Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ubatizo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • ‘Ubatizo kwa ajili ya wafu’—unamaanisha nini?

      1 Kor. 15:29, UV: “Au je! Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu watafanyaje? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, kwa nini kubatizwa kwa ajili yao?”

      Neno la Kigiriki hy·perʹ, linalotafsiriwa hapa “kwa ajili ya,” pia humaanisha “juu ya,” “kwa niaba ya,” “badala ya,” “kwa kusudi la,” n.k. (A Greek-English Lexicon, iliyoandikwa na Liddell na Scott) Neno hilo linamaanisha nini katika andiko hilo? Je, Paulo alikuwa akipendekeza watu walio hai wabatizwe kwa ajili ya wale waliokuwa wamekufa bila kubatizwa?

      Yale maandiko mengine yanayotaja kifo kuhusiana na ubatizo moja kwa moja hurejelea ubatizo ambao mtu mwenyewe hubatizwa, wala si ubatizo kwa ajili ya mtu mwingine, aliyekufa

      Rom. 6:3: “Hamjui kwamba sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika kifo chake?” (Pia Marko 10:38, 39)

      Kol. 2:12: “Kwa maana [ninyi washiriki walio hai wa kutaniko la Kolosai] mlizikwa pamoja naye katika ubatizo wake, na kwa uhusiano pamoja naye mlifufuliwa pia pamoja kupitia imani yenu katika utendaji wa Mungu, aliyemfufua huyo kutoka kwa wafu.”

      Fasiri iliyo katika “Tafsiri ya Ulimwengu Mpya” ni sahihi kisarufi na inapatana na maandiko haya mengine ya Biblia

      1 Kor. 15:29: “Kama sivyo, watafanya nini wale wanaobatizwa kwa kusudi la kuwa wafu? Ikiwa wafu hawatafufuliwa kamwe, kwa nini pia wanabatizwa kwa kusudi la kuwa hivyo?” (Kwa hiyo, wanabatizwa, au wanazamishwa, katika mwendo wa maisha utakaoongoza kwenye kifo cha kushika utimilifu kama kile cha Kristo na kisha wafufuliwe kwenye uzima wa kiroho kama yeye.)

      Ni nini linalotokana na ubatizo wa moto?

      Luka 3:16, 17: “Yeye [Yesu Kristo] atawabatiza ninyi kwa . . . moto. Sepetu yake ya kupepetea imo mkononi mwake ili kuusafisha kabisa uwanja wake wa kupuria . . . Makapi atayateketeza kwa moto usioweza kuzimwa.” (Uharibifu wa makapi hayo utakuwa wa milele.)

      Mt. 13:49, 50: “Hivyo ndivyo itakavyokuwa katika umalizio wa mfumo wa mambo: malaika watatoka kwenda na kuwatenga waovu kutoka katikati ya waadilifu nao watawatupa ndani ya tanuru ya moto.”

      Luka 17:29, 30: “Siku ambayo Loti alitoka Sodoma kulinyesha moto na kiberiti kutoka mbinguni na kuwaangamiza wote. Itakuwa vivyo hivyo siku ile ambayo Mwana wa binadamu atafunuliwa.”

      Si sawa na ubatizo kwa roho takatifu, uliokuwa wa wanafunzi

      Mdo. 1:5: “Yohana, kwa kweli, alibatiza kwa maji, lakini ninyi [mitume waaminifu wa Yesu] mtabatizwa kwa roho takatifu siku chache baadaye.”

      Mdo. 2:2-4: “Ghafula kukatokea kutoka mbinguni kelele kama ile ya upepo wenye nguvu unaovuma, nao ukaijaza nyumba yote ambamo walikuwa wameketi. Nao wakaona ndimi kama za moto, nazo zikagawanyika huku na huku, na mmoja ukaketi juu ya [lakini haukumfunika au kumzamisha] kila mmoja wao, nao wote wakajazwa roho takatifu wakaanza kusema katika lugha tofauti, kama vile roho ilivyokuwa ikiwawezesha kusema.”

  • Ufalme
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Ufalme

      Maana: Ufalme wa Mungu huwakilisha enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu wote kuelekea viumbe wake, au njia anayoitumia kuonyesha enzi hiyo. Neno hili linatumiwa hasa kurejelea enzi kuu ya Mungu kupitia serikali inayoongozwa na Mwana wake, Yesu Kristo. Neno “ufalme” linaweza kurejelea utawala wa yule aliyetiwa mafuta awe Mfalme, au linaweza kurejelea dunia inayotawaliwa na serikali hiyo ya mbinguni.

      Je, Ufalme wa Mungu ni serikali halisi?

      Au ni hali iliyo katika mioyo ya wanadamu?

      Luka 17:21, UV: “Wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama ufalme wa Mungu umo ndani yenu [pia ZSB, NAJ; lakini “kati yenu,” BHN, VB; “katikati yenu,” NW].” (Ona kwamba, kama vile mstari wa 20 unavyoonyesha, Yesu alikuwa akizungumza na Mafarisayo, ambao pia aliwashutumu kuwa wanafiki, kwa hiyo, hangeweza kumaanisha kwamba Ufalme ulikuwa katika mioyo yao. Lakini Ufalme kama unavyowakilishwa na Kristo ulikuwa katikati yao.)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki