Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uhuru
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Mwa. 3:1-5: “Basi nyoka [akitumiwa kuwa msemaji wa Shetani; Ona Ufunuo 12:9] . . . akaanza kumwambia mwanamke: ‘Je, ni kweli kwamba Mungu alisema msile matunda ya kila mti wa bustani?’ Mwanamke akamjibu na kumwambia nyoka: ‘Tunaweza kula matunda ya miti ya bustani. Lakini kuhusu kula matunda ya mti ulio katikati ya bustani, Mungu amesema, “Msiyale, wala msiyaguse ili msife.”’ Ndipo nyoka akamwambia mwanamke: ‘Hakika hamtakufa. Kwa maana Mungu anajua kwamba siku ileile mtakapokula matunda yake macho yenu yatafunguliwa, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.’”

      Ni roho gani inayomchochea mtu anapopuuza mapenzi ya Mungu ili atosheleze tamaa zake binafsi?

      Efe. 2:1-3: “Ninyi ndio ambao Mungu alifanya kuwa hai ingawa mlikuwa wafu katika makosa na dhambi zenu, ambazo wakati fulani mlitembea ndani yake kulingana na mfumo wa mambo wa ulimwengu huu [ambao Shetani ndiye mtawala wake], kulingana na mtawala wa mamlaka ya hewa, roho ambayo sasa hutenda katika wana wa kutotii. Ndiyo, wakati fulani sisi sote tulijiendesha katikati yao kupatana na tamaa za mwili wetu, tukifanya mambo yanayopendwa na mwili na fikira, nasi kiasili tulikuwa watoto wa ghadhabu sawa na wale wengine.”

      Ni mitazamo gani ya kutaka kuwa huru ambayo wale wanaodai kwamba wanamtumikia Mungu ni lazima waepuke?

      Met. 16:18: “Kiburi hutangulia kuanguka, na roho ya majivuno hutangulia kujikwaa.”

      Met. 5:12: “Nawe utalazimika kusema: ‘Nimechukia nidhamu kama nini nao moyo wangu umedharau karipio kama nini!’” (Mtazamo huo unaweza kumwongoza mtu katika matatizo mazito, kama muktadha unavyoonyesha.)

      Hes. 16:3: “Basi wakakutana dhidi ya Musa na Haruni [ambao Yehova alikuwa akiwatumia wakiwa waangalizi kati ya watu wake] na kuwaambia: ‘Imetosha, kwa sababu kusanyiko lote, wote hao ni watakatifu na Yehova yuko katikati yao. Kwa nini, basi, mjiinue wenyewe juu ya kutaniko la Yehova?’”

      Yuda 16: “Watu hawa ni wanung’unikaji, walalamikaji juu ya fungu lao maishani, wakiendelea kulingana na tamaa zao wenyewe, na vinywa vyao husema mambo ya kujigamba, huku wakisifu kwa kustaajabia watu mashuhuri kwa ajili ya faida yao wenyewe.”

      3 Yoh. 9: “Diotrefe, anayependa kuwa na mahali pa kwanza katikati yao, hapokei kwa heshima jambo lolote kutoka kwetu.”

      Met. 18:1: “Mtu anayejitenga na wengine atatafuta mapendezi yake mwenyewe; atashindana na hekima yote inayotumika.”

      Yak. 4:13-15: “Haya, basi, ninyi ambao husema: ‘Leo au kesho tutasafiri kwenda jiji fulani nasi tutakaa mwaka mmoja huko, tutafanya biashara na kupata faida,’ ingawa hamjui uzima wenu utakuwa namna gani kesho. Kwa maana ninyi ni ukungu unaotokea kwa muda kidogo na kisha kutoweka. Badala yake, mnapaswa kusema: ‘Yehova akipenda, tutaishi na pia kufanya hili au lile.’”

      Mtu huongozwa na nani wakati tamaa yake ya kuwa na uhuru inapomfanya aige mambo ya ulimwengu nje ya kutaniko la Kikristo? Na Mungu anaonaje jambo hilo?

      1 Yoh. 2:15; 5:19: “Msiwe mkiupenda ulimwengu au vitu vilivyo katika ulimwengu. Yeyote akiupenda ulimwengu, kumpenda Baba hakumo ndani yake.” “Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.”

      Yak. 4:4: “Yeyote anayetaka kuwa rafiki ya ulimwengu anajifanya kuwa adui ya Mungu.”

  • Ukumbusho (Mlo wa Jioni wa Bwana)
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Ukumbusho (Mlo wa Jioni wa Bwana)

      Maana: Mlo wa kukumbuka kifo cha Yesu Kristo; kwa hiyo, huo ni ukumbusho wa kifo chake, kifo ambacho kimekuwa na matokeo makubwa kuliko kile cha mtu mwingine yeyote. Hili ndilo tukio pekee ambalo Bwana Yesu Kristo aliwaamuru wanafunzi wake walifanyie ukumbusho. Pia unaitwa Mlo wa Jioni wa Bwana.—1 Kor. 11:20.

      Ukumbusho una umuhimu gani?

      Yesu aliwaambia hivi mitume wake waaminifu: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.” (Luka 22:19) Alipokuwa akiwaandikia washiriki wa kutaniko la Kikristo lililozaliwa kwa roho, mtume Paulo aliongeza hivi: “Kila mara mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mnaendelea kukitangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapofika.” (1 Wakorintho 11:26) Kwa hiyo, Ukumbusho unakazia kwa njia ya pekee umuhimu wa kifo cha Yesu Kristo katika kutimiza kusudi la Yehova. Unakazia maana ya kifo cha kidhabihu cha Yesu hasa kuhusiana na agano jipya na matokeo ya kifo chake kwa wale watakaokuwa warithi pamoja naye wa Ufalme wa mbinguni.—Yoh. 14:2, 3; Ebr. 9:15.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki