Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Dini
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Unaweza kujibu hivi: ‘Nashukuru kwa kuniambia hivyo. Nina hakika utakubali kwamba jambo muhimu kwelikweli kwetu sote ni kupata kibali cha Mungu, sivyo?’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Mungu anatupa sote jambo zito la kufikiria hapa katika andiko la Ufunuo 18:4, 5. . . . Hata ikiwa sisi binafsi hatutendi mambo mabaya, Biblia inaonyesha kwamba tuna lawama ikiwa tunaunga mkono dini hizo. (Ona pia kichwa “Babiloni Mkubwa.”)’ (2) (Unaweza pia kutumia habari kwenye ukurasa wa 65, 66.) (3) ‘Mungu anawatafuta watu wanaoipenda kweli, naye anawakusanya pamoja ili wamwabudu kwa umoja. (Yoh. 4:23, 24)’

      ‘Dini zote ni nzuri; wewe una yako, nami nina yangu’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Inaonekana unaheshimu mawazo ya wengine. Lakini unatambua pia kwamba sote tunahitaji mwongozo ambao Neno la Mungu linatoa, na ndiyo sababu una dini, sivyo?’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Hapa katika andiko la Mathayo 7:13, 14 Biblia inatupa mwongozo muhimu sana katika maneno ya Yesu. (Soma.) . . . Kwa nini huenda ikawa hivyo?’

      Ona pia ukurasa wa 59, 60.

      ‘Maadamu unamwamini Yesu, haidhuru unashirikiana na kanisa gani’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Bila shaka, ni muhimu kumwamini Yesu. Nadhani unamaanisha kwamba unakubali kila jambo alilofundisha. Bila shaka wewe umeona, kama mimi, kwamba wengi wanaosema ni Wakristo kwa kweli hawaishi maisha ya Kikristo.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Ona jambo ambalo Yesu alisema katika Mathayo 7:21-23.’ (2) ‘Kuna wakati ujao ulio mzuri ajabu kwa wale wanaotaka kujua mapenzi ya Mungu kisha kuyafanya. (Zab. 37:10, 11; Ufu. 21:4)’

      ‘Kwa nini unafikiri kwamba kuna dini moja tu ya kweli?’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Bila shaka, kuna watu wanyoofu katika karibu kila dini. Lakini jambo la maana kwelikweli ni lile ambalo Neno la Mungu linasema. Linasema kuna dini ngapi za kweli? Ona yaliyoandikwa hapa katika Waefeso 4:4, 5.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Hilo linapatana na maandiko mengine. (Mt. 7:13, 14, 21; Yoh. 10:16; 17:20, 21)’ (2) ‘Basi, tatizo tulilo nalo ni kuitambua dini hiyo. Tunaweza kuitambuaje? (Unaweza kutumia habari katika ukurasa wa 65, 66.)’ (3) (Ona pia habari katika ukurasa wa 188, 189, chini ya kichwa, “Mashahidi wa Yehova.”)

      ‘Mimi husoma tu Biblia nyumbani na kusali kwa Mungu nipate kuielewa’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Je, umefaulu kuisoma Biblia nzima?’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Unapojitahidi kufanya hivyo, utaona jambo lenye kupendeza sana katika Mathayo 28:19, 20. . . . Jambo hilo ni muhimu kwa sababu linaonyesha kwamba Kristo anawatumia wanadamu wengine watusaidie kuelewa yanayohusika katika kuwa Mkristo wa kweli. Kupatana na hilo, Mashahidi wa Yehova wanajitolea kuwatembelea watu katika nyumba zao kwa muda wa saa moja hivi kila juma, bila malipo, ili kuzungumzia Biblia. Je, ninaweza kutumia dakika chache tu nikuonyeshe jinsi tunavyofanya?’

      Ona pia ukurasa wa 64.

      ‘Mimi naamini kwamba dini ni jambo la kibinafsi’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Siku hizi watu wengi wana maoni hayo, na ikiwa watu hawapendezwi kikweli na ujumbe wa Biblia, sisi huwaacha na kwenda katika nyumba nyingine. Lakini je, unajua kwamba nimekuja kukuona kwa sababu Yesu aliwaagiza wafuasi wake wafanye hivyo? . . . (Mt. 24:14; 28:19, 20; 10:40)’

  • Dunia
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Dunia

      Maana: Katika Maandiko, neno “dunia” linatumiwa katika maana zaidi ya moja. Kwa kawaida tunalifikiria kuwa linamaanisha sayari yenyewe, ambayo Yehova aliiumba ikiwa na vitu vya kuendeleza uhai wa binadamu kwa kusudi la kufanya maisha yetu yaridhishe sana. Hata hivyo, tunapaswa kufahamu kwamba neno “dunia” huenda likatumiwa pia kumaanisha, kwa mfano, watu wanaoishi duniani au kikundi cha watu wenye tabia fulani.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki