Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Urithi wa Upapa
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • 1 Tim. 3:2, UV: “Basi imempasa askofu awe . . . mume wa mke mmoja [“ameoa mara moja tu,” NAB].”

      Kabla ya enzi ya Ukristo, dini ya Ubudha iliwataka makasisi na watawa wake wa kiume wawe waseja. (History of Sacerdotal Celibacy in the Christian Church, London, 1932, chapa ya nne, iliyosahihishwa, Henry C. Lea, uku. 6) Hata mapema zaidi, makasisi wakuu wa Kibabiloni walitakiwa wawe waseja, kulingana na The Two Babylons cha A. Hislop.—(New York, 1943), uku. 219.

      1 Tim. 4:1-3, UV: “Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; . . . wakiwazuia watu wasioe.”

      Kujitenga na ulimwengu

      Papa Paulo wa Sita, alipokuwa akihutubia Umoja wa Mataifa katika mwaka wa 1965, alisema hivi: “Watu wa dunia wanageukia Umoja wa Mataifa kuwa tumaini la mwisho la upatano na amani; Tunatoa sifa yao ya heshima na ya tumaini, pamoja na Yetu wenyewe.”—The Pope’s Visit (New York, 1965), Time-Life Special Report, uku. 26.

      Yoh. 15:19, UV: “[Yesu Kristo akasema:] Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.”

      Yak. 4:4, UV: “Hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu?”

      Kutumia silaha za vita

      Mwanahistoria Mkatoliki E. I. Watkin aliandika hivi: “Ingawa ni vigumu kukubali, hatuwezi kukataa wala kupuuza uhakika wa kihistoria kwamba nyakati zote Maaskofu wameunga mkono vita vyote vinavyopiganwa na serikali ya nchi yao ili kuendeleza mafundisho ya uwongo au ushikamanifu usio wa kweli. Kwa hakika, sijui kisa chochote ambapo makasisi wa taifa walishutumu vikali vita vyovyote kuwa si vya haki . . . Hata nadharia rasmi iwe gani, kwa matendo, wakati wa vita Maaskofu wa Wakatoliki wamefuata kanuni ya kwamba ‘nchi yangu ni sawa sikuzote.’”—Morals and Missiles (London, 1959), kilichohaririwa na Charles S. Thompson, uku. 57, 58.

      Mt. 26:52, UV: “Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga.”

      1 Yoh. 3:10-12, BHN: “Asiyempenda ndugu yake, huyo si mtoto wa Mungu. Hiyo ndiyo tofauti iliyoko kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi. . . . Tunapaswa kupendana! Tusiwe kama Kaini ambaye, kwa kuongozwa na yule Mwovu, alimwua ndugu yake.”

      Kutokana na yaliyotangulia, je, kwa kweli wale wanaodai kuwa warithi wa mitume wamefundisha na kutenda yale ambayo Kristo na mitume wake walitenda?

  • Utatu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Utatu

      Maana: Fundisho kuu la dini za Jumuiya ya Wakristo. Kulingana na Imani ya Athanasia, kuna Watu watatu wa kimungu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu), inasemekana kwamba kila mmoja ni wa milele, kila mmoja ni mweza-yote, hakuna aliye mkubwa au mdogo kuliko mwingine, kila mmoja ni Mungu, na hata hivyo wote pamoja ni Mungu mmoja tu. Maelezo mengine kuhusu fundisho hilo hukazia kwamba hao “Watu” watatu si watu mbalimbali bali ni maumbo matatu ambayo Mungu hukaa ndani yake. Kwa hiyo Wana-Utatu fulani hukazia imani yao kwamba Yesu Kristo ni Mungu, au kwamba Yesu na Roho Mtakatifu ni Yehova. Hilo si fundisho la Biblia.

      Fundisho la Utatu lilitoka wapi?

      The New Encyclopædia Britannica husema: “Neno Utatu, wala fundisho la wazi kama hilo, halipatikani katika Agano Jipya, wala Yesu na wafuasi wake hawakukusudia kupinga ile Shema katika Agano la Kale: ‘Sikiliza, Ee Israeli; BWANA, Mungu wetu, BWANA, ndiye mmoja’ (Kum. 6:4). . . . Fundisho hilo lilisitawi hatua kwa hatua kwa muda wa karne kadhaa na kupitia mabishano mengi. . . . Kufikia mwisho wa karne ya 4 . . . fundisho la Utatu likawa jinsi lilivyo leo hii.”—(1976), Micropædia, Buku la 10, uku. 126.

      New Catholic Encyclopedia hueleza hivi: “Maneno ‘Mungu mmoja katika Watu watatu’ hayakuthibitishwa imara, nayo hayakuwa sehemu kamili ya maisha ya Wakristo na imani yao, kabla ya mwisho wa karne ya 4. Lakini ni maneno hayo hasa ambayo yalianza kuitwa kwanza fundisho la Utatu. Kati ya Mababa wa Kimitume, hakukuwa na jambo lolote linalokaribia hata kidogo mawazo au maoni hayo.”—(1967), Buku la 14, uku. 299.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki