Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lff somo la 36
  • Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote
  • Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
  • Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Kuna Faida ya Kuwa Mnyoofu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Faida ya Kuwa Mnyoofu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
lff somo la 36
Somo la 36. Mtu akitia sahihi kwenye stakabadhi.

SOMO LA 36

Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Sote tunapenda kuwa na marafiki wanyoofu. Yehova anataka rafiki zake wawe wanyoofu pia. Lakini si rahisi kuwa wanyoofu kwa sababu tunaishi katika ulimwengu uliojaa watu wasio wanyoofu. Kuna manufaa gani ya kuwa wanyoofu katika mambo yote?

1. Ni sababu gani muhimu zaidi ya kuwa wanyoofu?

Tunapowatendea wengine kwa unyoofu, tunamwonyesha Yehova kwamba tunampenda na tunamheshimu. Kumbuka kwamba Yehova anajua mambo yote tunayofikiria na kutenda. (Waebrania 4:13) Anaona tunapotenda kwa unyoofu na jambo hilo linamfurahisha. Neno lake linasema: “Yehova humchukia mtu mwenye hila, lakini ana urafiki wa karibu na watu wanyoofu.”​—Methali 3:32.

2. Tunawezaje kutenda kwa unyoofu katika maisha yetu ya kila siku?

Yehova anataka “kila mtu amwambie mwenzake ukweli.” (Zekaria 8:16, 17) Hilo linamaanisha nini? Iwe tunazungumza na watu wa familia yetu, wafanyakazi wenzetu, ndugu na dada zetu Wakristo, au maofisa wa serikali, hatusemi uwongo wala kutoa habari zinazopotosha. Watu wanyoofu hawawaibii au kuwapotosha watu wengine. (Soma Methali 24:28 na Waefeso 4:28.) Na wanalipa kodi zote wanazodaiwa. (Waroma 13:5-7) Kwa njia hizo na nyinginezo, “[tunajiendesha] kwa unyoofu katika mambo yote.”​—Waebrania 13:18.

3. Kuna manufaa gani za kuwa wanyoofu?

Tunapojulikana kuwa watu wanyoofu ni rahisi kwa watu wengine kutuamini. Pia, tunachangia hali ya usalama na upendo katika kutaniko. Tunafurahia dhamiri safi. Tunapokuwa wanyoofu, “[tunalipamba] fundisho la Mwokozi wetu, Mungu,” na tunawavuta watu wengine wajiunge nasi kumwabudu Yehova.​—Tito 2:10.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze kwa nini unyoofu ni jambo muhimu kwa Yehova, na jinsi unavyoweza kuwa mnyoofu katika hali mbalimbali maishani.

4. Unyoofu humfurahisha Yehova

Soma Zaburi 44:21 na Malaki 3:16, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Kwa nini si jambo la hekima kufikiri kwamba tunaweza kuficha ukweli?

  • Unafikiri Yehova anahisije tunapoamua kusema ukweli, hata inapokuwa vigumu kufanya hivyo?

Msichana mdogo akizungumza na baba yake ambaye amekunja goti ili amtazame binti yake. Glasi iliyoanguka mezani na kinywaji kikiwa kimemwagika chini.

Watoto wanaposema ukweli wanawafurahisha wazazi wao. Tunaposema ukweli tunamfurahisha Yehova

5. Tenda kwa unyoofu nyakati zote

Watu wengi hufikiri kwamba haiwezekani kuwa mnyoofu nyakati zote. Hata hivyo, chunguza kwa nini tunapaswa kuwa wanyoofu kila wakati. Onyesha VIDEO.

VIDEO: Ni Mambo Gani Yanayoleta Shangwe?​—Dhamiri Safi (2:32)

Picha za video ‘Ni Mambo Gani Yanayoleta Shangwe?​—Dhamiri Safi.’ Baada ya Ben kumwambia mwajiri wake kwamba alikosea, wanasalimiana.

Soma Waebrania 13:18, kisha mzungumzie jinsi tunavyoweza kuwa wanyoofu . . .

  • katika familia.

  • kazini au shuleni.

  • katika hali nyingine.

6. Tunanufaika tunapokuwa wanyoofu

Nyakati nyingine tunaweza kupatwa na matatizo kwa sababu ya kuwa wanyoofu. Lakini ukweli ni kwamba tutanufaika tunapokuwa wanyoofu sikuzote. Soma Zaburi 34:12-16, kisha mzungumzie swali hili:

  • Unyoofu unaweza kukusaidiaje kuwa na maisha bora?

A. Mume na mke wakizungumza wakiwa wanakunywa kahawa. B. Fundi wa magari akipongezwa na mwajiri wake kazini. C. Mwanamume aliye kwenye gari lake akimwonyesha leseni afisa wa polisi.
  1. Waume na wake wanyoofu huimarisha ndoa zao

  2. Wafanyakazi wanyoofu huaminiwa na waajiri wao

  3. Raia wanyoofu huheshimiwa na maofisa wa serikali

WATU FULANI HUSEMA: “Uwongo mdogo ni jambo la kawaida.”

  • Kwa nini unaamini kwamba Yehova anachukia uwongo wa kila aina?

MUHTASARI

Yehova anataka rafiki zake wawe wanyoofu katika mambo yote wanayosema na kutenda.

Ungejibuje?

  • Tunaweza kuwa wanyoofu katika njia gani?

  • Kwa nini si jambo la hekima kufikiri kwamba tunaweza kuficha ukweli?

  • Kwa nini ungependa kuwa mnyoofu nyakati zote?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Wazazi wanaweza kuwasaidiaje watoto wao wawe wanyoofu?

Sema Kweli (1:44)

Tunapata manufaa gani tunapotimiza ahadi zetu?

Timiza Ahadi, Upate Baraka (9:09)

Chunguza kwa nini tunapaswa kulipa kodi hata kama zinatumiwa vibaya.

“Je, Ni Lazima Ulipe Kodi?” (Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 2011)

Nini kilichomchochea mwanamume fulani asiye mnyoofu abadili maisha yake?

“Nilijifunza Kwamba Yehova Ni Mwenye Rehema na Mwenye Kusamehe” (Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 2015)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki