Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sala
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Isa. 42:8, ZSB; Mt. 4:10, UV: “Mimi ni BWANA [“Yehova,” NW], ndilo jina langu; na utukufu wangu sitamupa mwingine, wala sanamu ya kuchonga sifa zangu.” “Msujudie Bwana Mungu [“Yehova Mungu,” NW] wako, umwabudu yeye peke yake.” (Pia Zaburi 113:4-8 [115:4-8], VB) (Sala ni namna ya ibada. Ukisali mbele ya vitu vya kuchongwa, au sanamu, je, hilo litampendeza Mungu?)

      Isa. 8:19: “Nao wakiwaambia ninyi: ‘Toeni maombi kwa wenye kuwasiliana na pepo au kwa wale wenye roho ya kubashiri wanaonong’oneza na kusema maneno kwa sauti za chini,’ je, kundi lolote la watu halipaswi kutoa maombi kwa Mungu wake? Je, maombi yatolewe kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?”

      Yak. 1:6, 7: “Na aendelee kuomba kwa imani, bila kutia shaka hata kidogo, kwa maana yeye anayetia shaka ni kama wimbi la bahari linaloendeshwa na upepo na kupeperushwa huku na huku. Kwa kweli, mtu huyo asidhani kwamba atapokea kitu chochote kutoka kwa Yehova.”

      Ni mambo gani yanayofaa kutolewa sala?

      Mt. 6:9-13: “Basi, ninyi msali hivi: ‘[1] Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. [2] Ufalme wako na uje. [3] Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni. [4] Utupe leo mkate wetu kwa ajili ya siku hii; na [5] utusamehe madeni yetu, kama vile ambavyo sisi pia tumewasamehe wadeni wetu. Na [6] usituingize katika jaribu, bali utukomboe kutokana na yule mwovu.’” (Ona kwamba jina la Mungu na kusudi lake vinapaswa kutangulizwa.)

      Zab. 25:4, 5: “Nijulishe njia zako, Ee Yehova; nifundishe mapito yako mwenyewe. Nitembeze katika kweli yako na kunifundisha, kwa maana wewe ni Mungu wangu wa wokovu.”

      Luka 11:13: “Ikiwa ninyi, mjapokuwa waovu, mnajua jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi zilizo njema, je, Baba aliye mbinguni hatawapa hata zaidi roho takatifu wale wanaomwomba!”

      1 The. 5:17, 18: “Salini bila kuacha. Kuhusiana na kila jambo toeni shukrani.”

      Mt. 14:19, 20: “[Yesu] akachukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akatoa baraka na, baada ya kuimega ile mikate, akawagawia wanafunzi, nao wanafunzi wakaugawia ule umati. Kwa hiyo wote wakala wakashiba.”

      Yak. 5:16: “[M]sali kwa ajili ya mtu na mwenzake.”

      Mt. 26:41: “Endeleeni kukesha na kusali sikuzote, ili msiingie katika jaribu.”

      Flp. 4:6: “Msihangaike juu ya kitu chochote, bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu.”

      Mtu Akisema—

      ‘Tuombe kwanza, kisha unipe ujumbe wako’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Ninafurahi kujua kwamba wewe unafahamu umuhimu wa sala. Mashahidi wa Yehova pia husali kwa ukawaida. Lakini kuna jambo ambalo Yesu alisema kuhusu wakati na jinsi ya kusali ambalo huenda likawa jipya kwako. Je, unajua kwamba aliwaambia wanafunzi wake wasisali hadharani ili wengine waone kwamba wao ni watu wa dini, watu wenye kusali? . . . (Mt. 6:5)’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Ona yale ambayo alisema tunapaswa kuyahangaikia zaidi na ambayo tunapaswa kutanguliza katika sala zetu. Hayo ndiyo mambo ambayo nimekuja kukueleza. (Mt. 6:9, 10)’

      Au unaweza kusema: ‘Ninajua kwamba washiriki wa vikundi fulani vya kidini hufanya hivyo. Lakini Mashahidi wa Yehova hawafanyi hivyo, kwa sababu Yesu aliwaagiza wanafunzi wake wafanye kazi yao ya kuhubiri kwa njia tofauti. Badala ya kusema, “mnapoingia ndani ya nyumba, salini kwanza,” ona aliyosema, kama yalivyoandikwa katika Mathayo 10:12, 13. . . . Na ona hapa katika mstari wa 7 jambo walilopaswa kuzungumzia. . . . Ufalme huo unaweza kuwasaidiaje watu kama mimi na wewe? (Ufu. 21:4)’

  • Sanamu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Sanamu

      Maana: Viwakilishi vinavyoonekana vya watu au vitu. Wale wanaoabudu sanamu mara nyingi husema kwamba wanamwabudu roho anayewakilishwa na sanamu hiyo. Dini nyingi zisizo za Kikristo hutumia sanamu. Kuhusu desturi ya Kanisa Katoliki, New Catholic Encyclopedia (1967, Buku la 7, uku. 372) husema hivi: “Kwa kuwa mtu anapoabudu sanamu huwa anamwabudu mtu anayewakilishwa na sanamu hiyo, vivyo hivyo ibada anayostahili mtu huyo inaweza kutolewa kwa sanamu inayomwakilisha.” Hilo si fundisho la Biblia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki