Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Dhambi
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Rom. 5:8, 10: “Tulipokuwa tungali watenda-dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu. . . . Tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kupitia kifo cha Mwana wake.” (Ona kwamba watenda-dhambi wanaitwa adui za Mungu. Basi, ni jambo la hekima kama nini kujifaidi wenyewe na uandalizi ambao Mungu amefanya ili tupatanishwe naye!)

      1 Tim. 1:13: “Nilionyeshwa rehema [asema mtume Paulo], kwa sababu nilikosa ujuzi nami nilitenda kwa ukosefu wa imani.” (Lakini Bwana alipomwonyesha njia iliyo sawa, hakukataa kuifuata.)

      2 Kor. 6:1, 2: “Tukifanya kazi pamoja naye, tunawasihi ninyi pia msipokee fadhili zisizostahiliwa za Mungu kisha mkose kusudi lake. Kwa maana anasema: ‘Katika wakati unaokubalika nilikusikia, na katika siku ya wokovu nilikusaidia.’ Tazama! Sasa ndio wakati unaokubalika hasa. Tazama! Sasa ndiyo siku ya wokovu.” (Sasa ndio wakati ambapo nafasi ya wokovu inapatikana. Mungu hatawaonyesha milele wanadamu wenye dhambi fadhili hizo zisizostahiliwa. Kwa hiyo, tunapaswa kuwa waangalifu ili tusikose kusudi la fadhili hizo.)

      Dhambi inaweza kuondolewaje?

      Ona kichwa, “Fidia.”

  • Dini
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Dini

      Maana: Namna ya ibada. Inatia ndani maoni ya kidini, imani, na mazoea; hayo huenda yakawa ya kibinafsi, au yakaungwa mkono na tengenezo fulani. Kwa kawaida dini inatia ndani imani katika Mungu au katika miungu kadhaa; au huona wanadamu, vitu, tamaa, au nguvu fulani kuwa vitu vya kuabudiwa. Dini nyingi zinategemea uchunguzi wa wanadamu juu ya mambo ya asili; pia kuna dini iliyofunuliwa. Kuna dini ya kweli na ya uwongo.

      Kwa nini kuna dini nyingi sana?

      Kadirio lililofanywa karibuni lilionyesha kwamba kuna dini kubwa 10 na madhehebu 10,000. Kati ya hizo, 6,000 ziko Afrika, 1,200 ziko Marekani, na mamia katika nchi nyingine.

      Mambo mengi yamesababisha kuongezeka kwa vikundi vipya vya kidini. Wengine wamesema kwamba dini hizo zote ni njia mbalimbali za kutoa kweli ya kidini. Lakini unapolinganisha mafundisho na mazoea yake pamoja na Biblia utaona kwamba kuna dini nyingi kwa sababu watu wanawafuata wanadamu badala ya kumsikiliza Mungu. Inafaa kuangaliwa kwamba, kwa kadiri kubwa, mafundisho ambayo wote wanashikilia, lakini yanayotofautiana na Biblia, yalianzia Babiloni la kale. (Ona ukurasa wa 28-30, chini ya kichwa “Babiloni Mkubwa.”)

      Ni nani aliyeanzisha mvurugo huo wa kidini? Biblia inamtambulisha Shetani Ibilisi kuwa “mungu wa mfumo huu wa mambo.” (2 Kor. 4:4) Inatuonya kwamba “vitu ambavyo mataifa huvitoa dhabihu wao huvitoa dhabihu kwa roho waovu, na si kwa Mungu.” (1 Kor. 10:20) Basi ni jambo muhimu kama nini kuhakikisha kwamba tunamwabudu Mungu wa kweli, yule Muumba wa dunia na mbingu, na kwamba ibada yetu inampendeza!

      Je, dini zote zinakubalika kwa Mungu?

      Amu. 10:6, 7: “Wana wa Israeli wakaanza tena kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, nao wakaanza kutumikia Mabaali na sanamu za Ashtorethi na miungu ya Siria na miungu ya Sidoni na miungu ya Moabu na miungu ya wana wa Amoni na miungu ya Wafilisti. Basi wakamwacha Yehova wala hawakumtumikia yeye. Hivyo hasira ya Yehova ikawaka juu ya Israeli.” (Ikiwa mtu anaabudu kitu chochote au mtu yeyote badala ya Mungu wa kweli, Muumba wa mbingu na dunia, ni wazi kwamba ibada yake haikubaliki kwa Yehova.)

      Marko 7:6, 7: “[Yesu] akawaambia [Mafarisayo na waandishi Wayahudi]: ‘Isaya kwa kufaa alitoa unabii juu yenu wanafiki, kama ilivyoandikwa, “Watu hawa huniheshimu mimi kwa midomo yao, bali mioyo yao iko mbali nami. Wao huniabudu bure, kwa sababu wao hufundisha amri za wanadamu kuwa mafundisho.”’” (Hata kikundi fulani kikidai kwamba kinamwabudu Mungu, ikiwa kinashikilia mafundisho ya wanadamu badala ya Neno la Mungu lililoongozwa na roho, ibada yake ni bure.)

      Rom. 10:2, 3: “Nawatolea ushahidi kwamba wana bidii kwa ajili ya Mungu; lakini si kulingana na ujuzi sahihi; kwa maana, kwa sababu ya kukosa kujua uadilifu wa Mungu bali wakitafuta kujiwekea uadilifu wao wenyewe, hawakujitiisha kwa uadilifu wa Mungu.” (Huenda watu wakawa na Neno la Mungu lililoandikwa lakini wakakosa ujuzi sahihi wa mambo yaliyomo, kwa sababu hawakufundishwa sawasawa. Huenda wakaona kwamba wana bidii kwa ajili ya Mungu, lakini huenda hawafanyi yale anayotaka. Je, ibada yao itampendeza Mungu?)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki