Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lff somo la 24
  • Malaika Ni Nani na Wanafanya Kazi Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Malaika Ni Nani na Wanafanya Kazi Gani?
  • Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Ukweli Kuhusu Malaika
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Viumbe wa Roho Wanahusikaje Katika Maisha Yetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Yesu Ana Nguvu Kuliko Roho Waovu
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
lff somo la 24
Somo la 24. Sanamu ya malaika.

SOMO LA 24

Malaika Ni Nani na Wanafanya Kazi Gani?

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Yehova anataka tujifunze kuhusu familia yake iliyo mbinguni. Familia hiyo inatia ndani malaika ambao wanaitwa “wana . . . wa Mungu.” (Ayubu 38:7) Biblia inasema nini kuhusu malaika? Je, wanaweza kuwasaidia au kuwadhuru watu? Je, malaika wote ni sehemu ya familia ya Mungu?

1. Malaika ni nani?

Yehova aliwaumba malaika kabla ya kuumba dunia. Malaika wanaishi mbinguni na hatuwezi kuwaona kama tu ambavyo hatuwezi kumwona Yehova. (Waebrania 1:14) Kuna mamilioni ya malaika na kila mmoja wao ana utu wa pekee. (Ufunuo 5:11) Malaika ‘wanatekeleza neno la Yehova, wakitii sauti yake.’ (Zaburi 103:20) Nyakati za kale, Yehova aliwatuma malaika wapeleke ujumbe au kuwasaidia na kuwaokoa watu wake. Leo, malaika wanawaongoza Wakristo kwa watu wanaotaka kujifunza kumhusu Mungu.

2. Shetani na roho wake waovu ni nani?

Baadhi ya malaika hawakuendelea kuwa waaminifu kwa Yehova. Malaika wa kwanza aliyeasi ni yule “anayeitwa Ibilisi na Shetani, anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa.” (Ufunuo 12:9) Shetani alitamani kuwatawala viumbe wengine, basi aliwashawishi wanadamu wa kwanza wamwasi Yehova na baadaye aliwashawishi malaika wengine wajiunge naye katika uasi. Malaika hao waasi wanaitwa roho waovu. Yehova aliamua wafukuzwe kutoka mbinguni waje duniani, nao wataangamizwa.​—Soma Ufunuo 12:9, 12.

3. Shetani na roho wake waovu wanatumia mbinu gani kuwapotosha wanadamu?

Shetani na roho waovu huwapotosha watu wengi kupitia zoea baya la kujaribu kuwasiliana na viumbe wa roho. Kwa mfano, baadhi ya watu hutafuta habari kutoka kwa wanajimu, wabashiri, na waganga wa kienyeji. Na wengine hutafuta matibabu yanayohusisha roho waovu. Pia, watu hudanganywa waamini kwamba wanaweza kuzungumza na watu waliokufa. Lakini Yehova anatuonya hivi: “Msiende kwa watu wanaowasiliana na roho, wala msitafute ushauri kutoka kwa wabashiri.” (Mambo ya Walawi 19:31) Anatupatia onyo hilo ili kutulinda dhidi ya Shetani na roho waovu. Wao ni maadui wa Mungu na wanataka kutusababishia madhara.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze kuhusu mambo mazuri ambayo malaika wanafanya, hatari za kuwasiliana na roho waovu, na jinsi tunavyoweza kujilinda dhidi ya Shetani na roho waovu.

Malaika akiwaongoza Mashahidi wawili wa Yehova wanapohubiri nyumba kwa nyumba.

4. Malaika huwasaidia watu wajifunze kumhusu Yehova

Malaika wa Mungu hawahubirii watu moja kwa moja. Badala yake, wanaweza kuwaongoza watu wa Mungu wawahubirie watu wanaotaka kujifunza kumhusu. Soma Ufunuo 14:6, 7, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Kwa nini tunahitaji msaada wa malaika tunapohubiri?

  • Je, unatiwa moyo kujua kwamba malaika wanaweza kukuongoza uwahubirie watu wanaohitaji kusikia ujumbe wa Biblia? Kwa nini?

