Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lff somo la 34
  • Tunaweza Kuonyeshaje Kwamba Tunampenda Yehova?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tunaweza Kuonyeshaje Kwamba Tunampenda Yehova?
  • Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Upendo Mshikamanifu wa Yehova Unamaanisha Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Jinsi Unavyoweza Kuwa Rafiki ya Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Yehova Anashangilia Katika Upendo Mshikamanifu—Namna Gani Wewe?
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Upendo wa Mungu Unadumu Milele
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
lff somo la 34
Somo la 34. Mwanamume aliye katikati ya jiji anatazama angani akiwaza.

SOMO LA 34

Tunaweza Kuonyeshaje Kwamba Tunampenda Yehova?

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Tangu ulipoanza kujifunza Biblia, je, upendo wako kwa Mungu umeongezeka? Je, ungependa kuendelea kuimarisha urafiki wako na Mungu? Ikiwa ndivyo, kumbuka kwamba Yehova anapoona upendo wako kwake ukizidi kuongezeka, ndivyo atakavyoendelea kukupenda na kukujali zaidi. Unawezaje kumwonyesha kwamba unampenda?

1. Tunawezaje kumwonyesha Yehova kwamba tunampenda?

Tunaonyesha kwamba tunampenda Yehova kwa kumtii. (Soma 1 Yohana 5:3.) Yehova hamlazimishi mtu yeyote amtii. Badala yake, amempa kila mmoja wetu nafasi ya kuamua ikiwa tutamtii au la. Kwa nini? Yehova anataka tuwe “watiifu kutoka moyoni.” (Waroma 6:17) Hilo linamaanisha kwamba anataka tumtii si kwa kulazimishwa, bali kwa sababu tunampenda. Sehemu ya 3 na ya 4 ya kitabu hiki imekusudiwa kukusaidia kuonyesha kwamba unampenda Yehova kwa kufanya mambo yanayomfurahisha na kuepuka mambo anayochukia.

2. Kwa nini inaweza kuwa vigumu kwetu kumpenda Yehova?

“Mwadilifu ana matatizo mengi.” (Zaburi 34:19) Sote tunapambana na hali yetu ya kutokamilika. Huenda pia tukakabili matatizo ya kiuchumi, ukosefu wa haki, na matatizo mengine. Tunapokabili matatizo, huenda isiwe rahisi kwetu kumtii Yehova. Kwa sababu matatizo yanaweza kufanya iwe vigumu kumtii Yehova. Lakini ikiwa utakuwa mwaminifu na kumtii Yehova, utaonyesha kwamba unampenda kuliko kitu kingine chochote. Na utathibitisha kwamba wewe ni mshikamanifu kwake. Naye atakuwa mshikamanifu kwako. Hatakuacha kamwe.​—Soma Zaburi 4:3.

CHIMBA ZAIDI

Chunguza kwa nini Yehova anafurahi unapomtii, na ujifunze jinsi unavyoweza kuendelea kuwa mwaminifu kwake.

3. Suala linalokuhusu

Katika kitabu cha Biblia cha Ayubu, Shetani alitokeza madai si dhidi ya Ayubu tu, bali pia dhidi ya kila mtu anayetaka kumtumikia Yehova. Soma Ayubu 1:1, 6–2:10, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Kulingana na madai ya Shetani, kwa nini Ayubu alimtii Yehova?​—Ona Ayubu 1:9-11.

  • Shetani anadai nini kuhusu wanadamu wote, kutia ndani wewe?​—Ona Ayubu 2:4.

Soma Ayubu 27:5b, kisha mzungumzie swali hili:

  • Ayubu alithibitishaje kwamba alimpenda sana Yehova?

Shetani akimpinga Yehova. Anatilia shaka utimilifu wa Ayubu, ambaye amejaa majipu, na utimilifu wa dada anayemtumikia Yehova leo.

Ayubu alithibitisha kwamba anampenda Yehova kwa kuendelea kuwa mshikamanifu kwake

Tunathibitisha kwamba tunampenda Yehova tunapoendelea kuwa washikamanifu kwake

4. Fanya moyo wa Yehova ushangilie

Soma Methali 27:11, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Yehova anahisije unapotenda kwa hekima na kumtii? Kwa nini?

5. Unaweza kuwa mshikamanifu kwa Yehova

Upendo wetu kwa Yehova hutuchochea kuwaambia wengine kumhusu. Ushikamanifu wetu kwake hutuchochea kufanya hivyo hata inapokuwa vigumu. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

VIDEO:Tetea Imani Yako Licha ya Upinzani (5:09)

  • Je, wakati mwingine ni vigumu kwako kuwaambia wengine kumhusu Yehova?

  • Katika video hiyo, ni nini kilichomsaidia Grayson ashinde woga wake?

Ni rahisi kuwa washikamanifu kwa Yehova ikiwa tunapenda mambo anayopenda na kuchukia mambo anayochukia. Soma Zaburi 97:10, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Kutokana na mambo uliyojifunza, ni baadhi ya mambo gani ambayo Yehova anapenda? Na anachukia mambo gani?

  • Unawezaje kujifunza kupenda mambo mazuri na kuchukia mambo mabaya?

6. Tunanufaika tunapomtii Yehova

Sikuzote kumtii Yehova ndilo jambo bora. Soma Isaya 48:17, 18, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Je, tunaweza kuwa na hakika kwamba sikuzote Yehova anajua jambo linalotufaa kabisa? Kwa nini?

  • Kufikia sasa, umenufaikaje kwa kujifunza Biblia na kumhusu Mungu wa kweli, Yehova?

WATU FULANI HUSEMA: “Mungu hajali ninachofanya.”

  • Unaweza kutumia andiko gani kuthibitisha kwamba matendo yetu yanaweza kumfurahisha au kumhuzunisha Yehova?

MUHTASARI

Unaweza kuonyesha kwamba unampenda Yehova kwa kumtii na kuendelea kuwa mshikamanifu kwake hata unapokabili changamoto.

Ungejibuje?

  • Mfano wa Ayubu umekufundisha nini?

  • Utathibitishaje kwamba unampenda Yehova?

  • Ni nini ambacho kitakusaidia uendelee kuwa mshikamanifu kwa Yehova?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Ona jinsi unavyoweza kuwa mshikamanifu kwa Yehova na kutaniko?

“Kwa Mtu Mshikamanifu Unatenda kwa Ushikamanifu” (16:49)

Jifunze kuhusu madai ya Shetani dhidi ya wanadamu.

“Ayubu Adumisha Utimilifu” (Biblia​—Ina Ujumbe Gani? sehemu ya 6)

Ona jinsi vijana na watoto wanavyoweza kuonyesha kwamba wanampenda Yehova.

Mfurahishe Yehova (8:18)

Vijana wanawezaje kuendelea kuwa washikamanifu kwa Mungu hata wanaposhinikizwa na vijana wenzao?

Simama Imara Unaposhinikizwa na Marafiki! (4:00)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki