-
Shetani IbilisiKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Shetani ataruhusiwa kuwapotosha wanadamu mpaka wakati gani?
Ili kupata uthibitisho kwamba tunaishi katika siku za mwisho za mfumo mbovu wa mambo wa Shetani, ona ukurasa wa 397-400, chini ya kichwa “Vipindi vya Wakati,” na vilevile ona kichwa “Siku za Mwisho.”
Kitulizo kutoka katika uvutano mwovu wa Shetani kinafafanuliwa kwa njia hii ya mfano: “Nikamwona malaika akishuka kutoka mbinguni mwenye ufunguo wa abiso na mnyororo mkubwa mkononi mwake. Naye akamkamata yule joka mkubwa, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, na kumfunga kwa miaka elfu. Naye akamtupa ndani ya abiso na kuifunga na kuitia muhuri juu yake, ili asipotoshe mataifa tena mpaka ile miaka elfu itakapokwisha. Baada ya mambo hayo yeye atafunguliwa kwa muda kidogo.” (Ufu. 20:1-3) Halafu nini? “Ibilisi aliyekuwa akiwapotosha alitupwa ndani ya lile ziwa la moto na kiberiti.” (Ufu. 20:10) Hilo linamaanisha nini? Andiko la Ufunuo 21:8 linajibu hivi: “Hili linamaanisha kifo cha pili.” Atatoweka milele!
Je, Shetani kutupwa katika “abiso” humaanisha kwamba atafungiwa kwa miaka 1,000 katika dunia iliyo ukiwa ambayo haina mtu ambaye yeye atamshawishi?
Watu fulani hurejezea andiko la Ufunuo 20:3 (lililonukuliwa hapo juu) ili kuunga mkono wazo hilo. Wao husema kwamba “abiso,” au “shimo pasipo mwisho” (ZSB), huwakilisha dunia ikiwa katika hali ya ukiwa. Je, hiyo ni kweli? Andiko la Ufunuo 12:7-9, 12, (ZSB) huonyesha kwamba wakati fulani kabla ya kutupwa kwake katika abiso, Shetani ‘anatupwa’ kutoka mbinguni kuja duniani, ambako anawaletea wanadamu ole nyingi. Kwa hiyo, wakati andiko la Ufunuo 20:3 (ZSB) linaposema kwamba Shetani ‘anatupwa katika shimo pasipo mwisho,’ hakika haachwi tu mahali alipo tayari—akiwa bila kuonekana lakini akiwa amefungiwa katika ujirani wa dunia. Yeye anaondolewa na kupelekwa mbali kutoka hapo, ili “asipate kudanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie.” Ona kwamba andiko la Ufunuo 20:3 linasema kwamba, mwishoni mwa ile miaka elfu, si mataifa yanayofunguliwa kutoka katika abiso, bali ni Shetani. Shetani atakapofunguliwa, watu ambao hapo zamani walifanyiza mataifa hayo watakuwa tayari wapo.
Nyakati nyingine, andiko la Isaya 24:1-6 na Yeremia 4:23-29 (UV) hutumiwa kuunga mkono imani hiyo. Maandiko hayo yanasema hivi: “Tazama, BWANA ameifanya dunia kuwa tupu, aifanya ukiwa . . . dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana BWANA amenena neno hilo.” “Naliiangalia nchi, na tazama, ilikuwa ukiwa . . . Nikaangalia, na tazama, hapakuwa na mtu hata mmoja . . . Maana BWANA asema hivi, Nchi yote itakuwa ukiwa . . . Kila mji umeachwa, hapana hata mtu mmoja akaaye ndani yake.” Unabii huo unamaanisha nini? Ulitimizwa mara ya kwanza juu ya Yerusalemu na nchi ya Yuda. Katika kutekeleza hukumu yake, Yehova aliwaruhusu Wababiloni waishambulie nchi hiyo. Mwishowe yote iliachwa ukiwa, bila kitu. (Ona Yeremia 36:29.) Lakini Mungu wakati huo hakuwaondoa watu katika dunia yote, wala hatafanya hivyo sasa. (Ona ukurasa wa 69-72, chini ya kichwa “Dunia,” pia kichwa “Mbingu.”) Hata hivyo, ataifanya ukiwa kabisa sehemu ya kisasa inayofananishwa na Yerusalemu lisilo na uaminifu, yaani, Jumuiya ya Wakristo, ambayo kwa mwenendo wake usio mtakatifu inalishutumu jina la Mungu, na sehemu nyingine zote za tengenezo la Shetani linaloonekana.
Badala ya kuwa ukiwa kabisa, wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo, na wakati Shetani atakapokuwa katika abiso, dunia yote itakuwa paradiso. (Ona “Paradiso.”)
-
-
SikukuuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Sikukuu
Maana: Siku ambazo watu hawaendi kazini na shuleni ili kuadhimisha tukio fulani. Huenda siku hizo pia zikawa vipindi vya sherehe za familia au za jamii. Huenda washiriki wakaziona kuwa ni sikukuu za kidini au za kijamii au kilimwengu.
Je, mwadhimisho wa Krismasi unapatana na Biblia?
Tarehe ya mwadhimisho
Cyclopædia ya M’Clintock na Strong inasema: “Mungu hakuagiza Krismasi iadhimishwe, wala mwadhimisho huo hautokani na A[gano] J[ipya]. A[gano] J[ipya] wala chanzo kingine chochote, hakitaji siku ya kuzaliwa kwa Kristo.”—(New York, 1871) Buku la 2, uku. 276.
-