-
MisaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Je, yote hayo ni “fumbo lisiloweza kufahamika”?
Biblia inasema kuhusu mafumbo ya Mungu, au siri takatifu. Lakini hakuna moja la mafumbo hayo linalopingana na kweli za Kimaandiko zilizoandikwa waziwazi. Kuhusu wale waliotanguliza mapokeo yao badala ya Maandiko, Yesu alisema: “Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema, Watu hawa huniheshimu kwa midomo; ila mioyo yao iko mbali nami. Nao waniabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu.”—Mt. 15:7-9, UV.
Je, Yesu alikusudia ukumbusho huo ufanywe labda kila siku au kila juma?
Kichapo Basic Catechism kinasema: “Kazi za Pekee za Wakristo Wakatoliki” hutia ndani “kushiriki Misa kila Jumapili na sikukuu ya amri.” (Boston, 1980, uku. 21) “Kwa hakika waamini wanatiwa moyo kushiriki Misa na kupokea Komunyo mara kwa mara, hata kila siku.”—The Teaching of Christ—A Catholic Catechism for Adults, Chapa Iliyofupishwa (Huntington, Ind.; 1979), uku. 281.
Je, marejeo yote katika Maandiko kuhusu “kuumega mkate” yanaonyesha kwamba kifo cha Kristo kilikuwa kikikumbukwa? (Mdo. 2:42, 46; 20:7, UV) Yesu ‘aliimega mikate’ walipokuwa wakila chakula hata kabla ya Mlo wa Jioni wa Bwana. (Marko 6:41; 8:6) Mkate uliotumiwa na Wayahudi wakati huo haukuwa ule ambao watu wengi wanaujua leo. Wakati wa kuula, mara nyingi waliumega au kukata kipande.
Yesu hakutaja waziwazi Ukumbusho wa kifo chake ulipaswa kufanywa mara ngapi. Hata hivyo, aliuanzisha kwenye tarehe ya Pasaka ya Wayahudi, sikukuu ambayo, kwa wanafunzi wake, mahali pake palichukuliwa na Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Pasaka ilikuwa sherehe ya kila mwaka, iliyofanywa Nisani 14. Vivyo hivyo, sherehe za Wayahudi, yaani, Sherehe ya Keki Zisizo na Chachu, Sherehe ya Majuma (Pentekoste), Sherehe ya Vibanda, au ya Kukusanya, na Siku ya Upatanisho zote zilifanywa mara moja kila mwaka.
Je, kutolewa kwa Misa kunazisaidia nafsi zilizo toharani (purgatori)?
Kichapo The Teaching of Christ—A Catholic Catechism for Adults kinasema: “Neno hili ‘toharani’ halimo katika Biblia, wala fundisho la toharani halifundishwi waziwazi katika Biblia. . . . Vitabu vya Mababa vina marejeo mengi si kuhusu kuwako kwa toharani tu, bali pia uhakika wa kwamba waamini waliokufa wanaweza kusaidiwa kwa sala za walio hai, hasa kwa Dhabihu ya Misa.”—Uku. 347, 348.
Kuhusu hali ya wafu, Maandiko Matakatifu yanasema: “Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote.” (Mhu. 9:5, UV) “Nafsi [“roho,” UV; “yeyote,” BHN] inayofanya zambi, itakufa.” (Eze. 18:4, ZSB) (Ona pia ukurasa wa 102-104, chini ya kichwa “Kifo.”)
-
-
Mpinga-KristoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Mpinga-Kristo
Maana: Neno mpinga-Kristo lamaanisha kuwa dhidi au badala ya Kristo. Neno hilo linahusu wote wanaokana yale ambayo Biblia inasema kumhusu Yesu Kristo, wote wanaoupinga Ufalme wake, na wote wanaowatesa wafuasi wake. Pia linatia ndani watu mmoja mmoja, mashirika, na mataifa ambayo kwa uwongo yanadai kumwakilisha Kristo au yanayojihesabia isivyofaa cheo cha Masihi.
Je, Biblia inasema kwamba kuna mpinga-Kristo mmoja tu?
1 Yoh. 2:18: “Watoto wachanga, ni saa ya mwisho, na, kama vile ambavyo mmesikia kwamba mpinga-Kristo anakuja, hata sasa kumekuwa na wapinga-Kristo wengi; uhakika ambao kutokana nao tunajua kwamba ni saa ya mwisho.”
2 Yoh. 7: “Wadanganyifu wengi wametokea katika ulimwengu, watu ambao hawamkiri Yesu Kristo kuwa alikuja katika mwili. Hao ndio yule mdanganyifu na mpinga-Kristo.” (Ona kwamba “wapinga-Kristo wengi” katika 1 Yohana 2:18 wanatajwa hapa kwa ujumla kuwa ndiye “mpinga-Kristo.”)
Je, mpinga-Kristo atakuja wakati fulani ujao?
1 Yoh. 4:3: “Kila neno lililoongozwa na roho ambalo halimkiri Yesu halitokani na Mungu. Zaidi ya hayo, ambalo mmesikia kwamba linakuja, na sasa tayari limo ulimwenguni.” (Maneno hayo yaliandikwa karibu na mwisho wa karne ya kwanza W.K.)
-