Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Dawa za Kulevya
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kwanza, kwa kujifunza Biblia na kutafakari unahitaji kusitawisha tamaa yenye nguvu ya kumpendeza Mungu na kuishi katika mfumo wake mpya wa mambo wenye uadilifu. Ukimkaribia, atakukaribia, naye atakupa msaada unaohitaji.— Yak. 4:8.

      Ni muhimu mtu asadiki ubaya wa mazoea hayo na kuyachukia kikweli. (Zab. 97:10) Jambo hilo linaweza kufanywa kwa kurudia mambo ya hakika yaliyoandikwa katika sehemu hii ya kitabu na kutafakari, si juu ya raha za muda za sasa ambazo huenda zikatokana na mazoea hayo, bali juu ya yale yanayompendeza Mungu na jinsi matokeo ya mazoea mabaya yanavyochukiza sana.

      Ikiwa unatamani sana kuvuta sigara au kutumia moja kati ya zile dawa nyingine za kulevya, sali kwa Mungu kwa bidii ili akusaidie. (Luka 11:9, 13; linganisha na Wafilipi 4:13.) Fanya hivyo bila kukawia. Pia, chukua Biblia yako na uisome kwa sauti kubwa, au mwendee Mkristo aliyekomaa. Mwambie yanayokupata na umwombe msaada.

  • Dhambi
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Dhambi

      Maana: Kulingana na maandishi ya Biblia ya Kiebrania na Kigiriki, dhambi ni kukosa alama. Mungu mwenyewe huweka “alama” ambayo viumbe wake wenye akili wanapaswa kufikia. Kukosa kufikia alama hiyo ni dhambi, ambayo pia ni ukosefu wa uadilifu, au uasi-sheria. (Rom. 3:23; 1 Yoh. 5:17; 3:4) Dhambi ni chochote ambacho hakipatani na utu wa Mungu, viwango vyake, njia, na mapenzi yake, ambayo yote ni matakatifu. Huenda ikatia ndani mwenendo mbaya, mtu kushindwa kufanya anayopaswa kufanya, maneno mabaya, mawazo machafu, au tamaa au nia ambazo ni za ubinafsi. Biblia inatofautisha kati ya dhambi iliyorithiwa na dhambi ya kukusudiwa, kati ya tendo la dhambi ambalo mtu anatubia na zoea la kutenda dhambi.

      Iliwezekanaje Adamu afanye dhambi ikiwa alikuwa mkamilifu?

      Kuhusu habari ya Adamu kuwa mkamilifu, soma Mwanzo 1:27, 31 na Kumbukumbu la Torati 32:4. Yehova Mungu alipotangaza uumbaji wake wa duniani, kutia ndani mwanamume na mwanamke, kuwa kitu “chema sana,” alimaanisha nini? Ili Mungu, ambaye kazi yake ni kamilifu, aseme kwamba kile alichoumba kilikuwa “chema sana,” ni lazima kilifikia viwango vyake vikamilifu.

      Je, ukamilifu ulimaanisha kwamba Adamu na Hawa hawawezi kufanya kosa? Mtu anayetengeneza roboti huitarajia itende sawasawa na alivyoipangia kutenda. Lakini roboti kamilifu haiwezi kuwa mwanadamu mkamilifu. Sifa zinazoonwa kuwa za lazima hazifanani. Adamu na Hawa walikuwa wanadamu, si roboti. Mungu aliwapa wanadamu uwezo wa kuchagua kati ya mema na mabaya, kati ya kutii na kutotii, kufanya maamuzi ya kiadili. Kwa kuwa wanadamu waliumbwa hivyo, kutoweza kufanya maamuzi hayo (na si uamuzi usio wa hekima) ndiko kungeonyesha kutokamilika.—Linganisha na Kumbukumbu la Torati 30:19, 20; Yoshua 24:15.

      Ili isemwe kwamba Adamu na Hawa waliumbwa wakamilifu, je, ni lazima maamuzi yao yote yawe sawa baada ya kuumbwa? Hilo lingemaanisha kwamba hawakuwa na uchaguzi. Lakini Mungu hakuwaumba kwa njia ya kwamba watii tu bila kutaka. Mungu aliwapa uwezo wa kuchagua, ili waweze kutii kwa sababu walimpenda. Au, wakiruhusu mioyo yao iwe na ubinafsi, wangekuwa wasiotii. Ni jambo gani la maana zaidi kwako—mtu anapokufanyia jambo fulani kwa sababu amelazimishwa kulifanya au kwa sababu anataka kulifanya?—Linganisha na Kumbukumbu la Torati 11:1; 1 Yohana 5:3.

      Watu hao wakamilifu wangewezaje kuwa na ubinafsi, na kutenda dhambi? Ijapokuwa waliumbwa wakiwa wakamilifu, miili yao haingeendelea kutenda kazi kikamilifu ikiwa haingelishwa chakula kinachofaa. Vivyo hivyo, pia, ikiwa wangeruhusu akili zilishwe mawazo mabaya, hilo lingesababisha uharibifu wa kiadili, kutokuwa watakatifu. Andiko la Yakobo 1:14, 15 linasema hivi: “Kila mtu hujaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe. Kisha tamaa, wakati imetunga mimba, huzaa dhambi; nayo dhambi, wakati imetimizwa, huleta kifo.” Kwa habari ya Hawa, tamaa mbaya zilianza kusitawi alipomsikiliza Shetani, aliyesema kwa kutumia nyoka. Adamu alimtii mke wake wakati alipomsihi ajiunge naye kula tunda lililokatazwa. Badala ya kuyakataa mawazo mabaya, watu hao wawili walisitawisha tamaa za ubinafsi. Dhambi ikatokea.—Mwa. 3:1-6.

      Je, dhambi ya Adamu ilikuwa sehemu ya “mpango wa Mungu?”

      Ona ukurasa wa 27, chini ya kichwa “Adamu na Hawa,” pia ukurasa wa 172, 173, chini ya kichwa “Majaliwa.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki