-
UhaiKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Je, kuna uhai katika sayari nyingine?
Gazeti The New York Times linasema hivi: “Kutafutwa kwa viumbe vyenye akili kwingineko ulimwenguni . . . kulianza miaka 25 iliyopita . . . Kazi hiyo kubwa mno inayohusisha kuchunguza mamia ya mabilioni ya nyota, kufikia sasa haijatoa uthibitisho ulio wazi kwamba kuna uhai nje ya Dunia.”—Julai 2, 1984, uku. A1.
The Encyclopedia Americana yasema: “Hakuna sayari nyingine [nje ya mfumo wetu wa jua] ambazo zimeonekana waziwazi. Lakini kwa kila sayari ambayo huenda iko nje ya mfumo wa jua, kuna uwezekano wa kwamba uhai ulianza, kisha ukageuka na kuingia katika ustaarabu ulioendelea.” (1977, Buku la 22, uku. 176) (Tangu wakati huo, sayari nyingi zimegunduliwa nje ya mfumo wetu wa jua, lakini hakuna uthibitisho wowote wa kwamba kuna uhai katika yoyote ya sayari hizo. Hata hivyo, kama maneno hayo yanavyoonyesha, je, inawezekana kwamba sababu kubwa ya kazi hiyo yenye gharama kubwa sana ya kutafuta viumbe vingine katika anga la juu ni ile tamaa ya kupata uthibitisho wa nadharia ya mageuzi, uthibitisho fulani wa kwamba mwanadamu hakuumbwa na Mungu na kwa hiyo hawezi kutozwa hesabu na Yeye?)
Biblia inafunua kwamba uhai hauko katika dunia hii peke yake. Kuna watu wa roho—Mungu na malaika—ambao akili na uwezo wao unapita wa mwanadamu kwa mbali sana. Tayari wamewasiliana na wanadamu, wakieleza asili ya uhai na utatuzi wa matatizo mazito yanayoukabili ulimwengu. (Ona vichwa “Biblia” na “Mungu.”)
-
-
UhuruKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Uhuru
Maana: Hali ya kutowategemea wengine, kutotii mwelekezo wao au uvutano wao. Kwa kuwa wana uhuru wa kuchagua, kiasili wanadamu hutamani kuwa na kadiri fulani ya uhuru. Hata hivyo, inapopita kiasi, tamaa hiyo inaweza kutokeza kutotii, au hata uasi.
Watu wanapopuuza viwango vya Biblia, je, kwa kweli wanapata uhuru?
Rom. 6:16, 23: “Je, hamjui kwamba ikiwa mnaendelea kujitoa wenyewe kwa yeyote kuwa watumwa ili kumtii yeye, ninyi ni watumwa wake kwa sababu mnamtii yeye, ama watumwa wa dhambi kwa kutazamia kifo ama wa utii kwa kutazamia uadilifu? . . . Mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo, lakini zawadi ambayo Mungu hutoa ni uzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.”
-