-
WokovuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Unaweza kujibu hivi: (1) ‘Ndiyo, kufikia wakati huu. Ninasema hivyo kwa sababu ninajua shauri la Biblia linalosema kwamba tusiwe na uhakika kupita kiasi. Je, unalijua andiko hili? (1 Kor. 10:12)’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Kwa nini hivyo? Mtume Paulo aliwaandikia watu waliokuwa wamezaliwa mara ya pili na waliokuwa na tumaini la kuishi mbinguni (Ebr. 3:1), akisema hivi . . . (Ebr. 3:12-14) Tunaimarisha imani yetu tunapoendelea kulijua Neno la Mungu.’
Au unaweza kusema: ‘Ninaweza kujibu swali hilo kwa kusema tu, Ndiyo. Lakini unajua kwamba Biblia inasema kuhusu wokovu zaidi ya mmoja? Kwa mfano, je, umewahi kufikiria maana ya andiko la Ufunuo 7:9, 10, 14? . . . Kwa hiyo, kuna watu watakaookolewa katika dhiki kuu inayokuja, na waishi hapa duniani. (Mt. 5:5)’
‘Je, unamkubali Yesu kuwa Mwokozi wako?’
Ona ukurasa wa 438, chini ya kichwa “Yesu Kristo.”
‘Ninyi mnasema kwamba ni 144,000 tu ndio watakaookolewa’
Unaweza kujibu hivi: ‘Ninafurahi kwa vile umetaja jambo hilo ili nikuambie jambo ambalo sisi tunaamini hasa. Watu wowote watakaokuwa na imani ya kweli katika uandalizi ambao Mungu amefanya kupitia Yesu watapata wokovu. Lakini Biblia inasema kwamba ni 144,000 tu ambao wataenda mbinguni wakawe pamoja na Kristo. Je, umewahi kuona jambo hilo katika Biblia? . . . Linapatikana hapa katika Ufunuo 14:1, 3.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Watafanya nini mbinguni? (Ufu. 20:6)’ (2) ‘Ni wazi kwamba watatawala juu ya mtu fulani. Huyo atakuwa nani? . . . (Mt. 5:5; 6:10)’
-
-
YehovaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Yehova
Maana: Jina la Mungu wa pekee wa kweli. Jina alilojipatia yeye mwenyewe. Yehova ndiye Muumba na, kwa haki, ndiye Mtawala Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu mzima. “Yehova” hutafsiriwa kutoka Herufi Nne za Kiebrania, יהוה, ambazo humaanisha “Yeye Husababisha Kuwa.” Katika lugha nyingi, herufi hizo nne za Kiebrania huwakilishwa na herufi JHVH au YHWH.
-