Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w11 5/1 uku. 9
  • Unabii wa 6. Kazi ya Kuhubiri Katika Dunia Yote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unabii wa 6. Kazi ya Kuhubiri Katika Dunia Yote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari Zinazolingana
  • “Nendeni Mkafanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Ni Nani Wanaohubiri Habari Njema?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Jinsi Habari Njema Inavyohubiriwa
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Wanahubiri Nyumba kwa Nyumba?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 5/1 uku. 9

Unabii wa 6. Kazi ya Kuhubiri Katika Dunia Yote

“Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote.”—MATHAYO 24:14.

● Vaiatea anaishi kwenye kisiwa kimoja kati ya visiwa vya mbali vya Tuamotu, katika bahari ya Pasifiki. Ingawa visiwa vya Tuamotu ambavyo ni 80 hivi, vimesambaa katika eneo lenye ukubwa wa kilomita 802,900 za mraba, vina watu wapatao 16,000 tu. Hata hivyo, Vaiatea na jirani zake wametembelewa na Mashahidi wa Yehova. Kwa nini? Kwa sababu Mashahidi wangependa kuwahubiria watu wote habari njema kuhusu Ufalme wa Mungu—hata wawe wanaishi wapi.

MAMBO ya HAKIKA YANAONYESHA NINI? Ujumbe wa Ufalme unaenezwa katika pembe zote za dunia. Katika mwaka wa 2010 pekee, Mashahidi wa Yehova walitumia muda wa saa bilioni 1.6 wakitangaza habari njema katika nchi 236. Kwa hiyo, kila Shahidi alihubiri muda wa dakika 30 hivi kila siku. Katika miaka kumi iliyopita, wametayarisha na kugawa vifaa zaidi ya bilioni 20 vya kuwasaidia watu kuielewa Biblia.

NI KIPINGAMIZI GANI KINACHOTOLEWA MARA NYINGI? Ujumbe wa Biblia umehubiriwa kwa maelfu ya miaka.

JE, KIPINGAMIZI HICHO KINA MSINGI? Ni kweli kwamba watu wengi wamehubiri ujumbe fulani wa Biblia. Hata hivyo, wengi wamefanya hivyo kwa muda mfupi na kwa kiwango kidogo. Kinyume cha hilo, Mashahidi wa Yehova wanashiriki katika kazi iliyopangwa vizuri ya kuhubiri duniani kote, na wameweza kuwafikia mamilioni ya watu. Mashahidi wameendelea na kazi yao ya kuhubiri ingawa wamekabili upinzani kutoka kwa mashirika yenye nguvu na yenye ukatili zaidi katika historia ya wanadamu.a (Marko 13:13) Zaidi ya hayo, Mashahidi wa Yehova hawalipwi ili kuhubiri. Badala yake, wanatumia wakati wao kuhubiri, na wanatoa machapisho yao bila malipo. Kazi yao yote inategemezwa kwa michango ya hiari.

UNA MAONI GANI? Je, “habari njema ya ufalme” inahubiriwa katika dunia yote? Je, kutimia kwa unabii huo kunaweza kumaanisha kwamba kuna mambo mazuri yatakayotokea hivi karibuni?

[Maelezo ya Chini]

a Kwa habari zaidi, tazama video hizi tatu: “Faithful Under Trials,” “Purple Triangles,” na “Jehovah’s Witnesses Stand Firm Against Nazi Assault,” ambazo zimetolewa na Mashahidi wa Yehova.

[Blabu katika ukurasa wa 9]

“Maadamu Yehova hajaleta mwisho huo, tutaendelea kuhubiri habari njema ya Ufalme kwa bidii, tukifanya yote tuwezayo ili kuwafikia watu katika maeneo yetu.”​—2010 KITABU CHA MWAKA CHA MASHAHIDI WA YEHOVA.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki