Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Vipindi vya Wakati
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Mapema Oktoba, 607 K.W.K., hadi Desemba 31, 607 K.W.K. = mwaka 1⁄4

      Januari 1, 606 K.W.K., hadi Desemba 31, 1 K.W.K. = miaka 606

  • Wanawake
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Wanawake

      Maana: Wanadamu wa jinsia ya kike ambao ni watu wazima. Katika Kiebrania, neno mwanamke ni ’ish·shahʹ, ambalo kihalisi humaanisha “mwanadamu wa kike.”

      Je, Biblia inawashushia wanawake heshima au inawatendea kana kwamba ni watu duni?

      Mwa. 2:18: “Yehova Mungu akaendelea kusema: ‘Si vema huyo mwanamume aendelee kuwa peke yake. Nitamfanyia msaidizi, awe kikamilisho chake.’” (Katika andiko hilo, Mungu hasemi kwamba mwanamume ni mtu bora kuliko mwanamke. Badala yake, Mungu alionyesha kwamba mwanamke angekuwa na sifa ambazo zingekamilisha zile za mwanamume katika mpango wa Mungu. Kikamilisho ni kimoja cha vitu viwili vinavyokamilishana. Basi wanawake kwa ujumla hutokeza katika sifa na uwezo fulani; wanaume nao hutokeza katika sifa nyingine. Linganisha na 1 Wakorintho 11:11, 12.)

      Mwa. 3:16: “[Mungu] akamwambia mwanamke: ‘ . . . tamaa yako itakuwa kwa mume wako, naye atakutawala.’” (Tangazo hilo lililotolewa baada ya Adamu na Hawa kufanya dhambi halikumaanisha jambo ambalo wanaume wanapaswa kufanya bali lilimaanisha jambo ambalo Yehova alijua mapema kwamba wanaume wangefanya kwa kuwa sasa ubinafsi ulikuwa umeingia katika maisha ya wanadamu. Masimulizi kadhaa ya Biblia yaliyoandikwa baada ya tukio hilo husema kuhusu hali zenye huzuni sana zilizositawi kwa sababu ya wanaume kuwatawala wanawake kwa ubinafsi. Lakini Biblia haisemi kwamba Mungu alikubali mwenendo huo wala haisemi kwamba huo ni mfano wa kufuatwa na wengine.)

      Je, kuwapa wanaume ukichwa ni kuwashushia heshima wanawake?

      Kuwa chini ya ukichwa kwenyewe si kushushiwa heshima. Ukichwa hufanya mambo yaendeshwe kwa utaratibu, na Yehova ‘si Mungu wa machafuko, bali ni wa amani.’ (1 Kor. 14:33) Yesu Kristo yuko chini ya ukichwa wa Yehova Mungu, naye huridhika sana na uhusiano huo.—Yoh. 5:19, 20; 8:29; 1 Kor. 15:27, 28.

      Mwanamume pia amepewa ukichwa wa kiasi, hasa katika familia na katika kutaniko la Kikristo. Mungu hajampa mwanamume mamlaka kamili juu ya mwanamke; mwanamume lazima atoe hesabu kwa kichwa chake, Yesu Kristo, na kwa Mungu kuhusu jinsi anavyotumia ukichwa huo. (1 Kor. 11:3) Zaidi ya hayo, waume wanaamuriwa ‘wawe wakiwapenda wake zao kama miili yao wenyewe’ na ‘kuwapa heshima’ wake zao. (Efe. 5:28; 1 Pet. 3:7) Mahitaji ya kingono ya mume hayawekwi juu ya yale ya mke wake katika mpango wa Mungu kwa watu waliooana. (1 Kor. 7:3, 4) Wajibu wa mke mwenye uwezo, kama ulivyoandikwa katika Biblia, hukazia ubora wake katika familia na jumuiya. Wajibu huo unampa nafasi tele ambapo anaweza kutumia uwezo wake huku akithamini ukichwa wa mume wake. (Met. 31:10-31) Biblia inawaamuru watoto wamheshimu baba yao na pia mama yao. (Efe. 6:1-3) Hiyo pia hutoa uangalifu wa pekee kuhusu kutunza mahitaji ya wajane. (Yak. 1:27) Kwa hiyo, kati ya Wakristo wa kweli, wanawake wanaweza kupata usalama mkubwa, wajithamini kwelikweli, na kuridhika na utendaji wao wenyewe.

      Heshima ya cheo cha mwanamke katika mpango wa Mungu inaonyeshwa zaidi na uhakika wa kwamba Yehova analitaja tengenezo lake mwenyewe la viumbe wa roho washikamanifu kama mwanamke, mke wake, mama ya watoto wake. (Ufu. 12:1; Gal. 4:26) Pia, kutaniko la Yesu Kristo la watiwa-mafuta linasemwa kuwa bibi-arusi wake. (Ufu. 19:7; 21:2, 9) Na kwa maoni ya kiroho hakuna tofauti kati ya mwanamume na mwanamke kati ya wale walioitwa katika Ufalme wa mbinguni pamoja na Kristo.—Gal. 3:26-28.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki