Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuteseka
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Mara nyingi wanadamu ndio hasa wanaopaswa kulaumiwa kwa sababu ya madhara yanayotokea. Kwa njia gani? Hata wanapopewa onyo la kutosha, watu wengi hukataa kutoka katika eneo la hatari au hukosa kuchukua tahadhari zinazohitajiwa.—Met. 22:3; linganisha na Mathayo 24:37-39.

      Mungu anaweza kuzuia nguvu hizo za asili. Alimwezesha Yesu Kristo kutuliza upepo mkubwa juu ya Bahari ya Galilaya, ili kuonyesha yale ambayo Yeye atawafanyia wanadamu chini ya Ufalme Wake wa Kimasihi. (Marko 4:37-41) Kwa kumkataa Mungu, Adamu alikataa msaada kutoka kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe na wazao wake. Wale watakaopewa uzima wakati wa Utawala wa Kristo wa Kimasihi watauona utunzaji huo wenye upendo ambao serikali iliyowekwa na Mungu peke yake ndiyo inayoweza kuutoa.—Isa. 11:9.

      Je, watu wanaopatwa na taabu wanaadhibiwa na Mungu kwa sababu ya kutenda maovu?

      Wale wanaovunja viwango vya Mungu vya maisha hupata matokeo mabaya. (Gal. 6:7) Nyakati nyingine wao huvuna upesi mavuno machungu. Katika visa vingine, huenda wakaonekana wanafanikiwa kwa muda mrefu. Tofauti na hilo, Yesu Kristo, ambaye hakufanya kosa kamwe, alitendewa kikatili na kuuawa. Kwa hiyo, katika ulimwengu huu, ufanisi haupasi kuonwa kuwa uthibitisho wa kwamba mtu ana baraka ya Mungu, wala taabu isifikiriwe kuwa uthibitisho wa kwamba mtu amekataliwa na Mungu.

      Ayubu alipopoteza mali zake naye akasumbuliwa na ugonjwa mbaya, hilo halikuwa kwa sababu ya kukataliwa na Mungu. Biblia inasema waziwazi kwamba Shetani ndiye aliyesababisha hayo. (Ayu. 2:3, 7, 8) Lakini rafiki waliokuja kumtembelea Ayubu walidai kuwa hali mbaya ya Ayubu ilithibitisha kwamba amefanya jambo ovu. (Ayu. 4:7-9; 15:6, 20-24) Yehova aliwakaripia, akisema: “Hasira yangu imewaka juu yako . . . kwa maana ninyi hamkusema mambo ya kweli kunihusu mimi kama mtumishi wangu Ayubu.”—Ayu. 42:7.

      Huenda waovu wakafanikiwa kwa muda fulani. Asafu aliandika hivi: “Niliwaonea wivu wenye kujisifu, nilipokuwa nikiiona amani ya watu waovu. Wala hawamo katika taabu ya mwanadamu anayeweza kufa, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine. Wao hudhihaki na kuzungumza juu ya yaliyo mabaya; wanazungumza juu ya upunjaji kwa majivuno. Tazama! Hao ndio waovu waliostarehe mpaka wakati usio na kipimo. Wameongeza mali yao.”—Zab. 73:3, 5, 8, 12.

      Siku ya Mungu ya kutoza hesabu itafika. Wakati huo atawaadhibu waovu, na kuwaharibu milele. Andiko la Methali 2:21, 22 linasema hivi: “Wanyoofu ndio watakaokaa duniani, na wasio na lawama ndio watakaobaki ndani yake. Nao waovu, watakatiliwa mbali kutoka duniani; nao wenye hila, watang’olewa kutoka ndani yake.” Hapo ndipo wanyoofu, ambao wengi wao wameteseka, watakapopata afya kamilifu na kufurahia mazao mengi ya dunia.

      Mtu Akisema—

      ‘Kwa nini Mungu anaruhusu kuteseka?’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Hilo ni jambo linalotuhangaisha sana sisi sote. Hebu nikuulize, Kwa nini umeuliza swali hilo leo?’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘(Tumia habari katika ukurasa wa 124-128.)’ (2) ‘(Tumia maandiko mengine yanayoonyesha kwamba hali fulani hususa ambayo imemfanya mtu huyo binafsi ateseke itaondolewa.)’

      Au unaweza kusema: (ikiwa wanahangaishwa na ukosefu wa haki ulimwenguni): ‘Biblia inaonyesha kwa nini hali hizi zipo leo. (Mhu. 4:1; 8:9) Je, unajua kwamba inaonyesha pia mambo ambayo Mungu atafanya ili atuletee kitulizo? (Zab. 72:12, 14; Dan. 2:44)’

      Pia unaweza kusema: ‘Inaonekana wewe unamwamini Mungu. Je, unaamini kwamba Mungu ni upendo? . . . Je, unaamini kwamba yeye ni mwenye hekima na kwamba yeye ni mweza-yote? . . . Basi ni lazima awe ana sababu fulani nzuri za kuruhusu kuteseka. Biblia inaonyesha sababu hizo. (Ona ukurasa wa 124-128.)’

  • Kutoa Mimba
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kutoa Mimba

      Maana: Kutoa mimba ni kuondoa tumboni kiini-tete au kitoto ambacho kwa kawaida hakiwezi kuishi nje ya tumbo la uzazi. Huenda mimba ikatoka yenyewe kwa sababu ya kutokamilika kwa kibinadamu au kwa sababu ya msiba. Kutoa mimba kimakusudi ili kuepuka tu kuzaa mtoto asiyetakiwa ni sawa na kumwua binadamu kimakusudi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki