-
UovuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Unaweza kujibu hivi: ‘Ninafurahi kusikia kwamba unamwamini Mungu. Ni kweli kwamba kuna uovu mwingi, nao ulianza zamani sana kabla ya wakati wetu. Lakini umepata kufikiria jambo hili . . . ? (Tumia mawazo yaliyo katika fungu la 1 katika ukurasa wa 352, kuhusu urefu wa wakati ambao Mungu amevumilia uovu.)’
Au unaweza kusema: ‘Bila shaka utakubaliana nami ninaposema kwamba yeyote aliye na uwezo wa kujenga nyumba hakika ana uwezo wa kuisafisha pia. . . . Kwa kuwa Mungu aliiumba dunia, halingekuwa jambo gumu kwake kuisafisha. Kwa nini amengojea muda mrefu sana? Niliona jibu hili linaridhisha sana. Niambie maoni yako. (Ndipo someni pamoja habari iliyo katika ukurasa wa 352-354.)’
-
-
UponyajiKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Uponyaji
Maana: Kumfanya mtu ambaye amekuwa mgonjwa kimwili, kiakili, au kiroho apate afya njema. Roho ya Mungu iliwawezesha baadhi ya manabii Waebrania waliokuwako kabla ya Ukristo na pia Yesu Kristo na washiriki fulani wa kutaniko la kwanza la Kikristo waponye kimuujiza.
Je, uponyaji wa kimuujiza leo unafanywa kupitia roho ya Mungu?
Je, uwezo wa kufanya miujiza unaweza kutoka chanzo kingine ambacho si Mungu wa kweli?
Musa na Haruni walienda mbele ya Farao wa Misri ili wamwombe awaruhusu Waisraeli waende nyikani kumtolea Yehova dhabihu. Kama uthibitisho wa kwamba anaungwa mkono na Mungu, Musa alimwelekeza Haruni atupe chini fimbo yake nayo ikawa nyoka mkubwa. Muujiza huo ulifanywa kwa nguvu za Mungu. Lakini makuhani wa Misri wenye kufanya uchawi nao wakazitupa chini fimbo zao nazo pia zikawa nyoka wakubwa. (Kut. 7:8-12) Walifanya muujiza wao kwa uwezo wa nani?—Linganisha na Kumbukumbu la Torati 18:10-12.
Katika karne ya 20 uponyaji fulani wa imani unafanywa katika ibada zinazoongozwa na makasisi wa Jumuiya ya Wakristo. Kati ya dini zisizo za Kikristo kuna makuhani wa uchawi, walozi, waganga, na wengine wanaoponya pia; mara nyingi wanatumia uchawi na uaguzi. Watu fulani ambao huponya kwa kuchunguza akili husema kwamba uponyaji wao hauna uhusiano na dini. Katika visa hivyo vyote, je, uwezo huo wa kuponya unatoka kwa Mungu wa kweli?
Mt. 24:24: “Makristo wa uwongo na manabii wa uwongo watatokea na kutoa ishara kubwa na maajabu [“miujiza,” NAJ] ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale waliochaguliwa.”
Mt. 7:15-23: “Jihadharini na manabii wa uwongo . . . Wengi wataniambia siku hiyo, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii katika jina lako, na kufukuza roho waovu katika jina lako, na kufanya matendo mengi yenye nguvu [“miujiza,” UV, BHN, VB] katika jina lako?’ Na hata hivyo nitawaambia waziwazi: Sikuwajua ninyi kamwe! Ondokeni kwangu, ninyi wenye matendo ya uasi-sheria.”
Je, maponyo ya leo yenye kusisimua yanafanywa kwa njia ileile kama maponyo ya kimuujiza yaliyofanywa na Yesu na wanafunzi wake wa kwanza?
Malipo: “Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, fukuzeni roho waovu. Mlipokea bure, toeni bure.” (Mt. 10:8) (Je, waponyaji leo wanafanya hivyo—wanatoa bure, kama Yesu alivyoamuru?)
Kiwango cha mafanikio: “Umati wote ulikuwa ukitafuta kumgusa, kwa sababu nguvu zilikuwa zikimtoka na kuwaponya wote.” (Luka 6:19) “Wakawaleta wagonjwa nje hata katika zile njia pana na kuwalaza huko juu ya vitanda na machela, ili, wakati Petro anapopita hapo, angalau kivuli chake kipate kumwangukia mtu fulani kati yao. Pia, umati kutoka kwenye majiji yanayozunguka Yerusalemu ukazidi kuja pamoja, ukiwa umewabeba wagonjwa na wale wenye kutaabika wakiwa na roho wachafu, nao wote wakawa wakiponywa.” (Mdo. 5:15, 16) (Katika siku zetu, je, wote wanaowaendea waponyaji wa kidini au wanaoenda kwenye mahekalu ya kidini wakitafuta kuponywa, huponywa?)
Je, maisha ya wafuasi wa mashirika ambayo “waponyaji” wanashirikiana nayo yanaonyesha kwamba wana roho ya Mungu?
Wakiwa kikundi, je, wanaonyesha waziwazi matunda ya roho kama vile upendo, ustahimilivu, upole, kujizuia?—Gal. 5:22, 23.
Je, kwa kweli wao “si sehemu ya ulimwengu,” wakiepuka kujiingiza katika siasa zote za ulimwengu? Je, wamejiepusha kabisa na hatia ya damu wakati wa vita? Je, wana sifa nzuri kwa sababu ya kuepuka mwenendo usio wa adili wa ulimwengu?—Yoh. 17:16; Isa. 2:4; 1 The. 4:3-8.
Je, leo Wakristo wa kweli wanatambuliwa kwa uwezo wa kuponya kimuujiza?
Yoh. 13:35: “Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mkiwa na upendo kati yenu wenyewe.” (Hivyo ndivyo Yesu alivyosema. Ikiwa tunamwamini kweli kweli, tutatafuta kuona upendo, wala si uponyaji wa kimuujiza, kuwa uthibitisho wa Ukristo wa kweli.)
Mdo. 1:8: “Mtapokea nguvu wakati roho takatifu itakapofika juu yenu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu . . . mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Muda mfupi tu kabla ya kuwaacha mitume wake na kurudi mbinguni, Yesu aliwaambia kwamba hiyo ilikuwa ndiyo kazi ya maana sana ambayo walipaswa waifanye, wala si kufanya uponyaji. Ona pia Mathayo 24:14; 28:19, 20.)
1 Kor. 12:28-30: “Mungu amewaweka watu mbalimbali katika kutaniko, kwanza, mitume; pili, manabii; tatu, walimu, kisha matendo yenye nguvu; kisha zawadi za maponyo; utumishi wenye msaada, uwezo wa kuelekeza, lugha tofauti. Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote hufanya matendo yenye nguvu? Je, wote wana zawadi za maponyo?” (Biblia inaonyesha waziwazi kwamba si Wakristo wote wa kweli ambao wangekuwa na zawadi za maponyo.)
Je, andiko la Marko 16:17, 18 halionyeshi kwamba uwezo wa kuponya wagonjwa ungekuwa ishara ya kutambulisha waamini?
Marko 16:17, 18, UV: “Ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.”
-