufa (kwa kufanya sherehe au kwa njia nyingine) kwa sababu wanaamini kwamba mababu hao wanaishi katika makao yasiyoonekana na wanaweza kuwasaidia au kuwadhuru walio hai na kwa hiyo wanapaswa kutulizwa. Hilo si fundisho la Biblia.
-