Utii
Kwa nini ni muhimu kutii?
Kut 19:5; Kum 10:12, 13; Mhu 12:13; Yak 1:22
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Sa 15:17-23—Nabii Samweli anamkemea Mfalme Sauli kwa kutomtii Yehova; kisha Samweli anakazia umuhimu wa kutii
Ebr 5:7-10—Ingawa sikuzote Yesu amekuwa Mwana mkamilifu wa Mungu, alijifunza kuwa mtiifu alipotendewa kwa njia isiyofaa akiwa duniani
Mkristo anapaswa kufanya nini ikiwa wanadamu wenye mamlaka wanamwambia asimtii Mungu?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Da 3:13-18—Hata walipohatarisha uhai wao, Waebrania watatu waaminifu walikataa kuinamia sanamu iliyosimamishwa na Mfalme Nebukadneza
Mt 22:15-22—Yesu anaeleza kwamba wafuasi wake wanawatii wenye mamlaka isipokuwa tu wenye mamlaka wawaambie wasimtii Yehova Mungu
Mdo 4:18-31—Hata walipoamriwa na wenye mamlaka waache kuhubiri, mitume waliendelea kuhubiri kwa ujasiri
Ni lazima tufanye nini ikiwa tunataka kuendelea kutii amri za Yehova?
Kum 6:1-5; Zb 112:1; 1Yo 5:2, 3
Tazama pia Zb 119:11, 112; Ro 6:17
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Ezr 7:7-10—Kuhani mwaminifu Ezra anatayarisha moyo wake ili aweze kuweka mfano mzuri wa kutii amri za Mungu na kuwafundisha wengine
Yoh 14:31—Yesu anafunua kwa nini anatenda kama vile Baba yake alivyomwamuru
Ni nini kinachopaswa kutuchochea kumtii Yehova na Yesu?
Utii wetu unaonyeshaje imani yetu?
Ro 1:5; 10:16, 17; Yak 2:20-23
Tazama pia Kum 9:23
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 6:9-22; Ebr 11:7—Noa anaonyesha imani yake kwa kujenga safina kama tu Yehova anavyomwamuru, ‘ndivyo anavyofanya’
Ebr 11:8, 9, 17—Abrahamu anaonyesha imani yake kwa kutii amri za Yehova, kutia ndani kuondoka Uru, na kumtoa mwana wake
Yehova anatupa baraka gani tunapotii?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Law 26:3-6—Yehova anaahidi kuwabariki na kuwatunza wale wanaomtii
Hes 13:30, 31; 14:22-24—Kalebu anaonyesha roho ya utii, na hivyo anapata baraka za Yehova
Ni nini kitakachotokea tusipotii?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 2:16, 17; 3:17-19—Kwa sababu hawamtii Yehova Mungu, Adamu na Hawa wanapoteza Paradiso, ukamilifu, na uzima wa milele
Kum 18:18, 19; Mdo 3:12, 18, 22, 23—Yehova anatabiri kuja kwa Nabii mkuu zaidi ya Musa na kufunua kwamba kutomtii Nabii huyo kutasababisha matokeo mabaya sana
Yud 6, 7—Malaika waasi na watu wa Sodoma na Gomora wanamkasirisha Yehova kwa sababu ya kutotii
Kwa nini tunapaswa kumtii Yesu Kristo?
Simulizi la Biblia linalohusika:
Yoh 12:46-48; 14:24—Yesu anaeleza kwamba kutotii maneno yake kutaongoza kwenye hukumu kali
Kwa nini Wakristo wanawatii wale wanaoongoza kutanikoni?
Kwa nini mke Mkristo anapaswa kujitiisha kwa mume wake?
Kwa nini watoto wawatii wazazi wao?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 37:3, 4, 8, 11-13, 18—Kijana Yosefu anamtii baba yake na kusafiri kwenda kuwaona ndugu zake hata ingawa wanamchukia
Lu 2:51—Yesu anaendelea kuwatii Yosefu na Maria hata ingawa yeye ni mkamilifu na wazazi wake wa kibinadamu si wakamilifu