Vifaa mbalimbali vinavyohusiana na ulozi na kuwasiliana na roho waovu, kutia ndani ubao unaotumiwa kusoma habari, mpira wa kioo, kitabu kuhusu mizimu, kadi za kubashiri, wanasesere wa kichawi, ubani, hirizi za kujilinda.

5. Epuka kuwasiliana na roho waovu

Shetani na roho waovu ni maadui wa Yehova. Wao ni adui zetu pia. Soma Luka 9:38-42, kisha mzungumzie swali hili:

  • Roho waovu wanawatendeaje wanadamu?

Hatungependa kujihusisha kwa vyovyote na roho waovu. Soma Kumbukumbu la Torati 18:10-12, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Roho waovu wanatumia njia gani kujaribu kutushawishi na kuwasiliana nasi? Katika eneo unaloishi, watu hutumia njia gani kuwasiliana na roho waovu?

  • Yehova anatuagiza tuepuke kabisa mazoea ya kuwasiliana na roho waovu. Je, unafikiri jambo hilo linafaa? Kwa nini?

Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

VIDEO: “Mpingeni Ibilisi” (5:02)

  • Je, unafikiri hirizi ambayo binti ya Palesa alivishwa mkononi ina madhara? Kwa nini?

  • Unafikiri Palesa alihitaji kufanya nini ili ajilinde dhidi ya roho waovu?

Sikuzote Wakristo wa kweli wamewapinga roho waovu. Soma Matendo 19:19 na 1 Wakorintho 10:21, kisha mzungumzie swali hili:

  • Kwa nini unapaswa kuharibu kitu chochote ulicho nacho ambacho kinahusiana na roho waovu?

Mwanamke akiharibu vitu mbalimbali vinavyotumiwa kuwasiliana na roho waovu kwa kuvichoma kwa moto.

6. Shinda vita dhidi ya Shetani na roho wake waovu

Shetani ndiye mtawala wa roho waovu. Lakini kiongozi wa malaika waaminifu anaitwa Mikaeli, ambalo ni jina lingine la Yesu. Mikaeli ana nguvu kadiri gani? Soma Ufunuo 12:7-9, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Ni nani mwenye nguvu zaidi? Je, ni Mikaeli na malaika zake au ni Shetani na roho wake waovu?

  • Je, unafikiri wafuasi wa Yesu wanapaswa kumwogopa Shetani na roho wake waovu?

Unaweza kushinda vita dhidi ya Shetani na roho wake waovu. Soma Yakobo 4:7, kisha mzungumzie swali hili:

  • Unawezaje kujilinda dhidi ya Shetani na roho wake waovu?

WATU FULANI HUSEMA: “Si vibaya kucheza michezo ya video au kutazama sinema zinazohusiana na roho waovu. Ni njia ya kujifurahisha tu.”

  • Kwa nini ni hatari kuwa na maoni kama hayo?

MUHTASARI

Malaika waaminifu hutusaidia. Shetani na roho wake waovu ni maadui wa Yehova, na wanatumia mazoea ya kuwasiliana na roho ili kuwapotosha watu.

Ungejibuje?

  • Malaika wa Yehova wanawasaidiaje watu wajifunze kumhusu?

  • Shetani na roho wake waovu ni nani?

  • Kwa nini unapaswa kujiepusha na mazoea ya kuwasiliana na roho waovu?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Chunguza uthibitisho unaoonyesha kwamba Yesu ndiye Mikaeli, yule malaika mkuu.

“Yule Malaika Mkuu Mikaeli Ni Nani?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Chunguza uthibitisho unaoonyesha kwamba Ibilisi si uovu tu ulio ndani yetu, bali ni kiumbe halisi.

“Je, Ibilisi Ni Kiumbe Halisi?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Ona jinsi mwanamke aliyesumbuliwa na roho waovu alivyowekwa huru.

“Alipata Kusudi Maishani” (Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 1993)

Jifunze jinsi Shetani anavyotumia mazoea ya kuwasiliana na roho waovu ili kuwadanganya watu.

“Ukweli Kuhusu Uchawi na Ulozi” (Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele, sehemu ya 5)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki