-
Dawa za KulevyaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kwanza, kwa kujifunza Biblia na kutafakari unahitaji kusitawisha tamaa yenye nguvu ya kumpendeza Mungu na kuishi katika mfumo wake mpya wa mambo wenye uadilifu. Ukimkaribia, atakukaribia, naye atakupa msaada unaohitaji.— Yak. 4:8.
Ni muhimu mtu asadiki ubaya wa mazoea hayo na kuyachukia kikweli. (Zab. 97:10) Jambo hilo linaweza kufanywa kwa kurudia mambo ya hakika yaliyoandikwa katika sehemu hii ya kitabu na kutafakari, si juu ya raha za muda za sasa ambazo huenda zikatokana na mazoea hayo, bali juu ya yale yanayompendeza Mungu na jinsi matokeo ya mazoea mabaya yanavyochukiza sana.
Ikiwa unatamani sana kuvuta sigara au kutumia moja kati ya zile dawa nyingine za kulevya, sali kwa Mungu kwa bidii ili akusaidie. (Luka 11:9, 13; linganisha na Wafilipi 4:13.) Fanya hivyo bila kukawia. Pia, chukua Biblia yako na uisome kwa sauti kubwa, au mwendee Mkristo aliyekomaa. Mwambie yanayokupata na umwombe msaada.
-
-
DhambiKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Dhambi
Maana: Kulingana na maandishi ya Biblia ya Kiebrania na Kigiriki, dhambi ni kukosa alama. Mungu mwenyewe huweka “alama” ambayo viumbe wake wenye akili wanapaswa kufikia. Kukosa kufikia alama hiyo ni dhambi, ambayo pia ni ukosefu wa uadilifu, au uasi-sheria. (Rom. 3:23; 1 Yoh. 5:17; 3:4) Dhambi ni chochote ambacho hakipatani na utu wa Mungu, viwango vyake, njia, na mapenzi yake, ambayo yote ni matakatifu. Huenda ikatia ndani mwenendo mbaya, mtu kushindwa kufanya anayopaswa kufanya, maneno mabaya, mawazo machafu, au tamaa au nia ambazo ni za ubinafsi. Biblia inatofautisha kati ya dhambi iliyorithiwa na dhambi ya kukusudiwa, kati ya tendo la dhambi ambalo mtu anatubia na zoea la kutenda dhambi.
Iliwezekanaje Adamu afanye dhambi ikiwa alikuwa mkamilifu?
Kuhusu habari ya Adamu kuwa mkamilifu, soma Mwanzo 1:27, 31 na Kumbukumbu la Torati 32:4. Yehova Mungu alipotangaza uumbaji wake wa duniani, kutia ndani mwanamume na mwanamke, kuwa kitu “chema sana,” alimaanisha nini? Ili Mungu, ambaye kazi yake ni kamilifu, aseme kwamba kile alichoumba kilikuwa “chema sana,” ni lazima kilifikia viwango vyake vikamilifu.
-