Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rr uku. 120
  • Msaada wa Kusimama Tena

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msaada wa Kusimama Tena
  • Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Habari Zinazolingana
  • “Mtakuwa Hai”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Jinsi Yehova Anavyotusaidia Kutimiza Huduma Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • “Waeleze . . . Kuhusu Hekalu”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Kitabu Cha Biblia Namba 28—Ezekieli
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
rr uku. 120
Ndugu mwenye umri mkubwa akitafakari mambo aliyotoka kusoma katika kitabu cha Ezekieli.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 10C

Msaada wa Kusimama Tena

TUNAWEZA kuimarishwa kwa kutafakari somo tunalopata kutokana na maono haya yenye kustaajabisha yaliyoandikwa kwenye Ezekieli 37:1-14, somo ambalo tunaweza kulitumia maishani. Ni somo gani?

Nyakati nyingine, huenda tukalemewa na mikazo na majaribu maishani hivi kwamba tukachoka na kushindwa kusonga mbele. Hata hivyo, nyakati kama hizo, tunaweza kuimarishwa tukitafakari maelezo yaliyo wazi ya maono ya Ezekieli kuhusu kurudishwa. Kwa nini? Tunajifunza kutokana na unabii huo kwamba Mungu anayeweza kupuliza uhai ndani ya mifupa iliyokufa kwa kweli anaweza kutupatia nguvu tunazohitaji ili kushinda vikwazo—hata vikwazo ambavyo kwa maoni ya kibinadamu hatuwezi kuvishinda.—Soma Zaburi 18:29; Flp. 4:13.

Huenda tukakumbuka kwamba karne nyingi kabla ya siku za Ezekieli, nabii Musa alisema kwamba Yehova ana nguvu na pia anatamani kutumia nguvu zake kwa ajili ya watu wake. Musa aliandika hivi: “Mungu ni kimbilio tangu nyakati za kale, mikono yake ya milele iko chini yako.” (Kum. 33:27) Naam, tunaweza kuwa na uhakika kwamba tukimtegemea Mungu nyakati za taabu, Yehova ataweka mikono yake yenye upendo chini yetu, atatuinua kwa wororo, na kutusaidia kusimama tena.—Eze. 37:10.

Ndugu mwenye umri mkubwa akitafakari mambo aliyotoka kusoma katika kitabu cha Ezekieli.

Angalia sura ya 10, fungu la 15, 16

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki