Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • scl kur. 38-39
  • Kupenda Mali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kupenda Mali
  • Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
scl kur. 38-39

Kupenda Mali

Je, Biblia inafundisha kwamba ni vibaya kuwa na pesa au vitu vya kimwili?

Mhu 7:12

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Fa 3:​11-14—Yehova anambariki Mfalme Sulemani kwa kumpatia utajiri mwingi kwa sababu ni mnyenyekevu

    • Ayu 1:​1-3, 8-10—Ingawa Ayubu alikuwa na mali nyingi sana, alijulikana zaidi kwa kuwa mtu mtimilifu

Kwa nini kuwa na mali na utajiri hakutufanyi turidhike au kuwa na amani ya akili?

Met 23:​4, 5; Mhu 2:​18, 19; 5:​10, 12

Ni wakati gani utajiri hauwezi kutusaidia hata kidogo?

Zb 49:​6, 7, 9, 10; Mt 16:26

Ni hatari gani kubwa zaidi inayoletwa na pesa na mali?

Kum 6:​10-12; Mt 6:24; 1Ti 6:​9, 10

Nguvu za utajiri zinawezaje kutudanganya?

Met 11:​4, 18, 28; 18:11; Mt 13:22

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Mdo 8:​18-24—Kwa upumbavu Simoni anaamini kwamba anaweza kutumia pesa kununua pendeleo katika kutaniko la Kikristo

Kupenda pesa kunaweza kutugharimu nini?

Mt 6:​19-21; Lu 17:​31, 32

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mk 10:​17-23—Mwanamume kijana tajiri ambaye anapenda sana mali zake anapoteza pendeleo la kuwa mfuasi wa Yesu

    • 1Ti 6:​17-19—Mtume Paulo anawaonya Wakristo matajiri waepuke majivuno, ambayo yanaweza kufanya wapoteze kibali cha Mungu

Kupenda mali kunawezaje kudhoofisha imani yetu na kusababisha tupoteze kibali cha Mungu?

Kum 8:​10-14; Met 28:20; 1Yo 2:​15-17

Tazama pia Zb 52:​6, 7; Amo 3:​12, 15; 6:​4-8

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Ayu 31:​24, 25, 28—Ayubu anaona waziwazi hatari ya kutumaini mali, kwa sababu kufanya hivyo ni kama kumkana Mungu

    • Lu 12:​15-21—Yesu anatoa onyo kuhusu kupenda mali kwa kumzungumzia mwanamume tajiri ambaye si tajiri kwa Mungu

Tunawezaje kuridhika na vitu tulivyo navyo?

Met 30:​8, 9; 1Ti 6:​6-8; Ebr 13:5

Ni hazina gani ambazo ni muhimu zaidi kuliko vitu vya kimwili, na kwa nini?

Met 3:​11, 13-18; 10:22; Mt 6:​19-21

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Hag 1:​3-11—Kupitia nabii Hagai, Yehova anaeleza kwamba anawanyima watu Wake hata baraka za kimwili kwa sababu wanatanguliza nyumba zao na starehe badala ya kujenga upya hekalu Lake takatifu

    • Ufu 3:​14-19—Yesu analikemea kutaniko la Laodikia kwa kutanguliza mali badala ya kuthamini zaidi utumishi wao kwa Mungu

Kwa nini tunapaswa kutumaini kwamba Yehova atatuandalia mahitaji yetu ya kimwili?

Zb 37:25; Met 3:​9, 10; Mt 6:​25-33

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki